MTITU, STEVE NYERERE BIFU KALI WAAPA KUTOZIKANA!
Steve Nyerere, ndiye alikuwa wa kwanza ‘kuachama’ mbele ya gazeti hili ndani ya Viwanja vya Leaders, Dar kulikokuwa na kikao cha maandalizi ya sherehe ya harusi ya msanii mwenzao, Hadji Adam ‘Baba Haji’.
“Hakuna mtu mnafiki kama Mtitu, sitaki kabisa hata kumsikia na kila nikimtazama najisikia vibaya mno, mkiwa pamoja anaonekana mwema lakini baada ya hapo anakuwa msaliti, kwanza hata nikifiwa sitaki kumuona msibani, nikifa mimi hakika asihudhurie mazishi yangu, naapa,” alisema Nyerere huku akimtazama mwandishi kwa jicho la ‘sitanii kaka’.
Naye kwa upande wake, Mtitu aliposikia hayo alionekana kumpuuza Nyerere huku akimtolea maneno ya kejeli na dharau tele.
Comments
Post a Comment