MUONGOZAJI MAHIRI WA FILAMU NA VIPINDI TANZANIA GEORGE TYSON AFARIKI DUNIA KATIKA AJALI YA GARI ILIYOTOKEA MKOANI MOROGORO

George Tyson enzi za Uhai wake
Taarifa zilizotufikia katika meza yetu ya habari Usiku huu ni kuwa Muongozaji mahiri katika Tasnia ya Filamu Nchini na Mzazi Mwenza wa Msanii Nguli wa Filamu nchini Vyonne Cherry Au Monalisa, Bwana George Tyson amefariki Dunia mara baada ya kupata ajali ya gari Mkoani Morogoro Katika Eneo la Gairo wakati wakitokea Mkoani Dodoma ambapo walienda kwaajili ya Kuadhimisha Miaka Miwili ya Kipindi Cha Mboni Show.
Bw Tyson Mauti yamemfika mara baada ya Gari walilokuwa Wakitumia kusafiria Kutoka Mkoani Dodoma Kupasuka Matairi na kupelekea Kupoteza maisha na kupelekea hali ya watu wengine wanne waliokuwemo katika Gari hilo kuwa mbaya baada ya Kuumia vibaya na kukimbizwa katika hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwaajili ya Matibabu.

Ajali hiyo imetokea majira ya Saa Moja Usiku katika Eneo la Gairo

Tutaendelea Kupeana taarifa zaidi kadri tunavyozipata

Tunapenda kutoa Pole kwa Mmoja wa Majaji wa Shindano la Tanzania Movie Talents ambae ni Mzazi Mwenza wa Marehemu George Tyson, Bi Vyonne Chery Kwa kuondokewa na Mzazi mwenzie ambae walibahatika Kupata Mtoto Mmoja aitwaye Sonia.

Comments

Popular posts from this blog