Ni vitu vidogo lakini ukivizingatika kila asubuhi utakuwa na furaha siku nzima


Wimbo wa Happy wa Pharrell Williams ulikuwa moja ya nyimbo ninazosikiliza kila ninapo amka asubuhi, kwanini sababu ni siku mpya na nilitaka kuanza na furaha kama jina la nyimbo. Je, wewe unafanya nini cha kwanza unapoamka asubuhi.? Kuna vitu vidogo sana unaweza ukawa unafanya kila siku na ukajisikia mwenye furaha na ukaanza siku yako vizuri

Usizime Alarm (kengere).

Kuna wakati unahitaji kitu cha kukufanya uamke muda unaopanga wewe asubuhi. Kengere ya simu au saa ya mezani, inapoita wengi wetu sababu ya usingizi mwingi tunaizima na kuendelea na usingizi,  kwa dakika chache,  ila ni vizuri kama ulipanga kuamka muda huo basi na uamke . panga ratiba yako na uizoe.

Tafuta Ujumbe wa kukupa moyo.

Kuna wakati tunahitaji mtu wa kutuambia tunaweza,weka chumbani kwako ujumbe mzuri wa kukupa moyo kama “You’re the Best” au unaweza ukaingia Google na kutafuta “inspiration quotes” hizi ni nikuu za watu mbalimbali, ambazo unaweza kusoma kila unapo amka uanze na siku mpya.kila siku mpya ni zawadi na unatakiwa uwe na mwanzo mpya sababu siku hazifanani.

Kaa mbali na tekinologia kwa muda wa saa moja.

Hapa naongelea Tv,radio au simu.  Simu ni kitu cha kwanza mtu akiamka anashika asome ujumbe, aingie kwenye mitandao ya kijamii  Facebook,Twitter and Instagram si kitu kibaya kwenda na wakati nakujua nini kinaendela duniani, lakini chukua muda wa saa moja fanya mambo mengine na ufanye kama unahisahau simu kwa muda.

Fanya mazoezi.

Kuna watu wanasingizia muda inapokuja swala la mazoezi, please,  dakika 20 tu zinatosha kufanya mazoezi ukiwa nyumbani, sijui watu wengine wanatumiaje mitandao ya kijamii, kama instagram na Youtube kuna video zinaonyesha aina ya mazoezi unaweza ukafanya ukiwa nyumbani hii ni rahisi kwa mtu yoyote kufanya mazoezi akiwa nyumbani, mazoezi yanasaidia kupunguza stress na kusaidia mzunguko wa damu.

Pata kifungua kinywa.

Kwa kawaida tunakula mara 3 kwa siku ila kwa mara zote 3, kifungua kinywa ndo mlo wa muhimu kuliko yote, pata chai au kikombe cha kahawa kila siku asubuhi hautojuta,

Pangilia Ratiba yako ya siku.

Hili ni tatizo kwa wengi , mtu anaanza siku kama zali tu hajui anaanza na nini au wapi anaanza siku yake na kama ni mtu anafanya kazi ofisini hata hajui anaanza na kazi gani akifika ofisini,lazima uwe na ratiba  ujue unaanza na nini na unamaliza na nini. Hii itakufanya ufanye mambo yako kimpangilio zaidi.

Wajibika.

Wajibika katika majukumu yako,ukiwa na kazi ni rahisi kuona siku inaisha kirahisi na haraka uwe mama wa nyumbani, unafanyakazi ofisini ama we ni kaka muuza genge zote kazi cha msingi ni kujari muda na kupenda kazi yako ukiwa mtu wa kuwajibika hautokuwa na muda wa kufanya vitu visivyo na maana au kama mwanamke kujiingiza katika matatizo au vikundi vya kimbea.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Comments

Popular posts from this blog