MWANAMKE AMKATA KORODANI MPENZI WAKE MKOANI SIMIYU

 

JESHI la Polisi mkoani Simiyu linamshikilia mwanamke na mkazi wa Kijiji cha Usiulize wilayani Meatu kwa tuhuma za kumuua mpenzi wake kwa kumvuta korodani, kutokana na wivu wa kimapenzi.
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, Charles Mkumbo alisema tukio hilo lilitokea juzi saa tisa usiku katika Kitongoji cha Mlimani Kijiji cha Usiulize Kata ya Mwamalole. 

Alisema katika tukio hilo, wapenzi wawili Jumanne Gunda (39), mkazi wa Kijiji cha Kinyambuli wilayani Mkalamo, akiwa amelala na mchumba wake, Mariamu Khamis (49) mkazi wa Kijiji cha Ibaga Wilaya ya Mkalamo mkoani Singida, kulitokea kutoelewana kati yao na kusababisha wagombane.


Katika ugomvi huo, ambao chanzo chake ni wivu wa kimapenzi, Mariamu anatuhumiwa kuzivuta korodani za mpenzi wake na kusababisha mishipa muhimu kukatika na kusababisha kifo cha Jumanne papo hapo.

Comments

Popular posts from this blog