MTOTO WA KIGOGO UKO MORO... APIGA PICHA ZA UTUPU NA KUZIWEKA KWENYE MTANDAO


Wakati sakata la mastaa kupiga picha za chafu likiwa bado halijaondoka vichwani mwa watu, gazeti la Ijumaa limenasa picha nyingine zinazomwonesha binti aliyetajwa kwa jina moja la Tuma akiwa mtupu ambaye inasemekana ni mtoto wa kigogo mmoja mkoani Morogoro, shuka mstari kwa mstari.
Awali gazeti lenye heshima tele mbele ya jamii, Ijumaa lilipokea waraka pepe kutoka kwa msomaji mmoja mkoani Morogoro ambaye alisema, anazo picha chafu za binti huyo zinazosambazwa kwa kasi ya moto wa petroli kwenye mtandao wa intaneti.
Waraka pepe uliotumwa kwenye anuani pepe ya Ijumaa ilisomeka: “Hello Ijumaa, ninazo picha za Tuma. Yupo mtupu, amelala kitandani, kama mnahitaji hiyo habari, nipeni pesa niwape mchongo mzima.”

Kwa kutambua umuhimu wa habari hiyo, haraka, gazeti hili lilijibu waraka pepe wa ‘sosi’ huyo na baada ya makubaliano, alituma picha za mapozi tofauti za mrembo huyo (kama zinavyoonekana ukurasa wa mbele) na maelezo kwa ufupi.
Chanzo hicho, kilieleza kwamba, picha hizo zinadaiwa kupigwa katika hoteli moja yenye jina kubwa jijini Tanga, ingawa haikujulikana ni nani aliyempiga na alikuwa na nia gani.


Alidai kwamba, kwa sasa picha hizo siyo stori tena Morogoro, kwasababu zimezagaa kila kona ya ‘Mji Kasoro Bahari’. 
“Huku hakufai, mchezo aliofanyiwa ni mchafu na Tuma anahaha kila kona, amefedheheka sana, anaogopa kuchafua familia yake,” kiliendelea kupasha chanzo hicho.


Katika picha hizo, zipo zinazomwonesha binti huyo mrembo akiwa amepozi mwenyewe kitandani na kanga moja, wakati nyingine zikimwonyesha amelala mtupu, uso wake ukipambwa na tabasamu mwanana, tukio linaloashiria kwamba alikuwa akitoa ushirikiano wa kutosha wakati zoezi la kupigwa picha hizo lilipofanyika. 

Aidha, ipo picha inayomwonesha binti huyo akiwa analia, huku sababu za kilio chake akiwa anazijua mwenyewe.
Hakuna maelezo ya kutosha juu ya picha hizo ila Timu ya Ijumaa inaingia mzigoni ili kubaini upande wa pili kisha tutawaletea mwendelezo wake.

KUTOKA KWA MHARIRI
Kwa muda mrefu sasa, magazeti pendwa yamekuwa yakiripoti habari zinazohusu wasichana kupiga picha za utupu kwa lengo la kukemea tabia hiyo, lakini bado sikio la kufa halisikii dawa kwani ndiyo kwanza wamecharuka. 

Kwetu sisi, kupiga picha chafu si tabia njema na inaharibu maadili ya jamii nzima ambayo kimsingi si utamaduni wetu.
Tunarudia tena na tena kutoa angalizo letu kwa mabinti kuwa makini na wapenzi wao, wasikubali kupigwa picha chafu wanapokuwa nao faragha, kwani inaweza kuharibu taswira ya maisha yao siku zikivuja.

Comments

Popular posts from this blog