BREAKING NEWS : LOWASSA ATAJA SIKU RASMI YA KUAMIA CHADEMA


Zipo tetesi kwamba Edward Lowasa, Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya ufisadi wa Richmond anatarajia kuzungumza na waandishi wa habari Jumapili tarehe 26 Julai 2015 Jijini Dar es Salaam. Katika mkutano huo, Lowasa anatarajiwa kueleza mambo mengi juu ya mchakato wa uchaguzi ndani ya CCM uliopelekea jina lake kukatwa.

Pia katika mkutano huo, Lowasa anatarajiwa kutangaza rasmi kujivua uanachama wake ndani ya CCM na kujiunga na CHADEMA ambapo baadaye jioni ataelekea viwanja vya Mwembeyanga ambako ataungana na viongozi wengine wa CHADEMA kwenye mkutano wa hadharaza. Mtakumbuka kuwa uwanja huo wa Mwembeyanga uliopo Temeke Dar es Salaam ulitumika kutaja orodha ya mafisadi 11 na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Wilbroad Slaa mwaka 2007 ambapo jina la Lowasa lilikuwa miongoni mwa majina yaliyopo kwenye orodha hiyo.

Uamuzi wa Lowasa kwenda CHADEMA umetokana na kutimiza makubaliano ya kupeleka shilingi bilioni 10 ambapo fedha hizo zimekabidhiwa Jana Alhamis Tarehe 23 Julai 2015. Aliyekabidhi fedha hizo kwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe ni Apson Mwang'onda na makabidhiano yamefanyika kwenye Hotel ya Sea Cliff huku tukio hilo likishuhudiwa na Kingunge Ngombale Mwiru na wengine ambao sitawataja kutokana na sababu maalum.


Taarifa zinasema kuwa kumekuwa na shinikizo kubwa kutoka kwa watu walioathirika na kukatwa kwa Lowasa hasa kutokana na fedha nyingi na muda kwa matumaini kuwa watakuwa "UPPER" baada ya Lowasa kushinda Urais. Miongoni mwao ni pamoja na Prof Juma Kapuya, Nazir Karamagi, Parseko Kone, Mgana Msindai, Kingunge Ngombale Mwiru, Mchungaji Gwajima, Andrew Chenge nk.
Hata hivyo, inadaiwa pia kuwa watu walio karibu na Lowasa akiwemo mfadhili wake mkuu Rostam Aziz ambaye amegoma kutoa fedha za kufadhili harakati za kwenda upinzani wanaendelea kumsihi kuwa asiende huko kwani atakuwa amejimaliza kabisa kisiasa. Pia inadaiwa kuwa mkewe Regina Lowasa amekuwa bitter sana na mpango wa mumewe kwenda upinzani na kwamba kwa siku kadhaa sasa amekuwa akiwafukuza wageni waliokuwa wanaenda nyumbani kwake hasa wale wa upinzani.
Hata hivyo, uamuzi wa Lowasa kwenda CHADEMA unatokana na msukumo wa maslahi binafsi baina ya Lowasa, Freeman Mbowe na wale waliomzunguka Lowasa na kwamba mpango huo ni hatari kubwa kwa ustawi wa CHADEMA. FREEMAN MBOWE anamtaka Lowasa kwa tamaa ya fedha ambapo matamanio yake yamekamilika baada ya kukabidhiwa shilingi bilioni 10 alizohitaji. Hata hivyo, upo uwezekano kuwa fedha hizo zikamtokea puani hasa pale atakaposhindwa kushawishi viongozi wa UKAWA kumteua Lowasa kupeperusha Bendera yao kwa mujibu wa makubaliano ya Lowasa na Mbowe.
Pia mtakumbuka kuwa Lowasa ameenguliwa CCM kutokana na kukiuka kanuni na taratibu za chama huku kashfa za ufisadi zikitumika kama kigezo kikuu cha kuenguliwa kwake. Lowasa huyu anayeenda CHADEMA ni Lowasa yule yule wa Kashfa za Richmond na kwamba CHADEMA wanapokea mtu ambaye taifa limemkataa.
Aidha, viongozi wa CHADEMA wamekuwa na kauli tofauti juu ya Lowasa huku Tundu Lissu na Wilbroad Slaa bila kumsahau Godbless Lema wakiongoza mashambulizi dhidi ya Lowasa. Mathalan, hotuba za viongozi hawa wakati wa Uchaguzi Mdogo wa Arumeru Mashariki ambapo Nassari alikuwa anapambana na Sioi Sumari, Mkwe wa Lowasa zilitawala kashfa za Lowasa na kashfa hizo ndizo zilizopelekea Nassari kushinda. Pia, Dr Slaa amemtaja Lowasa kwenye list of shame na hajajitokeza kwenye vyombo vya habari na kutangaza kuwa amemuondoa kwenye Orodha hiyo.
Vilevile, shinikizo la Lowasa kwenda CHADEMA linafanywa na watu ambao image yao kwenye public ni mbaya. Watu kama Prof Kapuya, Nazir Karamagi, Andrew Chenge na wengineo hakika wanawakilisha kikundi cha watu ambao hawana taswira nzuri kwenye jamii.
CHADEMA wana wakati mgumu sana katika kumnadi Lowasa. Siku zote wamekuwa wakijipambanua kuwa chama chao kinapambana na ufisadi. Inashangaza kuwa wanaojinasibu kuwa wanapambana na ufisadi ndo wanapokea rushwa na wanakaribisha mafisadi kwenye chama chao.
Natambua kuwa CHADEMA wanataka kumtumia tu Lowasa katika uchaguzi Mkuu ujao na baada ya hapo watamtema. Hata hivyo watambue kuwa uamuzi huo si tu utakuwa na athari kwa Lowasa bali hata wao CHADEMA watakuwa wamejimaliza.
Nimalizie kwa kusema kuwa Lowasa huyu ambaye ameonekana mchafu ndani ya CCM hawezi kuwa msafi ndani ya CHADEMA.

CHANZO FULL HABARI

Comments

Popular posts from this blog