MAHABA: MWANAUME NDIYE MWENYE NAFASI YA KULINDA PENDO!!!

HABARI wadau wa safu yetu, tupo tena pamoja katika kujuzana jinsi gani maisha ya kimapenzi yalivyo. Leo nitakuwa tofauti kidogo na mara zote ambazo nimekuwa nikiwasiliana nanyi, kwani mara nyingi nimekuwa nikizungumzia kuhusu nafasi ya mwanamke, kuwa ili iwe hivi, basi afanye hivi na kadhalika.
Maandiko mengi yamekuwa ni kama ya kuonyesha kuwa mwanamke ndiye mwenye dhamana kubwa ya kuamua juu ya penzi au ndoa aliyomo. Ingawa ni kweli kuwa kuna umuhimu mkubwa wa mama kuwa mshirika muhimu katika ndoa, lakini amini usiamini, mwanaume ndiye hasa mwenye kushika turufu ya penzi linalohusika. 
Na ninasema hivi hasa kutokana na ukweli ambao nafsi zote mbili zinakubaliana kuwa mwanaume ndiye kichwa cha nyumba. Usemi huu unaweza kuonekana ni mwepesi kama utaangaliwa kwa upande mmoja tu, ambao kimsingi unabeba maana ya uwajibikaji juu ya majukumu ya kuilea na kuilinda familia.

TUPE MAONI YAKO NDUGU MDAU WETU KUHUSU HILI NA USISITE KUUNGANA NASI KUPITIA UKURASA WETU WA FACEBOOK KWA HABARI NA MATUKIO ZAIDI

Comments

Popular posts from this blog