WEMA, AUNT KIMENUKA KISA ZARI


KIMENUKA! Mashosti wa kufa na kuzikana, Wema Isaac Sepetu na Aunt Ezekiel Grayson wanadaiwa kugombana baada ya Aunt ‘kuposti’ kwenye ukurasa wake wa Instagram tangazo lililohusiana na pati ya mwandani wa mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ iliyofanyika Mlimani City jijini Dar wikiendi iliyopita.
Mashosti wa kufa na kuzikana, Wema Isaac Sepetu na Aunt Ezekiel Grayson.
Kwa mujibu wa mtu wa karibu wa mastaa hao wa sinema za Kibongo, baada ya Aunt kuposti tangazo hilo akiwalaumu watu wa mtandao wa huduma za simu waliomtumia ndipo Wema akaona na kuja juu.
Ilielezwa kwamba baada ya Aunt kutupia picha ya tangazo hilo, Wema alichukizwa na kitendo hicho huku akimuona Aunt kuwa amemsaliti.
Aunt Ezekiel Grayson.
Ilisemekana kwamba katika utetezi wake, Aunt hakupendezwa na tangazo hilo alilotumiwa na mtandao huo wa simu.
“Wema alivyoona alichukia na kusema Aunt alikuwa akimsaliti na alitumia tangazo lile kijanja kwa ajili ya kuwatangazia watu kuhusu pati ya Zari wakati anajua kabisa kuwa Wema hazipandi na Zari kwa sababu anatoka na aliyekuwa mchumba’ke (Diamond),” kilisema chanzo hicho.
 
Wema Isaac Sepetu.
Katika sakata hilo, kuna watu ambao waliona Aunt hakuwa na kosa lakini wapo walioona hakuwa sahihi, jambo ambalo lilichochea ugomvi wao huku wakidaiwa kukesha wakitukanana.
Gazeti hili lilipozungumza na Aunt kuhusiana na sakata hilo, alikiri kutokea akisema kuwa hakuwa na maana mbaya kuposti tangazo hilo lakini kila mtu ana mtazamo wake.
“Mimi sikumaanisha chochote kibaya kuhusu hilo tangazo na wala sikujua kama kuna mtu anaweza akalichukulia tofauti kabisa na hapo na mimi ndiyo nashindwa cha kuzungumza,” alisema Aunt.
Alipopigiwa Wema simu yake iliita bila kupokelewa hadi gazeti hili linakwenda mitamboni.

Comments

Popular posts from this blog