MBINU ZA KUKABILIANA NA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME, KUPIZI HARAKA, NA KUSHINDWA KURUDIA RAUNDI YA PILI

Tunapozungumzia upungufu wa nguvu za
kiume tunakuwa katika uwanja mpana
zaidi wa tafakari za kibaiolojia na
kisaikolojia walizonazo wanaume.
Lakini kwa kufupisha mlolongo wa mambo
sehemu kuu tatu zinaweza kabisa kukidhi
mchanganuo mzima wa jinsi tatizo hili
linavyowasumbua wanaume wengi
duniani.


Sehemu kubwa ya malalamiko ya
wanaume katika sakata hili yanagusa zaidi
maeneo matatu ambayo ni KUKOSA
MSISIMKO, KUSHINDWA KURUDIA TENDO NA
KUKOSA KABISA NGUVU, huku kufika kileleni
mapema kukihusishwa pia kama pacha wa
janga hili ambalo linawasumbua zaidi
wanaume, ingawa na wanawake
wanakabiliwa na sehemu ndogo ya tatizo
hili.



Hata hivyo uchunguzi wa hivi karibuni

uliowahusisha wanaume wanaofika kliniki

au kupata tiba za tatizo la upungufu wa
nguvu za kiume umeonesha kuwa, sio
wanaume wengi wenye sababu za
kibaiolojia zinazowafanya wakose nguvu
za kiume, isipokuwa wengi wao huwa na
matatizo ya kisaikolojia zaidi ambayo
wahusika wanaweza kujiponya nayo bila
hata kutumia vidonge wala dawa za miti
shamba.



Ingawa Matabibu wanataja magonjwa ya
moyo, kisukari, shinikizo la damu,
magonjwa ya zinaa, unene wa kupita kiasi,
umri mkubwa kuwa ndiyo chanzo cha
wanaume kupungukiwa na nguvu za
kiume, lakini imebainika kuwa idadi
kubwa ya wanaume wanaofika hospitalini
kutafuta nguvu za kiume hawana
magonjwa hayo
Huu ni ushahidi kuwa wanaokabiliwa na
janga hili wamebeba tatizo la upungufu
wa nguvu za kiume kimawazo zaidi kuliko
hali halisi.

Ukweli wa mambo ulioibuliwa na
wanasaikolojia umebaini kuwa, wale wote
wanaolalamikia/lalamikiwa kuwa hawana
nguvu iwe ya kufika kileleni mapema,
kutokuwa na msisimko na kushindwa
kurudia tendo wamekosa maarifa tu ya
kufahamu na hawaijui miili yao na
kwamba wanaishi kwa kusikia zaidi ya
kujitambua.

Katika hali ya kawaida kila mwanadamu
ameumbwa kwa njinsi yake na inapotokea
kushabihiana basi ni bahati, lakini mara
nyingi usawa hupatikana kwa mmoja
kujifunza au kusaidiwa kufikia kiwango
cha mtu anayemuhitaji kuwa nae katika
maisha hasa ya kimapenzi. Jambo hili
wataalamu wanasema kuwa miili iko tayari
kutii mafunzo na kubadilisha tabia zake
kulingana na utashi wa mhusika.

Tatizo kubwa lililopo kwa wapenzi wengi
wanaolalamikia upungufu wa nguvu ni
kwamba maisha yao wanayachezea
kwenye viwanja vya wenzao wanaokutana
nao katika vijiwe na sehemu za kazi.
Usikivu wa mazungumzo toka kwa
wanaume wengine wenye uwezo wa
kwenda mara nne hadi saba katika tendo
au wanatumia dakika arobaini kufika
kileleni umewafanya wanaume wengi
kujihisi tu kuwa wao wanakasoro eti kwa
kuwa huishia mara mbili au moja katika
kufanya tendo.

Dhana ya kujiona ni mwenye kasoro
inapojengeka akilini mwa mwanaume,
huchipua hofu na hatimaye kumfanya
ashindwe kabisa kusisimka anapofikiria au
kukutana na mwanamke. Matokeo ya
hangaiko la akili hushusha uwezo wa
mwili na kumuongoza mtu kwenye
kuwaza ugonjwa kisha kukimbilia hospitali
au kwa waganga kutafuta tiba ya
ugongwa ambao kimsingi hanao.

Lakini ukweli uko wazi kwamba kukimbilia
kutafuta uwezo wa kufanya mapenzi mara
sita au saba hakumfanyi mwanaume awe
mlinganifu mwenye kusifiwa na
wanawake wengi, kwani si wanawake
wote wana uwezo wa kufanya mapezi
kwa raundi hizo na si wote wanapenda
kutumia takika 30 kucheza mpira wa
kikubwa, wengine hukinai mapema na
huona kero kuwa na wanaume
ving’ang’anizi wenye sifa za kuganda
wanapopewa.

Kwa kufahamu haya utagundua kuwa
kukimbilia kutafuta tiba ya kumudu
kwenda mara saba ni jitihada mfu kabisa
zisizohitajika katika maisha ya mwanaume
hasa ukizingatia kwamba wenye uwezo
wa kufanya mapenzi mara nyingi
hawakuzaliwa hivyo, bali walijizoeza
kupitia mazingira ya malezi na makuzi yao.
Maana hawezi kuwa mzoefu wa raundi
mvulana aliyelelewa katika mafundisho ya
kukatazwa ngono na kulindwa hadi
akakakua.

Kadhalika hawi hodari wa kimapenzi
msichana aliyefundishwa kujitunza, yote
yatakayofuata kwa mvulana au msichana
humea baada ya kupandwa na tabia
chipukizi za ukubwani. Kwa msingi huo
mwanaume anajukumu la kuutengeneza
mwili wake uwe katika staili aitakayo.
Ndiyo maana kuna wengine hawamudu
kulala bila kufanya ngono, hii ikiwa na
maana kuwa wamejizoeza tu, si kwamba
wameumbwa na nguvu hizo.
Labda ili kufikia kilele cha somo hili ni
vema tukalejea matatizo matatu niliyosema
hapo juu ili tujue ni jinsi gani tunaweza
kuepukana nayo bila hata kumeza vidonge
na tukawa wanaume wa mbegu kama
wengi wenu mjuavyo.

Kwa kuanza tuzungumzie Kukosa
msisimko. Hapa tunatakiwa kuajitambua
sisi wenyewe kwanza, tukijua historia na
mazingira yetu ya kimapenzi.
Kwa wanaume ambao wamebanwa sana
kikazi na hufanya mapenzi mara moja
moja, hukabiliwa na tatizo la kukosa
msisimko kwa sababu miili yao imezoea.
Sasa ili kuifanya ichangamke lazima
waanze kuirejesha kwa kufanya mapenzi
mara kwa mara na kwa raundi chache.
Kisha wanatakiwa kufanya mazoezi na
kula vyakula, vinywaji vyenye nguvu ili
kujipa nguvu.

Pia kama mwanaume ameishi na
mwanawake kwa muda mrefu na
amekuwa na desturi ya kufanya mepenzi
mara kwa mara katika mazingira yale yale
anaweza kukumbwa na kasoro hiyo. Hivyo
anashauriwa kubadili mazingira ya
kufanyia mapenzi, kupeana mahaba
mapya, kuamsha mapenzi kwa kujaliana,
pia kuondoa fikra zote zenye kukinaisha
ikiwa sambamba na kuzingatia usafi wa
mwili. Yakifanyika hayo mwili utaitikia
taarifa ya akili na nguvu zitapatikana.
Kwa wanaoshindwa kurudia tendo
wanatakiwa kufuata kanuni hizo hapo juu.
Jambo kubwa ni suala la kuuzoeza mwili.
Usiulazimishe kuanza mara moja kwenda
mara nyingi wakati mapenzi yako
yamekuwa ya kuiba mpaka baba alale na
wakati mwingine muda wako wa kutoka
kazini umebana na hivyo kukufanya ufanye
mapenzi ya chap chap kila siku. Ukiwa mtu
wa namna hii haiwezi ikatoke siku moja
ghafla tu ukafanya mpenzi mara tatu bila
kuchoka.

Pia inawezekana mwanaume akashindwa
kurudia tendo si kwa sababu hana nguvu
bali hapewi ushirikiano wa kutosha toka
kwa mpenzi wake. Hivyo wakati wa
kutafuta uwezo wa kwenda raundi nyingi
ni vema usaidizi wa mwanamke
ukatolewa, isitokee kupokea lawama tu za
“huwezi, sijatosheka” kwani hizo ndizo
zinazowafanya wanaume washindwe
kabisa kwa hofu kuwa wanaaibika.
Mawazo ya kuaibika yanapopewa
kipaumbele huufanya uume kuzidi
kusinyaa, kwa maana hiyo ni vema
kuyatupilia mbali na kuacha kujihukumu.

Pia kuna hitilafu ya wakati wa
kuridhishana, inaweza kutokea
mwanamke akawa kamaliza raundi yake
ya kwanza, wakati anaingia msisimko wa
pili mwanaume anafika kileleni,
kinachotokea ni mwanamke kumlazimisha
mwanaume arudie tendo kwa muda mfupi
tangu amalize, jambo ambalo ni vigumu.
Sasa ikitokea mwanaume kachezewa na
hana msisimko anapata hofu kuwa
haweze, ikijengeka hivyo hata iweje jambo
halitawezekana tena. Hivyo ni bora
kupeana muda wa kupumzika kabla ya
hatua ya pili ya mchezo.

Pale inapotokea hamasa ya kurudia haipo
fikra za mwanaume zisipewe nafasi ya
kushindwa kwani nyakati, mchoko,
makujukumu, hofu za maisha na mambo
kama hayo yanapokuja katika siku ya
kustarehe ni wazi kuwa kiwango cha
ufanyaji mapenzi kitakuwa chini na hali hii
huwatokea wanaume wote, hata walio
hodari wa kwenda raundi kumi kwa siku.
Sambamba na hilo wanawake
wanashauriwa kutoonesha kujali pindi
inapotokea hali hiyo, badala yake
wawaambie wenzao kuwa siku hiyo
inatosha hata kama hawajatosheka, lengo
ni kuondoa hofu ambayo ndiyo msingi wa
wanaume kuishiwa uwezo wa kufanya
mapenzi. Hata hivyo maudhi, kufanya
mapenzi na usiyempenda, msongo wa
mawazo na kutokuaminiana huchangia
kupoteza msisimko wa kuwa ‘kidume’.
Ushauri wangu ni kwamba chochote
ambacho unataka mwili wako ukifanye
lazima uuzoeze. Ukizoea kuamka saa 12
asubuhi mwili utatii kanuni hiyo. Na
ukizoea kufanya mapenzi kila siku mara
mbili au tatu hali itakuwa hivyo.

Mwisho
katika sura hii ni vema wanaume na
wanawake wakajifahamu kuwa uwezo wa
kufanya mapenzi unapungua kufuatana na
umri isitokee mtu akakosa raha kisa
hawezi kwenda mara nyingi kama zamani
wakati anajua kabisa umri wake umekuwa
mkubwa.

Jamani kutafuta nguvu za ujana zirudie
uzeeni ni kujipa taabu ya bure. Ukiona
umeingia kwenye utu uzima na mwili
wako unaishiwa uwezo, kubaliana na hali.
Lakini jambo la kushangaza siku hizi hata
vikongwe wanapanga foleni kwa
waganga kutafuta tiba ya kufanya mapenzi
mara tatu kwa siku! Mapenzi yanataka
uwezo wa akili na mwili tusishindane na
uwezo asili tutapoteza muda na pesa bure.
Tatizo la mwisho ambalo nalo linatajwa
kuwasumbua zaidi wanaume ni maumbile
madogo ya uume.

Wanaume wengi
wamekuwa wakilalamika kuwa maumbile
yao yanawazuia kuwapa dozi wapenzi
wao. Lakini kama nilivyosema huko nyuma
kwamba mapenzi hayana kanuni kwamba
lazima mtu awe hivi ili amtosheleze
mwenzake. Kinacholeta raha katika
mapenzi ni hisia, hii ikiwa na maana
kwamba mwanaume au mwanamke
anaweza kufurahia mapenzi kwa
kutomasana na kuhamasishana kwa
viungo vingine vya mwili na kujikuta
wameridhika hata bila ya kuingiliana.

Kwa maana hiyo wale ambao
wanamaumbile madogo wanaweza
kutafuta wanawake ambao nao
wanamaumbile ya aina yao. Baadhi ya
watalaam wanasema kwamba kwa
kawaida umbile la nyeti za mtu linakwenda
sambamba na urefu wa mwili wake. Kwa
maana hiyo wanawake wafupi, ingawa si
wote wanatajwa kuwa na nyeti zenye
ukomo mfupi zaidi ya warefu na
wembamba wa umbo.

Mbali na chaguo la mtu mwenye kuendena
naye umbo, wanaume wenye kasoro hii
wanatakiwa kujifunza sana michezo ya
kimapenzi ambayo itawasaidia
kuwafikisha kileleni wapenzi wao. Ni
muhimu kwao kutumia sanaa na mitindo
inayopunguza umbali na ukomo wa nyeti
za kike.

Mwisho ni misingi ya tiba hii:
MOJA ni kuepuka hofu. Ikitokea siku moja
umeshindwa katika tendo haina maana
una kasoro, bali ni hali ya kawaida, hivyo
usiingize huzuni na hofu utakuza tatizo.
Hivyo kwa wale wenye tatizo hili
wapunguze wasiwasi na wajiamini kuwa
hawana tatizo.
PILI, nguvu za kiume zinahitaji mwili
wenye nguvu, hivyo ni busara kula lishe
bora na kufanya mazoezi yasiyokuwa
makali sana.
TATU, kumfundisha mwanamke namna ya
kukusisimua.
NNE, kuepuka mawazo ya kuhuzunisha
wakati wa tendo.
TANO, kupata muda wa kupumzisha mwili.
SITA, kuepukana na pupa, tumia muda
usiopungua takika 20 kufanya romance.
SABA, kujiamini.
SOURCE MANYANDAHEALTH


 

Comments

Popular posts from this blog