DKT JOHN POMBE MAGUFULI ATIKISA JIMBONI KWAKE CHATO,WANANCHI WAIBUA SHANGWE KILA KONA YA MJI

  Mbunge wa Chato na Mgombea Urais kwa chama cha Mapinduzi 
CCM,Dkt John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa mji huo waliojitokeza kwa wingi kumlaki,mara baada ya kuwasili leo jioni mjini humo akitokea mkoani Mwanza ambako nako alipita kujitambulisha na kuwashukuru wakazi wa jiji hilo ambao nao walijitokeza kwa wingi. 
Kufuatia ujio wa Dkt Magufuli ndani ya mji wa Chato kuliibuka shamra shamra za mapokezi zilizokuwa zikirindima kila pande wakifurahia uteuzi wa CCM kwa Dkt Magufuli.

Baadhi
ya Wananchi wa Wilaya ya Chato na vitongoji vyake waliokuwa 
wamekusanyika kwenye kituo cha mabasi wilayani humo wakishangilia kwa 
furaha kubwa mara baada ya Mbunge wao na Mgombea Urais kwa chama cha 
Mapinduzi 
CCM,Dkt John Pombe Magufuli kujitambulisha kwao.
 Baadhi
ya Wananchi wa Wilaya ya Chato na vitongoji vyake wakiwa wamejitokeza 
kwa wingi kumlaki Mbunge wao na Mgombea Urais kwa chama cha Mapinduzi 
CCM,Dkt John Pombe Magufuli mara baada ya kuwasili leo jioni mjini humo 
na shamra shamra za mapokezi kurindima kila kona wakifurahia uteuzi wa 
CCM kwa Dkt Magufuli,huku wengine wakiwa wamebeba mabango kama hivyo 
pichani.

 
Mbunge wa Chato na Mgombea Urais kwa chama cha Mapinduzi 
CCM,Dkt John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa mji huo waliojitokeza
kwa wingi kumlaki,mara baada ya kuwasili leo jioni mjini humo akitokea 
mkoani Mwanza ambako nako alipita kujitambulisha na kuwashukuru wakazi 
wa jiji hilo ambao nao walijitokeza kwa wingi. 
Kufuatia ujio wa Dkt Magufuli ndani ya mji wa Chato kuliibuka shamra 
shamra za mapokezi zilizokuwa zikirindima kila pande wakifurahia uteuzi 
wa 
CCM kwa Dkt Magufuli.
 Naibu
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Luhavi akiwasalimia wachama wa CCM pamoja na 
Wananchi waliofika kumlaki Dkt Magufuli jioni ya leo katika kituo cha 
mabasi cha zamani ndani ya wilaya hiyo.
 Ilikuwa ni shangwe tu jioni ya leo ndani ya Wilaya ya Chato ambako ndiko nyumbani kwa Mbunge na  Mgombea Urais kwa chama cha Mapinduzi 
CCM,Dkt John Pombe Magufuli. 

   Mbunge wa Chato na Mgombea Urais kwa chama cha Mapinduzi 
CCM,Dkt John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa mji  wa Katoro mkoani Geita alipokuwa akipita njiani kuelekea wilayani Chato.Kufuatia ujio wa Dkt Magufuli mkoani humo wananchi walijitokeza kwa wingi kila baada ya kilometa kadhaa na kuziba barabara wakita kumuona Dkt Magufuli na kumpongeza kwa kuchaguliwa kwake na chama cha CCM.
 Mwananchi
akiwa amekumbwa na joto la furaha mara baada ya kumuona Dkt Jonh 
Magufuli akiwa na msafara mzima wakielekea jimboni kwake Chato mkoani 
Geita.
Mkuu
wa Mkoa wa Mwanza Mh.Magesse Mulongo akiwasalimia wananchi wa Chato 
jioni ya leo,kabla ya kumkaribisha Dkt John Magufuli aliyewasili mjini 
humo jioni ya leo akitokea mkoani Mwanza akijitambulisha kwa wananchi na
kuwashukuru. 


 Dkt Magufuli akizungumza jambo kwa maelfu ya wakazi wa mji wa Chato jioni ya leo

 Dkt Magufuli akifurahia jambo mbele ya umati wa watu,mara baada ya kujitambulisha kwao. 

 
Mgombea Urais kwa chama cha Mapinduzi 
CCM,Dkt John Pombe Magufuli akiwashukuru wakazi wa mji huo kwa 
kujitokeza kwa wingi kumlaki,mara baada ya kuwasili leo jioni mjini humo
akitokea mkoani Mwanza ambako nako alipita kujitambulisha na 
kuwashukuru wakazi wa jiji hilo ambao nao walijitokeza kwa wingi. 
Kufuatia ujio wa Dkt Magufuli ndani ya mji wa Chato kuliibuka shamra 
shamra za mapokezi zilizokuwa zikirindima kila pande wakifurahia uteuzi 
wa 
CCM kwa Dkt Magufuli. 




 Maelfu ya Watu walijitokeza kumlaki Dkt Magufuli jioni ya leo mjini Chato



  Mgombea Urais kwa chama cha Mapinduzi 
CCM,Dkt John Pombe Magufuli akiwaaga Wananchi wa Chato waliojitokeza kwa wingi kumlaki,mara baada ya kumaliza kujitambulisha na kuwashukuru kwa kiasi kikubwa kwa kuchaguliwa kwake katika nafasi ya kupeperusha bendera ya chama chake kuwania nafasi ya Urais .PICHA NA MICHUZI JR-CHATO-GEITA.

Comments

Popular posts from this blog