UUME WAKE NI MDOGO SANA HAJAWAHI KUNIFIKISHA KILELENI.

Mwanamke mmoja nchini Taiwan amedai talaka mahakamani toka kwa mumewe wa miaka minne kutokana na udogo wa maumbile yake ya kiume na pia kwa kushindwa kutimiza ahadi ya kutoa unyumba mara tatu kwa wiki.Mwanamke huyo aliyetajwa kwa jina la Zhang mwenye umri wa miaka 52, amevunja ndoa yake ya miaka minne na mumewe Zhou mwenye umri wa miaka 55 sababu kubwa ikiwa ni udogo wa uume wake.

"Uume wake ni mdogo sana sawa na wa mtoto, una urefu wa sentimita tano tu, hatujawahi kufurahia mapenzi kwa muda wote wa ndoa yetu", alisema Zhnag.

Zhang aliongeza kuwa alikutana na mumewe mwaka 2008 kupitia kwa rafiki yake na walifunga ndoa miezi mitano baadae.

Zhnag aliendelea kusema kuwa kabla ya ndoa hawakuwahi kufanya mapenzi kwakuwa mumewe huyo alikuwa akidai kuwa yeye ni mtu wa dini sana hawezi kufanya mapenzi nje ya ndoa.

"Niligundua tatizo alilonalo siku ya harusi", alisema Zhang na kuongeza "Pia hajiwezi kutimiza majukumu yake ya kutoa unyumba kwa mkewe".

"Tuligombana usiku mzima na nilimwambia afanye hima kutafuta tiba" alisema Zhang ambaye sasa amefanikiwa kuivunja ndoa hiyo kupitia mahakama.

Hii sio mara ya kwanza kesi za kuvunja ndoa kufika mahakamani sababu ikiwa ni ufanisi kwenye tendo la ndoa. Mwaka 2008, Mwanaume mmoja wa nchini Urusi alikimbiwa na mkewe baada ya kwenda kufanya operesheni ya kuongeza ukubwa wa uume wake lakini wakati wa malavidavi kipande kilichoongezwa kwenye uume kilinyofoka.

Comments

Popular posts from this blog