Kajala sasa ajis’tukia kuzeeka

Kajala-1Na Imelda Mtema
Staa wa Filamu Bongo, Kajala Masanja amesema kuwa mambo ya kimjini kama wafanyavyo mastaa wengine kwa sasa ameyapa mgongo kwa madai kuwa anaona anaelekea kuzeeka.
Akizungumza na mwandishi wa habari hii hivi karibuni, Kajala alisema kila anapojiangalia anaona kabisa alivyokuwa zamani sivyo alivyo sasa hivyo ana kila sababu ya kubadilika.
“Kiukweli najiona kabisa naelekea kuzeeka, ule usichana unapotea hivyo ni vyema sasa mambo mengine ya kimjini nikayapa kisogo. Kwenda klabu usiku nimepunguza na kuna siku nitaacha kabisa, nguo za ajabuajabu najifikiria mara mbilimbili,” alisema Kajala.

Comments

Popular posts from this blog