ANGALIA PICHA MTOTO AFARIKI BAADA YA KUANGUKIWA NA JIWE KUBWA

Huyu ni baba wa mtoto, bwana Jackson Ismail akimwangalia mwanae kwa uchungu..
Wangali wakipata chakula hicho, baba aliwahi kumaliza na hivyo kuendelea na kazi hiyo ya kuponda mawe huku mkewe na watoto wakimalizia kupata chakula....
Wakati bwana Ismail akiendelea kuyaporomosha mawe hayo,ghafla alisikia mtikisiko mkubwa na hivyo kumtaka mkewe na watoto watoke haraka.....
Mama akiwa na mtoto mchanga waliwahi kunyanyuka na kutoka,lakini kabla binti Malaika mwenye umri wa miaka mitano hajatoka, jiwe kubwa lilimuwahi na kumkandamiza na kumfanya afariki dunia papo hapo....

Mwili wa Marehemu Malaika Jackson...


Baadhi ya wananchi wakiwa eneo la tukio
Comments
Post a Comment