MTOTO HUYU AMEOKOTWA NDANI YA HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI JANA SAA SITA MCHANA


Mtoto huyu anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 2. hadi 2.5 kasoro ameokotwa eneo kati ya Jengo la Wazazi ndani ya  Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Tafadhali yeyote anayefahamu wazazi wake, au ndugu zake atufahamishe mara moja. Mtoto huyu kwa sasa tunaye  na ili uweze kumchukua uje na vielelezo vifuatavyo;

1.    RB ya Polisi
2.    Cheti cha Kuzaliwa cha mtoto
3.    Picha ya mtoto mwenyewe
4.    Kadi ya Kliniki ya Mtoto
5.    Barua kutoka Serikali ya Mtaa ikikutambulisha
6.    Kitambulisho cha Mpiga Kura
7.    Kitambulisho cha Taifa kama tayari umepata

Wasiliana nami kupitia 0755 648636. Mtoto hawezi kuongea vizuri hivyo tumeshindwa kufahamu vizuri jina lake anavyolitamka.

Comments

Popular posts from this blog