ROONEY NJE KIKOSI CHA MAN UNITED NGAO YA JAMII LEO WEMBLEY


MSHAMBULIAJI wa Manchester United, Wayne Rooney ameenguliwa kwenye kikosi kitakachomenyana na Wigan kuwania Ngao ya Jamii leo kwenye Uwanja wa Wembley kutokana na maumivu ya bega.
Mchezaji mwenye umri wa miaka 27 amekuwa akifanya mazoezi na wachezaji wa akiba na wiki hii aliteuliwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya England kwa ajili ya mechi na Scotland Jumatano.
Rooney amecheza dakika 45 katika mechi za kujiandaa na msimu na huo ulikuwa mchezo wa kirafiki uliochezwa buila mashabiki dhidi ya Real Betis.
Injured: Wayne Rooney has been ruled out of playing for Manchester United in the Community Shield
Majeruhi: Wayne Rooney ameenguliwa kwenye kikosi kitakachomenyana na Wigan leo
Last time out: Rooney scored for England against Brazil in Rio
Rooney aliifungia England dhidi ya Brazil mjini Rio
Rooney ameandika shukrani binafsi kwa kocha wa England, Roy Hodgson baada ya kumjumuisha kwenye kikosi hicho.
Alisema: "Siwezi kuchelewa kujiunga na kikosi cha England na ninatumai kucheza mechi ya ushindani, wakati wote Scotland wapo dhidi yetu. 
"Shukrani kubwa kwa Roy Hodgson kwa kuniteua na kuonyesha imani na sapoti yake, nakubali hii.'
IMEWEKWA AGOSTI 11, 2013

Comments

Popular posts from this blog