DIAMOND ATOA MSAADA KWA WATOTO WAISHIO KWENYE MAZINGIRA MAGUMU, BUGURUNI



 Maisha yetu wengi ni ya mikiki mikiki ya hapa na pale
ya kutafuta..nimekuwa bize mwaka mzima ..lakini

siku  yangu ya leo baada ya Swalt Ijumaa niliitumia

 kujumuika na watoto waishio
kwenye mazingira magumu kilichopo

 Buguruni ambapo nilipata wasaa wa ..kula nao pamoja ,kucheza..kubadilishana mawazo.

.lakini pia kutumia nafasi hiyo kuwaonyesha kwa

mara ya ,kwanza kabisa,video yangu ya number 1 remix
niliyoifanya na Davido .

.nimefanya hii kwa

 sababu ,hawa ndio mashabiki wetu wakubwa.

mara nyingi show zetu tunafanya usiku..mda ambao watoto

 hawaruhusiwi na ukizingatia watotot

 hawa ,wanaishi katika mazingira ambayo hawawezi 

kuhudhuria maonyesho yetu
hivyo leo nimeamua kwa mara ya kwanza niwaonyeshe

 wao kwanza,kabla sijaisambaza kwa wananchi wote...lingine

 la mhimu ni kwamba..mwezi huu tarehe

 25..nimeandaa onyesho maalum pale Readers

 club kwa ajili ya watoto wote ambao 

kawaida hawapati nafasi ya

 kuhudhuria,show zetu za usiku na nimetoa 

complimentary 50 kwa hawa watoto niliokuwa nao leo ...

Cha kukumbushia tu ni kuwa..zoezi hili ni

 endelevu..nitaendelea kutembelea

 maeneo mbali mbali kutoa sadaka kwa

 watoto wenye mazingira magumu

lakini pia nitoe wito..kwa yeyote 

atakaye wiwa kufanya nami zoezi hili..anakalibishwa kuungana nami..

Wasiliana nasi kupitia0715333346. 




 Mama na Anko wakiwa mtaani kununua zawadi








 Baada ya kuwasili tukishusha zawadi mbali mbali tulizoandaa















 Wadogo zangu wakiniskiliza kwa makini wakati nikizungumza nao machache


 Mama mlezi wa kituo


 Babu Tale alikuwepo pia






 Mkubwa fella pia






 Mama yangu pia alipata nafasi ya kuzungumza






































 Tukila pamoja,tukitaniana,kubadilishana mawazo..pia kushauriana
























 Nikitoa mausia kwa wadogo zangu jinsi ya

 kupambana katika maisha pasipo kukata tamaa







Comments

Popular posts from this blog