Posts

Showing posts from March 20, 2016

Uchaguzi Zanzibar; Dk Shein, Balozi Seif wapiga kura zao

Image
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ambaye ni mgombea wa Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Dk. Ali Mohamed Shein akipiga kura katika uchaguzi wa marudio kituo cha kupiga kura namba 1 Skuli ya msingi Bungi Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja leo, Wananchi wa Zanzibar leo wanapiga kura katika uchanguzi wa marudio baada ya kufutwa kwa uchanguzi uliofanyika Oktoba 25, 2015 kutokana na kasoro zilizojitokeza. Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Ally Iddi akiwa katika maandalizi ya kupiga kura katika uchaguzi wa marudio kituo cha Skuli ya Kitope, Wilaya ya Kaskazini B, Mkoa wa Kaskazini. Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Ally Iddi akipiga kura katika uchaguzi wa marudio kwenye kituo cha Skuli ya Kitope, Wilaya ya Kaskazini B, Mkoa wa Kaskazini. Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Ally Iddi akizungumza na baadhi ya Waandishi wa Habari mara baada ya

Mbunge Vicky Kamata Afunga Ndoa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Dk. Likwelile

Image
Mbunge wa Viti Maalamu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Vicky Kamata amefunga ndoa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Dk Servacius Likwelile.Dk Likwelile amefunga ndoa hiyo baada ya mkewe wa awali kufariki dunia Mei mwaka 2014.Kwa hatua hiyo, Dk Likwelile amemfuta machozi mbunge huyo kijana baada ya ndoa yake ya awali aliyotarajia kuifunga na Charles Pai kukwama dakika za mwisho wakati wa maandalizi yote ya msingi kukamilika. Dk. Likwelile Habari ambazo Tanzania Daima imezipata, zilieleza kwamba mbunge huyo ambaye ni msanii wa muziki wa kizazi kipya , alifunga ndoa hiyo Septemba mwaka jana katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Geita. Habari zinaeleza kuwa wawili hao baada ya kufunga ndoa, hawakuwa na sherehe kubwa bali walikuwa na ‘pati mchapalo’ iliyofanyika nyumbani kwa Dk Likwelile na kuwashirikisha baadhi ya wana ndugu na marafiki wa pande zote mbili. “Wamefunga ndoa bomani, hakukuwa na sherehe bali kulikuwa na hafla ndogo iliyofanyika nyumbani na wanafamil

Maajabu ya Mungu… Meja Jenerali Afariki, Afufuka!

Image
Meja Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Benjamin Noah Msuya (enzi akiwa kazini). Oscar Ndauka, RISASI JUMAMOSI DAR ES SALAAM: Kweli haya ni maajabu ya Mungu! Meja Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Benjamin Noah Msuya (74), ameanika kwamba, alifariki dunia na mipango ya mazishi ikafanywa lakini siku nne baadaye alifufuka, hapa anasimulia alichokiona baada ya kifo, fuatana na Risasi Jumamosi. Akiwa na famimilia yake wakati akiugua. AZUNGUMZA NA RISASI NYUMBANI KWAKE, DAR Akizungumza na gazeti hili Machi 16, mwaka huu, nyumbani kwake, Kunduchi Beach jijini Dar es Salaam, Msuya ambaye mwaka 1979 aliongoza majeshi ya Tanzania kuingia Uganda kwa mara ya kwanza, alisema kifo chake hicho kilitokana na ugonjwa wa saratani (kansa). MSIKIE MWENYEWE “Awali ya yote, mimi kwa sasa ni Meja Jenerali Mstaafu. Lakini katika utumishi wangu, ndiye niliyeingiza majeshi nchini Uganda mwaka 1979 na kumwangusha mtawala wa mabavu, Idi Amini

LIVE KUTOKA ZANZIBAR MDA HUU.... VIKOSI VYA 'JESHI' VYAIMARISHA ULINZI KWENYE VITUO VYA KUPIGIA KURA

Image
07:50  Safari zote za meli kati ya bandari ya Dar es Salaam na visiwa vya Zanzibar zimekatizwa. Hapa chini ni tangazo la kuwapasha wateja wa Azam Sealink kwamba hakutakuwa na safari za meli kuanzia tarehe 18 hadi 22 Machi kutokana na uchaguzi unaoendelea Zanzibar. Licha ya kukatizwa kwa safari, badi wapo watu waliojitokeza wakitarajia kusafiri. Wengi wa waliofika ni wageni kutoka Ulaya ambao hawakuwa na habari. 07:44  Usalama umeimarishwa visiwani. Hapa chini ni maafisa wa usalama wakiwa na mbwa wa kunusa kabla ya Dkt Shein kupiga kura yake katika kituo cha Bungi, Unguja. 07:42  Baadhi ya wapiga kura wakitafuta majina yao kituoni Madungu Chake-Chake, kisiwani Pemba. 07:30  Mwanamke akipakwa wino kwenye kidole chake baada ya kupiga kura kituo cha Madungu Chake-Chake, Pemba. Baadaye, atabasamu baada kutoka nje ya ukumbi. 07:20  Hii hapa ni picha nyingine ya Dkt Ali Shein, mgombea urais wa CCM baada yake kupiga kura Unguja. 07:05  Mgo

Paul Makonda Azungumza na Watendaji wa jiji la Dar

Image
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza na wenyeviti na maofisa watendaji wa jiji hilo leo kati ka Ukumbi Wa Mwalimu Nyerere asubuhi kuhusu mambo mbalimbali hasu suala la usafi wa mazingira.  Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Theresia Mmbando akiongoza mkutano huo.  Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi akizungumza katika mkutano huo.  Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema akizungumza katika mkutano huo.  Mwakilishi wa Taasisi ya Wakala wa Upimaji Ardhi Tanzania, Linus Kinyondo akizungumzia suala zima la ujenzi wa nyumba kwa kuzingatia mipango miji ili kutunza mazingira.  Wenyeviti na maofisa watendaji wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda (hayupo pichani) Maofisa Watendaji na Wenyeviti wa Manispaa ya Kinondoni wakipiga makofi kwenye mkutano huo. Na Mtandao wa habari za jamii