Posts

Showing posts from July 2, 2016

Kayumba Amuumbua Mkubwa Fela

Image
Akiongea kwenye Planet Bongo ya East Afrika Radio, Kayumba amesema pesa bado ipo ingawa imeshapungua, tofauti na alivyosema Mkubwa Fela, na kwamba hata ujenzi wa nyumba bado unaendelea. Kayumba “Hela ipo, ingawa sio tena milioni 50 , itakuwa uwongo nikisema bado ipo milioni 50, lakini zipo siwezi kusema imebakia ngapi, si unaona napendeza nini, nyumba ipo kama nyumba zingine, kawaida siwezi kuzungumzia labda vyumba vingapi, ili mradi nitaweka ubavu wangu nitashukuru Mungu”, alisema Kayumba. Hivi Karibuni kulikuwa na tetesi ambazo zilipigiwa mstari na bosi wa msanii huyo Mkubwa Fela, kwamba pesa alizoshinda msanii huyo zilishaisha kitambo, na nyumba yake ya kuishi ikiwa bado haijakamilika. eatv.tv

Zifahamu Faida/Hasara za kurudiana na Mpenzi wako wa zamani

Image
Kuna faida ya wapenzi kuachana na kurudiana? Vipi kuhusu hasara zake? Hiyo ndiyo mada yetu ya leo kama inavyojieleza. Bila shaka unawajua watu ambao walikuwa wakiishi pamoja kimapenzi, iwe ni ndoa, uchumba au uhusiano wa kawaida ambao wamewahi kutengana na baadaye wakarudiana, iwe ni mara moja au zaidi. Yawezekana hata wewe ukawa miongoni mwa watu wa aina hiyo, kwamba uliwahi kutengana na mtu umpendaye lakini baadaye ukajikuta unarudiana naye na kuanzisha upya uhusiano. Je, kuna faida na madhara gani kwa wapenzi kuachana kisha kuja kurudiana tena na kuanzisha upya uhusiano wa kimapenzi? Ukiwaona watu wanaoishi kwenye aina hii ya uhusiano wa kimapenzi unawachukuliaje? NI JAMBO LA KAWAIDA KATIKA MAPENZI Yawezekana aina hii ya uhusiano wa kuachana na kila mmoja akaendelea na maisha yake kisha baada ya muda mkarudiana tena, likaonekana jambo la ajabu au geni katika mila na desturi za Kiafrika lakini kwa taarifa yako, hili ni jambo la kawaida kabisa katika uhusiano wa kimapenz

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA ZIARA YA RAIS WA RWANDA PAUL KAGAME

Image
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wageni mbalimbali wa ndani na nje ya nchi wakati wa dhifa ya Kitaifa aliyomwandalia Rais wa Rwanda Paul Kagame Ikulu jijini Dar es Salaam.  Rais wa Rwanda Paul Kagame akizungumza na wageni mbalimbali katika dhifa ya kitaifa aliyoandaliwa na mwenyeji wake Rais Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Waziri Mkuu mstaafu Salim Ahmed Salim Ikulu jijini Dar es Salaam mara baada ya kumalizika kwa dhifa ya kitaifa aliyomwandalia Rais wa Rwanda Paul Kagame.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Rais Mstaafu wa awamu ya pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi Ikulu jijini Dar es Salaam mara baada ya kumalizika kwa dhifa ya kitaifa aliyomwandalia Rais wa Rwanda Paul Kagame.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na Ma

Msanii wa Diamond Atuhumiwa Kumbaka Mrembo Jack Wolper....Jack Wolper Afunguka Makubwa

Image
Habari iliyoandikwa kwenye gazeti la Sani la leo jumamosi limemsononesha mrembo Jack Wolper kwa tuhuma za uongo kuwa amebakwa na Msanii wa Diamond... Mwenye Kayaandika haya kwenye ukurasa wake wa Instagram: @wolperstylish - I am so sad kwakweli Hii sio kuniabisha mimi tu, ni kuaibisha na wanawake wenzangu, sijui kwanini magazeti ya kibongo yanatumia Nguvu nyingi kushusha hadhi ya wasanii wa kike haswa.. Nyie SANI no wonder mmepotea katika soko.. Hivi mlivyokua mnachapa mmefkiria kuna wadogo zangu wanasoma?? Au mama angu na baba angu! Naandika kwa uchungu kwakua najua ni limtu limekosa kazi ya kutumia kipaji chake na karama yake vyema linaishia kutumia kwa kuniharibia maisha yangu... Tena front page? Tunafany mangapi mazuri hatuingii page ya kwanza hata siku moja,?! Kesho kutwa nafungua biashara mtaona kama wataandika kitu Ila kwenye ujinga wa kutunga ndo wakwaza Mnaniuzi na nawahakikishia kama Mungu aishivyo mtaona kwa wanenu pia Si mmeamua kuniandika mimi hivi!??

Tamko la RC Makonda kuhusu mashoga waliopo jijini Dar es Salaam

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ametangaza vita na makaka poa (mashoga) na madada poa (makahaba) walioko jijini Dar es Salaam kuwa utaendeshwa msako mkali wa kuwaondoa. Mkuu wa Mkoa huyo aliyasema hayo kufuatia hali ya vitendo hivyo visiyokubalika na jamii kuzidi kushamiri na kuwa kuna hatari kubwa ya watoto wadogo kuiga vitendo hivyo vinavyoleta picha mbaya kwani ni kinyume na maadili ya mtanzania. Aidha alisema hawezi kuifumbia macho hali hii kwani inamomonyoa maadali ya jamii na kuwa yuko tayari kulivalia njuga suala hili ili kuhakikisha anawamaliza wote mkoani Sakati hili la ushoga na ukahaba limeibuka siku za hivi karibuni baada ya kituo cha televisheni cha Clouds Tv kumhoji shoga mmoja ambapo jamii ilipinga kitendo hicho na kuona kama walikuwa wakiuhalalisha ushoga na kuaminisha jamii kuwa ni kitu kizuri.

Nilivyofanya Bonge la Sherehe Baada ya Mke Wangu Kufukuzwa Kazi

Image
Huyu mke nilimuoa akiwa hana kitu, kwa bahati alitafutiwa kazi na ndugu yake kwenye kampuni moja ya simu akawa analipwa kama milioni 3 kwa mwezi fasheni na yeye yeye na fasheni vipodozi kila aina,handbag na nywele za laki mbili ndio mshahara wake ukawa unaishia huko mimi mshahara wangu hauzidi laki sita,nilifanyishwa vituko vyote ndani ya nyumba ,manyanyaso yote ,hapiki hafui,hafanyi chochote ndoa ikawa inaelekea kuvunjika. Nikaenda mahakamani kuprocess talaka wakasema mpaka nianzie baraza la usuluhishi la kata au kanisani,nikaamua kwenda kanisa tulilofungia ndoa tukaitwa kwa Baba Paroko for hearing sijui mediation sijui arbitration sijui mie nikatinga kwa bajaj ya kukodi nimepaukaaa yeye akaja na RAV4 . Baba Paroko alivyotusikiliza akaaniita pembeni akasema kijana hapa nadhani hata tukiomba na kukariri mistari yote ya biblia plus mapambio yote ndoa yako haitarudi kama mwanzo pambana utafute hela ,huyu ni mchaga katumwa pesa mjini Nilisali sana nikasugua goti n