MKAPA ATIMIZA MIAKA 75 YA KUZALIWA WAKE
Kwa upande wake, Kardinali Pengo aliwataka Watanzania kuwa na tabia ya kumshukuru Mungu kwa kila jambo.
“Alichofanya Rais Mstaafu Mkapa ni cha kuigwa. Tunatakiwa kutambua kuwa hatuishi kwa nguvu zetu bali kwa uwezo wa Mungu hivyo ni lazima tumshukuru kama alivyofanya mwenzetu,” alisema Kardinali Pengo.
Baadhi ya viongozi waliohudhuria ibada hiyo ni pamoja na Mawaziri Wakuu Wastaafu, Edward Lowassa na Cleopa Msuya, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu wa Bunge), William Lukuvi na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia.
Wengine ni waziri wa zamani, Profesa Philemon Sarungi, Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Alex Malasusa pamoja wakuu wa zamani wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Majenerali, Robert Mboma na George Waitara.
Comments
Post a Comment