Mchakato wa kumrejesha Alex Massawe waiva

alex d1118
Mchakato wa kumrejesha nchini, mfanyabiashara maarufu Alex Massawe, aliyekamatwa Dubai, Falme za Kiarabu, umeanza rasmi baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kutoa hati ya kumkamata na kumrejesha nchini kujibu mashtaka.
Hati hiyo ilitolewa juzi na Hakimu Mkazi Geni Dudu, kufuatia maombi ya Jamhuri, yaliyotolewa na Wakili Mwandamizi wa Serikali Tumaini Kweka, baada ya kumfungulia kesi ya jinai.

Katika kesi hiyo namba 150 ya mwaka 2013, Massawe anakabiliwa na mashtaka ya kughushi na kuwasilisha hati za nyumba.
Massawe ambaye alikamatwa hivi karibu na Shirika la Kimataifa la Polisi (Interpol), amekuwa akitafutwa akihusishwa na matukio ya uhalifu. Mahakama hiyo ilitoa usahihi wa majina yake, kuwa ni Alex Siryamala Massawe.
Kwa mujibu wa Kweka, mtuhumiwa anayeshikiliwa katika nchi nyingine anapoombwa kurejeshwa nchini,lazima kuwe na kesi ambayo anatakiwa kujibu mashtaka, vinginevyo inaweza kuwa vigumu kwa sababu inaonekana kuwa anatakiwa kwa masuala ya kisiasa.
Massawe alikamatwa kati ya Juni 20 na 25, mwaka huu wakati wa ukaguzi kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dubai, kufuatia notisi ya Interpol walioombwa na polisi wa Tanzania kumnasa mfanyabiashara huyo.
Siku chake baada ya kumnasa, Interpol lilimtangaza mfanyabiashara huyo kwenye tovuti yake kama mtu anayetakiwa kukamatwa na kurudishwa Tanzania kujibu tuhuma za uhalifu.
Utaratibu wa Interpol unaelekeza kuwa lazima litolewe tangazo la mtuhumiwa kutakiwa kukamatwa na kurudishwa katika nchi anayotuhumiwa kufanya makosa pale anaponaswa kwenye nchi ya kigeni.
Tangazo hilo kwa kawaida huwekwa picha, maelezo ya mtuhumiwa na alama nyekundu.
Taratibu za Interpol zinasema kuwa mtuhumiwa anayewekewa alama nyekundu ni yule, ambaye anatakiwa kukamatwa na kusafirishwa kwenye nchi anayotafutwa.
Hivyo katika tangazo hilo, lililowekwa kwenye tovuti ya Interpol, picha ya Massawe pia iliwekewa alama hiyo nyekundu kuashiria kuwa anatakiwa kurejeshwa nyumbani kutoka UAE.
Mbali na kesi hiyo, Massawe aliwahi kutajwa katika kesi ya mauaji ya mfanyabiashara Onesphory Kituly.Kituly aliuawa katika mazingira ya kutatanisha Novemba 6, 2011 akiwa nyumbani kwake Magomeni, Dar es Salaam :chanzo mwananchi.

Comments

Popular posts from this blog