FILIKUNJOMBE APITA BILA KUPINGWA WAPINZANI WAKE WAINGIA MITINI NA FOMU ,MGOMBEA WA CHADEMA ASHINDWA KUJAZA TAREHE NA KUTORUDISHA FOMU MMOJA‏

fomu ya mgombea wa Chadema ubunge Ludewa zikiwa hazijatimia baada ya tomu ya tamko kukosekana
Fomu ya mgombea wa Chadema ikiwa haijazwa senemu ya tarehe ,mwezi na mwaka
Mzee Kada wa Chadema akimpongeza mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe baada ya kupewa barua ya kupita bila kupingwa
Mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe akizungumza na wanachama wa CCM na wananchi wa Ludewa baada ya kupita bila kupingwa
Filikunjombe akionyesha barua ya kupita bila kupingwa
Msimamizi wa uchaguzi jimbo la Ludewa Bw Wiliam Waziri akimpongeza mbunge Filikunjombe baada ya kumkabidhi barua ya kupita bila kuingwa ubunge jana 
Na Matukiodaima Blog


ALIYEKUWA mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe (CCM) amepita bila kupingwa baada ya mgombea wa chama cha Demokrasia na maendeleo (chadema) Barthomew Mkinga kushindwa kutimiza Masharti na Taratibu za Ujazaji wa Fomu.
Msimamizi wa Uchaguzi Wilaya ya Ludewa Bw Wiliam Waziri alisema jana kuwa Mgombea wa Chadema ameshindwa kutimiza taratibu za ujazaji wa fomu hizo hivyo kukosa sifa ya kuwa Mgombea wa Ubunge hivyo kumkabidhi barua rasmi Filikunjombe ya kupita bila kupingwa
Waziri alisema kwamba Kati ya wagombea wanne waliochukua fomu aliyetimiza taratibu ni Mgombea wa CCM, Bw. Filikunjombe pekee;
Kuwa Wagombea wa DP na TLP walishindwa kabisa kurejesha fomu huku Mgombea wa Chadema akishindwa kujaza fomu vizuri na kushindwa kurejesha Fomu ya Kiapo cha Maadili ya Sheria za Uchaguzi.
Mgombea huyo wa Chadema aliyereja fomu ya wadhamini bila kujaza tarehe ,mwezi wala mwaka ambao uchaguzi mkuu utafanyika .
Kwa upande wake mgombea ubunge wa TLP Bw Blanka Haule alisema kuwa alishindwa kurejesha fomu hizo kwa wakati kutokana kukosa picha za kubandika katika fomu hiyo kutokana na hali ya mazingira ya Ludewa kukowa eneo la kupiga picha hizo.
Kwani alisema picha ambazo alipiga Njombe alizisahau alikoziweka hivyo kulazimika kwenda kupiga pich nyingine za haraka kwa muda wa dakika tatu ila cha kushangaza dakika tatu za kutoka picha hizo zilionekana kushindwa kutoka kwa wakati na kutoka saa 11 jioni .
“Nilijipanga kugombea ubunge ili kumpokea ubunge Deo Filikunjombe na kuendeleza yale yote aliyoyafanya jimboni ila watu wa picha walinikwamisha na kushindwa kupata picha kwa wakati hivyo kwa sasa ndio basi tena japo ilikuwa ni Demokrasia lakini kapita bila kupingwa ndio mbunge wetu:”
Akizungumzia hatua ya mgombea wao wa Chadema kushindwa kukamilisha taratibu za ujazaji wa fomu hizo Bw Daniel Songo alisema kuwa mgombea wao hakuwa makini hata kidogo kwani alikuwa ni mtu ambae hakutulia na muda mwingi alikuwa akifikiria juu ya wanachama wanaohama chama na kuacha kutulia katika kujaza fomu hizo .
Japo alisema chama hicho kimepoteza umaarufu kutokana na mwenendo wa viongozi wa juu wa chama hicho kuendekeza siasa za ukanda zaidi na kuacha kutazama uhai wa chama hicho.
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Ludewa Stanle Kolimba alisema kuwa amepokea kwa furaha kubwa hatua ya mgombea wake wa nafasi ya ubunge kupita bila kupingwa na kuwa kazi kubwa kwa sasa kuhakikisha mgombea urais wa CCM Dr John Magufuli anapata kura za kimbunga pamoja na kupigania kata zote kuona CCM .
Kwa upande wake Bw Filikunjombe akizungumzia hatua hiyo ya kupita bila kupingwa alisema ameipokea kwa vizuri sana kwa alitegemea wapinzani hao wajitokeze ili aweze kuwaonyesha kazi kwa kuhakikisha wanaangukia pua katika uchaguzi huo .
Alisema kazi kubwa ya maendeleo ambayo ameifanya katika jimbo hilo kwa miaka mitano na imani kubwa ambayo wananchi wa Ludewa wanayo dhidi yake ilikuwa ni vigumu kwa wapinzania hao kupata kura Ludewa.
Bw Filikunjombe aliwaomba wananchi wa Ludewa kura zote ambazo walipanga kumpigia yeye kuzielekeza kwa mgombea Urais Dr Magufuli na kwa madiwani wa CCM na furaha yake kuona wapinzani wanaambulia patupu katika wilaya ya Ludewa

Comments

Popular posts from this blog