KWANINI WATU HUPOTEZA HAMU YA KUJAMIIANA?
Katika utafiti uliofanyika miaka ya karibuni nchini Marekani, imebainika kwamba kati ya ndoa 6,000 zilizovunjika, asilimia 57 zimesababishwa na mwenza mmoja au wote kupenda kuchati au kutumia intaneti kupita kiasi na hivyo kusababisha msisimko kupotea kati ya wenza wawili na hatimaye mwisho ni kupungua uwezo au hamu ya kujamiana. Ni kundi gani la wanawake lililo katika hatari ya kukumbwa na tatizo hili? 1. Wanawake ambao wana historiaya kupungua hamu ya kujamiana 2. Wale ambao wamefanyiwa upasuaji wa kuondoa mayai yao ya uzazi kutokana na sababu mbalimbali 3. Wanawake waliofika umri wa kuacha kupata hedhi (miaka 42-58)) na kupata dalili mbalimbali kama kutokwa na jasho usiku, kukosa usingizi mzuri na msongo wa mawazo. Kwa wanaume, visababishi vya tatizo la kupungua hamu au uwezo wa kujamiana ni kama ifuatavyo; 1. Msongo wa mawazo kama nilivyoeleza hapo juu. Kupungua au kukosekana upendo/mapenzi katika uhusiano/ndoa. 2. Unywaji p