UKAWA WAPATA PIGO MKOANI IRINGA.....WAPOKELEWA KWA MABANGO YA KUWAPINGA, MKUTANO WAGUBIKWA NA VURUGU KUBWA


UMOJA  wa  Katiba  ya  Wananchi  (  UKAWA )   umepokelwa  kwa  mabango  yanayowapinga  wilaya  ya  Mufindi  mkoani  Iringa  yaliyokuwa  yamebebwa  na  vijana.... Mabango  hayo  yalikuwa  yanasomeka  kuwa, "Tuna  mashaka  na  ndoa  ya  UKAWA  watauza  nchi", huku  yakisisitiza  umuhimu  wa  vijana  wa  Wilaya  ya  Mufindi  kutaka  Serikali  mbili.....

Pia  mabango  hayo  yalikuwa  yanawataka  wajumbe  wa  UKAWA  warudishe  posho  kwanza  bungeni  mjini  Dodoma....
Katika  mkutano wao   uliofanyika  juzi mjini  Mafinga  Viwanja  vya  mashujaa, mkutano  huo  uliendeshwa  na  mwenyekiti  wa  chama  cha  Wananchi ( CUF )  ambaye  pia  ni  mwenyekiti  mwenza  wa  UKAWA.....
Wengine  waliohutubia  ni  pamoja  na  mwakilishi  wa  chama  cha  NNCR-Mageuzi,Danda  Juju  na  kiongozi wa  taasisi  ya  kiislam  ya  Shura  ya  Imamu,Rajabu  Katimba.


Baadhi  ya  mabango  yaliyokuwa  yamebebwa  na  vijana  hao  wilayani  Mufindi  yalikuwa  na  ujumbe  uliosomeka: "Vijana  Mafinga  tuna  mashaka  na  ndoa  ya  UKAWA,watauza  nchi" na  bango  la  waendesha  bodaboda  lilisomeka: "Rudisheni  posho  kwanza  mjengoni  Dodoma"
Mengine  na  ujumbe  wake  kwenye  mabano  ni lililowatambulisha  wafanyabiashara  wa  sokoni  lililosomeka, "Mafinga  Sokoni,Serikali  tatu  siyo  suluhisho  la  matatizo  ya  wananchi", na  la wapiga  debe  mafinga  stendi  lilisomeka, "Karume  Oyee, Nyerere Oyee, Muungano  Saafi!".

Bango  la  waliojitambulisha  kuwa  ni  machinga  lilisomeka,"Tunataka  Serikali  inayojali  wajasiriamali, siyo  kujali  matumbo  yao"...Na  lile  la  wakulima  lilisomeka, "Kilimo  Kwanza, Utaifa  kwanza".

Wakati  mabango  hayo  yakizungushwa  katika  mkutano huo  muda  ambao  Profesa  Lipumba  alikuwa  akihutubia, usikivu  ulipotea  kwa  takribani  dakika  15  hadi  20  baada  ya  sehemu  ya  kundi  la  vijana  lililokuwa  likimsikiliza  kuelekea  upande  walikokuwa  vijana  wenye  mabango  hayo....

Polisi  waliokuwepo  walilazimika  kuingilia  kati  kadhia  hiyo  na  mzozo  huo  baina  yao  na  vijana  waliokuwa  na  mabango  ulisikika....
Mmoja  wa  polisi  aliyekuwa  akiwatuliza  vjana  hao  alisema,"Jamani  huu  ni  mkutano  halali  wa  kisiasa, acheni  wenzenu  wafanye  mkutano  wao, yatoeni  mabango  yenu"

Mmoja  wa  vijana  aliyekuwa  amebeba  bango  mojawapo  jina  halikupatikana  mara moja  alisikika  akisema, "UKAWA  siyo  chama  cha  siasa, wao  wanamtazamo  wao  na  sisi  tuna mtazamo  wetu, kwa  hiyo  siyo  jambo  la  ajabu  wakajua  kwamba Mafinga  wengi  hatuwaungi  mkono  na  siyo  dhambi  kuonyesha  hisia  zetu  katika  mkutano  wao"

Akielezea  vurugu hizo, profesa  Lipumba  alisema zinafanywa  na  vijana  waliotumwa  na  CCM  kwa  sababu  ya  msimamo  wao wa kutaka  serikali mbili, tuhuma  zilizokanushwa  na  katibu  wa  CCM wilaya  ya  Mufindi,Miraji  Mtaturu  aliyehojiwa  baada  ya  mkutano  huo...

"Siamini  kama  mkutano  huu  ungekuwa  unahutubiwa  na   mwenyekiti  wa  CCM wa taifa  Jakaya  Kikwete  wangekuja  na  mabango  yao  na  kufanya  vurugu  hizi," alisema  Lipumba  na  sauti  toka  kwa  baadhi  ya  vijana  hao  zikasikika  zikisema, "Kama  angekuja  na  msimamo  wa  serikali  tatu  ni lazima  angekutana  na  mabango  haya, sisi  tunataka  serikali  mbili"


Hata  baada  ya  vurugu  hizo  kutulia  na  Profesa  Lipumba kuruhusu  maswali  baada  ya  kufafanua  sababu  mbalimbali  zilizowafanya  wasusie  bunge  la  katiba  na  kuanzisha  UKAWA, mkutano  huo  ulitaka  kuvurugika  tena....

Swali  liliotaka  kuuvuruga  mkutano  huo  lilitoka  kwa  kijana  aliyejitambulisha  kwa  jina  la  Rahid  Rashid  ambaye  alitaka  kujua  kwa  nini  CCM  hawapo  katika  umoja  huo.

Pamoja  na  vijana  wengine  kupiga  kelele  wakiashiria  kuwa  hilo  siyo  swali,Profesa  Lipumba  alijibu  na  kusema  hilo  ni  swali  zuri.

Alisema  milango  ya  UKAWA  ipo  wazi  kwa  mtu  yeyote  ndani  na  nje  ya  bunge  la  katiba  wakiwemo  wabunge  na viongozi  wa  CCM

"Tutafurahi  kuwapata  wana  CCM,tunawakaribisha  UKAWA  ili  kwa  pamoja  tushirikiane  kupata  katiba  inayotokana na  wananchi,"alisema

Mwingine  aliyeuliza  swali  alikuwa  Winfrida  Ngoti  aliyesema  harakati  za  kudai  serikali  tatu  hazitakuwa  na  maana  yoyote  kama  matatizo  ya  wananchi  hayatashughulikiwa.

"Watanzania  wana  matatizo  lukuki,vituo  vya  huduma  za  afya  havina  wataalamu,dada,wakulima  hawapati  pembejeo  kwa  wakati  na  bei  zake  ni  kubwa, wafanyabiashara  wadogo  wanabanwa  na  kukamuliwa  kodi, walimu  haapati  mishahara  kwa  wakati, askari  wana mishahara  midogo ," alifafanua


Katika  majibu  yake, profesa  Lipumba  alisema  hayo  yote  yatafanyiwa  kazi  kukiwa  na  katiba  bora  itakayosisitiza  uwajibikaji  na  uadilifu

Comments

Popular posts from this blog