MEMPHIS DEPAY AFANYA MAAMUZI MAGUMU NDANI YA OLD TRAFFORD

Mchezaji mpya wa Manchester United, Memphis Depay ameamua kuchukua maamuzi magumu ya kuvaa viatu vizito kwa kuomba kuvaa jezi namba 7 katika msimu huu wa ligi kuu ya Uingereza unaoanza Jumamosi hii.
Hiyo ni jezi ya heshima kwa Old Trafford ambapo iliwahi kuvaliwa na masupastaa waliochezea klabu hiyo wakiwemo George Best, Bryan Robson, Eric Cantona, David Beckham, Cristiano Ronaldo na Angel di Maria.
Hata hivyo kocha wa United, Louis van Gaal bado hajatoa namba katika kikosi chake.

Comments

Popular posts from this blog