SIMBA SPORT CLUB WAKUSOGEZEA KARIBU JEZI NA VIFAA VYA SIMBA MAHALI ULIPO

Upatikanaji wa jezi na vifaa vya Simba wasogezwa karibu
Klabu ya Simba leo imeanza rasmi utekelezaji wa kampeni yake ya uuzwaji wa jezi pamoja na vifaa mbalimbali venye chapa ya Simba, ikiwa na dhumuni la kukuza mapato kwa timu kwa kupitia wanachama na wadau wa Simba kununua bidhaa mbalimbali zenye chapa ya Simba, kupeleka huduma ya vifaa vinavyotolewa na duka rasmi la Simba karibu zaidi na wanachama na wapenzi wa Simba. Katika zoezi hili ambalo utaweza kununua jezi kwa Tsh. 15, 000/= ambapo yoyote atakaenunua atapata picha kubwa ya timu bure.
Kwenye mechi na watani wa jadi wetu Yanga siku ya Jumamosi, kikosi cha Simba kitavaa jezi nyeupe ambazo zitakuwa zikipatikana kwenye duka la Simba linalotembea katika mitaa mbalimbali yaani Mobile Shop.
Akizungumza na Simbasports.co.tz leo asubuhi wakati zoezi hili lilipoanza Rais wa Simba Evans Aveva alisema “ leo tunaanza rasmi zoezi letu la kutembea mtaa kwa mtaa kwenye kampeni yetu ya uuzwaji wa jezi pamoja na vifaa mbalimbali venye chapa ya Simba kwa kutumia duka linalotembea “Mobile Shop” zoezi hili ni maalumu kwa ajili ya kusogeza upatikanaji wa vifaa na jezi za Simba kwa karibu zaidi, lakini pia itahamasisha wanachama na wapenzi wa Simba kuchangia timu yao”
Tunatambua kwamba wanachama na wapenzi wa Simba waliopo mikoni wangependa zoezi hili lifike na mikoani  na punde tu tutakuwa na utaratibu wa jinsi Duka letu la Simba Sports Shop litakavyoweza kupeleka huduma katika mikoa mbalimbali Tanzania, aliongeza Rais wa Simba Evans Aveva.
Akizungumza mkurugenzi wa kampuni ya EAG Group Imani Kajula ambao ni washauri na watekelezaji wa masuala ya masoko ya klabu ya Simba alisema “zoezi hili litakuwa endelevu ambapo tutaendelea kubuni njia mbalimbali za kuwafikia watu waliopo mikoani nje ya Dar es Salaam ambapo kwa sasa wanaweza kupata jezi rasmi ya Simba kwenye duka mtandao la Simba kupitia Jumia www.jumia.co.tz na jezi zitawafikia popote walipo Tanzania”.

Simbasports.co.tz inaupongeza uongozi wa Simba SC pamoja na wasimamizi wa Duka la Simba Simba Sports Shop kwa ubunifu huu katika kuleta maendeleo ya klabu ya Simba.

Comments

Popular posts from this blog