RECHO WA THT ALIA NA BABU TALE BAADA YA KUZUIWA KUMTUNZA DIAMOND.


MREMBO mwenye sauti nyororo kutoka Jumba la Kukuza Vipaji Tanzania (THT), Winifrida Josephat ‘Recho Mapenzi,’ hivi karibuni alijikuta akiangua kilio baada ya kuzuiwa kupanda kwenye jukwaa kwa ajili ya kumtunza Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz.’

Mrembo mwenye sauti nyororo kutoka Jumba la Kukuza Vipaji Tanzania (THT), Winifrida Josephat ‘Recho Mapenzi.
Tukio hilo lilitokea ndani ya Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar kwenye shoo ya Zari All White Party ambapo bidada huyo akiwa katika hali ya mzuka alijikuta akiishia kuangua kilio baada ya kuzuiwa na Meneja wa Diamond, Babu Tale kupanda jukwaani.
Akilalama kwa machungu baada ya kukwamishwa kumfikia Diamond, Recho alisema kuwa hakufurahishwa hata kidogo na uamuzi wa Babu Tale kwani anamjua wazi ni msanii hivyo hakuwa na haja ya kuwaamuru mabaunsa kumzuia kwenda kumtuza staa mwenzake.
“Kweli Tale hajanitendea haki hata kidogo, kwani nilimuahidi mapema Diamond ningemtuza na pale nilitaka kutimiza ahadi yangu lakini nikazuiwa,” alisema Recho kwa masikitiko.

Comments

Popular posts from this blog