LAPF KUTUMIA BILIONI 35 UJENZI WA KITUO CHA MABASI MSAMVU


msamvu 3a13a
Na Fatma Salum na Hassan Silayo- MAELEZO
Mfuko wa pensheni wa LAPF unatarajia kutumia kiasi cha shilingi bilioni 35 katika mradi wa kituo cha mabasi eneo la msamvu Mkoani Morogoro.
Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Meneja wa mfuko huo Kanda ya Mashariki Sayi Lulyalya alisema mradi huo ambao ni ubia kati ya Manispaa ya Morogoro na mfuko wa LAPF unatarajiwa kuanza wakati wowote mwaka huu.
Sayi alisema hatua za awali za utekelezaji wa mradi huo ambao utakamilika baada ya miezi 18 zimeshaanza kwa kuzungushia uzio katika eneo la ujenzi wa kituo hicho.
"LAPF imeamua kutenga takriban bilioni 35 za ujenzi wa kituo cha Msamvu na tunashukuru uongozi wa Manispaa ya Morogoro kwa kutoa eneo la kutosha kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho na michoro imeshakamilika na shughuli za zabuni zinaendelea." Alisema Sayi.
Aidha Sayi aliongeza kuwa mradi huo wa uwekezaji utahusisha ujenzi wa hoteli yenye hadhi ya nyota tano itakayojengwa ndani ya eneo la kituo cha mabasi Msamvu ili kusaidia kuongeza mapato ya serikali.
Mradi wa kituo cha mabasi Msamvu ni muendelezo wa miradi mingi ya uwekezaji inayotekelezwa na mfuko wa pensheni wa LAPF ambapo baadhi ya miradi mingine ni ujenzi wa mabweni chuo cha Hombolo, Kituo cha Afya cha Chuo Kikuu Dodoma, jengo la biashara Mwanza na mradi wa malori na mabasi wa Mbezi Louis.

Comments

Popular posts from this blog