PICHA ZA MBUNGE JOSHUA NASSARI ALIVYOFUNGA NDOA YA KIHISTORIA HII JIJINI ARUSHA



Mbunge Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Samwel Nassari amefunga ndoa na Anande Nko kwenye Kanisa la Pentekoste lililopo Kilinga, Arumeru jijini Arusha ikifuatiwa na sherehe kubwa iliyofanyika katika Viwanja vya Usa-River Academy jirani na Hoteli ya Ngurdoto.Sherehe hiyo ilianza mishale ya saa 7:00 mchana siku ya leo ambapo watu wote walialikwa wakiwemo ndugu, marafiki, jamaa na wananchi wote wa Arumeru Mashariki ambao wamepiga ‘mpunga’ wa kutosha na vinywaji hadi kila mtu akaondoka akisema ‘Nassari ameacha historia’.
 

Comments

Popular posts from this blog