SAMATA: TUNGEKUWA MAKINI TUNGESHINDA KWA IDADI KUBWA YA MAGOLI
Mbwana Samata
Baada ya
kufanikiwa kuifungia Stars goli moja kwenye ushindi wa goli 2-0
ilioupata Stars ikiwa nyumbani dhidi ya Malawi, Mazembe Mbwana ambaye ni
nyota wa Tanzani anaecheza TP Mazembe amesema, kama wachezaji wa Stars
wangekuwa makini basi wangeweza kufunga magoli mengi zaidi kwenye mchezo
huo.
Samata
amesema ilikuwa ni rahisi kupata magoli mengi hasa kipindi cha kwanza
lakini Malawi walirudi tofauti kipindi cha pili. Samata ameongeza kuwa,
Stars inaweza kufuzu kwa hatua inayofuata kwasababu anaamini walimu
wameona makosa yaliyojitokeza kwenye mchezo wa Jumatano na watafanya
marekebisho kabla ya mechi ya marudiano siku ya Jumapili itakayochezwa
nchini Malawi.
“Kama
tungekuwa makini, tungeweza kushinda kwa idadi kubwa ya magoli lakini
sijui tulikuwa na uoga wa kudhani mechi inaweza kuwa ngumu zaidi ya
ilivyokuwa. Kipindi cha pili jamaa wakaja wamebadilika kwasababu
walikuwa wanaona kwamba matokeo yanaweza kuwa mabaya zaidi kwao”,
amesema Samata ambaye alifunga goli la kwanza wakati Stars ikiibuka na
ushindi wa goli 2-0 dhidi ya Malawi.
“Ilikuwa
rahisi kupata magoli mengi kipindi cha kwanza, lakini tushukuru kwa
ushindi huu tulioupata kwasababu hii ni game huwezi jua, tuache tu
ushindi ubakie hivyo”.
“Nadhani
hata kwa goli hizi mbili nadhani wanashukuru wanadhani wanawea
wakabadili matokeo wakiwa kwao. Lakini sisi tunaweza ku-qualify,
nafikiri walimu wameona wapi tunatakiwa kurebisha na kupata matokeo
mazuri Jumapili tukiwa Malawi”.
Comments
Post a Comment