"Nipo tayari kugombea URAIS endapo wananchi WATANICHAGUA."..Mwigulu Nchemba

 

Naibu katibu mkuu wa CCM bara, Mh. Mwigulu Nchemba ambaye pia ni mbunge wa Iramba  amefunguka  kuwa  vurugu zilizotekea bungeni wiki  iliyopita  zilisababishwa na kambi ya upinzani kukosa akili na kutumia nguvu kubwa ....

Akiongea  na  mpekuzi wetu , Mwigulu  ameitupia  lawama  kambi  ya  upinzani  na  kudai  kuwa  kambi hiyo  imekuwa ikitumia nguvu nyingi  badala ya akili na  maarifa  huku  ikisahau  kuwa Spika  pekee ndo  mwamuzi wa mwisho kwa jambo lolote ndani  ya bunge....

Mwigulu  alienda  mbali  na  kudai  kuwa, pamoja  na  vurugu hizo  ambazo  zimekuwa  zikifanywa   na  wapinzani  kwa  lengo  la  kujiimarisha  kisiasa, chama  chake  bado  kina imani  kubwa  ya  kushinda  kwa  kishindo  katika  uchaguzi  mkuu  wa  2015  kwa  kuwa  wapinzani  hawana SERA  wala  UBAVU  wa  kushindana  na  CCM  zaidi  ya  makelele na  vurugu.

Baada  ya  Mwigulu  kugusia  michakato  ya  uchaguzi  mkuu  ujao, mpekuzi  wetu  alitaka  kukata  kiu  yake  juu  ya  tetesi  zilizopo  kuwa  CCM wanamwandaa  kugombea  URAIS ...

Akijibu  swali  hilo, Mwigulu  ameweka  wazi  kuwa  yeye  yupo  tayari  kuwatumikia  wananchi  katika  nafasi  yoyote  ile   na  kwamba  wao  ndo  wenye  maamuzi  ya  mwisho.

"Wananchi  ndo  waamuzi  wa  mwisho.Endapo  wataona  ninafaa  kwa Rais, basi  ntafanya  hivyo  kwa  sababu  nipo  tayari  kuwatumikia  katika  nafasi  yoyote.

"Najua  vijana  wengi  wananichukia  kutokana  na  chuki  zinazopandikizwa  katika  mitandao  ya  wapinzani. Ukweli  ni  kwamba  chuki  hizo  zinatokana  na  ukweli  kwamba  mimi  ni  mtu  ninayejua  madhaifu  mengi  ya  wapinzani.

"Natoa  wito  kwa  vijana  wenzangu  kuwapuuza  watu  hao  kwa  kuwa  hawana  nia  njema  na  taifa  hili"..Mwigulu

Comments

Popular posts from this blog