HEIFER INTERNATIONAL TANZANIA YAZINDUA MRADI MKUBWA WA KUENDELEZA SEKTA YA MAZIWA KWA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI

Naibu waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi ambae pia alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo, Mh Kaika Telele akiongea na wageni waalikwa na wadau wa sekta ya Maziwa Afrika Mashariki uliofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwl Nyerere Mwishoni mwa Wiki.
 Mkurugenzi Mkuu wa Heifer International Tanzania, Dk Henry Njakoi akiongea na wageni waalikwa na wadau wa sekta ya maziwa nchini na wa kimataifa waliofika katika uzinduzi wa Mradi wa Uendelezaji Sekta ya Maziwa Afrika Mashariki uliodhaminiwa na Mfuko wa Bill na Melinda, Mradi huo mkumbwa ulizinduliwa ijumaa iliyopita katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwl Nyerere uliopo Jijini Dar Es Salaam
 Mkurugenzi Mkuu wa East Africa Dairy Development (EADD), Mh Rakesh Kapoor akichangia mada kwenye uzinduzi wa Mradi wa Kuendeleza sekta ya Maziwa kwa Nchi za Afrika Mashariki mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwl Nyerere, jijini Dar Es Salaam. Mradi huo mkubwa kutoka Heifer International Tanzania umedhaminiwa na Mfuko wa Bill na Melinda Foundation
Mgeni Rasmi katika uzinduzi huo ambae pia ni Naibu waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Mh Kaika Telele akifungua Pazia kuashiria Mradi huo wa Kuendeleza sekta ya maziwa umezinduliwa rasmi katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwl Nyerere uliopo jijini Dar Es Salaam.
 Mjasiliamali wa Maziwa kutoka Mkoani Iringa, Bi Diana akitoa Ushuhuda wake kwa wageni waalikwa kuhusu mafanikio aliyoyapata akiwa kama mdau wa sekta ya maziwa.
Mgeni Rasmi katika Uzinduzi huo ambae pia ni Naibu waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Mh Kaika Telele akimpongeza Mjasiliamali wa Waziwa kutoka Mkoani Iringa, Bi Diana wakati wa uzinduzi wa Mradi wa kuendeleza Sekta ya Maziwa Afrika Mashariki.

Comments

Popular posts from this blog