IBADA YA KIISLAMU KUFANYIKA VATICAN ( MAKAO MAKUU YA KANISA KATOLIKI ) KWA MARA YA KWANZA KATIKA HISTORIA

Kwa mara ya kwanza katika historia, sala na mafundisho kutoka kwenye Quran yatasikika Vatican Jumapili, ambako ni makao makuu ya kanisa katoliki duniani.
Uamuzi huo umefanywa na Papa Francis ikiwa ni hatua ya kutengeneza mazingira ya amani kati ya waisrael na wapalestina.
Kiongozi huyo wa kanisa katoliki duniani aliwaalika rais, Shimon Peres na rais wa Palestina Mahmoud Abbas kwenda Vatican pale alipozitembelea Palestina na Israel hivi karibuni.

Kwa mujibu wa Times of Israel, marais wote wawili wamekubali mualiko huo. Msemaji wa ikulu ya Israel ameeleza kuwa watasindikizwa na viongozi wa dini za kikristo na kiislam.

Kwa mujibu wa Associated Press, Papa Francis amesema kuwa kutakuwa na maombi ya jioni jumapili hiyo pale watakapokutana na kwamba yatalenga kusaidia amani kati ya matakwa ya wapalestina na waisrael katika nyanja zote.

Comments

Popular posts from this blog