Posts

Showing posts from December 31, 2014

JE! WAJUA KUWA WEWE UNAWEZA KUWA MCHAWI WA MAHUSIANO/MAPENZI YAKO?

Image
WATU wanaamini mno katika uchawi. Wanamaliza fedha kwa waganga wa kienyeji wakiamini kwamba wamerogwa, hivyo wanatafuta ufumbuzi kutoka kwa wataalamu wa mambo ya asili. Wapo wanaoita mambo ya Kiswahili. Kwangu napinga kuita hivyo kwa sababu nami ni Mswahili na kwa uzoefu wangu, sisi Waswahili hatuna utamaduni wa kutegemea mitishamba kuamua hatma za uhusiano wetu wa kimapenzi.  Ila baadhi wapo, tena wengi haswaaa! Shika hili kwamba wewe mwenyewe pengine ndiye mchawi wa mapenzi yako. Hujiulizi kwa nini wengine wanadumu? Ni vipi wenzi wengine wanaheshimiana? Inakuaje kwako imekuwa kinyume? Siyo suala la upepo, wakati mwingine ni kujitakia. Kivipi mwenzi wako hakuheshimu? Ni makosa gani ambayo wewe umefanya? Ukishapata majibu ya maswali hayo, utaweza kujua faida za wewe kujitambua. Nakuasa ushike moja kuu kwamba mapenzi ni nidhamu. Yapo kama kioo, ukiyaheshimu nayo yatakuheshimu na utayaona murua. Endapo utayachukulia kwa mzaha, n

WATU WANNE WANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA KUTOROKA NA ALBINO MKOANI MWANZA

Image
  Jeshi la Polisi mkoani Mwanza linawashikilia watu wanne akiwemo baba mzazi wa mtoto mwenye ulemavu wa ngozi Albinism aliyetekwa nyara na watu wasiojulikana usiku wakiwa wamelala na kuondoka naye kusikojulikana hali iliyozua hofu kubwa kwa jamii. Amebainisha hayo kamishina msaidizi mwandamizi ambaye ni kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Bw.Valentino Mulowola wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake amemtaja mtoto wa kike aliyetekwa nyara mwenye umri wa miaka minne Pendo Emmanuel mkazi wa kijiji cha Ndambi kata ya fukalo tarafa ya mwamashimba wilayani kwimba ambaye ni mlemavu wa ngozi amesema kuwa tarehe 27 Desemba mwaka huu majira ya saa nne na dakika 30 za usiku watu wasiojulikana walivamia nyumba ya Bw.Emmanuel Shilinde kwa kupiga jiwe mlango na kuvamia kisha wakamchukua mtoto mmoja kati ya watoto watatu waliokuwemo ndani ya nyumba hiyo kisha wakatoweka naye kusiko julikana. Kufuatia hali hiyo makao makuu ya jeshi la polisi Tanzania im

HAPPYNESS MAGESE AMSAPRAIZ JOKATE KIDOTI!

Image
Mwanamitindo maarufu Bongo, ambaye anafanya kazi zake nje ya nchi Happyness Magesse ‘Millen’.Mwanamitindo maarufu Bongo, ambaye anafanya kazi zake nje ya nchi Happyness Magesse ‘Millen’ ambaye pia alishawahi kunyakua taji la Miss Tanzania 2001, ‘amemsapraiz’ mwanamitindo na mbunifu Jokate Mwegelo, kwa kumpatia keki yenye sura ya mdomo wake.Awali, kulikuwa na kikao cha kawaida cha kujadili mambo mbalimbali ya kikazi baina yao kilichofanyika ndani ya hoteli ya Hyatt Kempisky, iliyopo Posta Jijini Dar, lakini kumbe Millen alikuwa ameandaa keki. Mwanamitindo na mbunifu Jokate Mwegelo. “Yaani mimi nilijua tunakutana kama tulivyopanga, lakini cha kushangaza nikakuta watu wakiongozwa na dada yangu Millen wameniandalia keki mbalimbali ikiwemo moja kama mdomo wangu kabisa na kidoti juu, kwa kweli nilifurahi sana siwezi kuelezea,” alisema Jokate

Zari The Bosslady na Diamond Platnumz ni KIMYE wa Afrika!

Image
Kabla ya kukutana na Diamond Platnumz, Zari the Bosslady alikuwa tayari ni mwanamke maarufu nchini Uganda.  Utajiri na urembo wake ulimfanya aitwe Kim Kardashian wa Uganda. Zari anamiliki msululu wa magari ya kifahari yakiwemo Range Rovers, Bentley, Limousine, Mercedes Benz, Chrysler na mengine ambapo mengi kati yake yana plate number za jina lake. Anamiliki mijengo kibao pamoja na biashara mbalimbali kikiwemo chuo kikubwa kilichopo nchini Afrika Kusini. Kukutana na Diamond Platnumz ambaye ukubwa wake tunaufahamu, umemfanya msichana huyo mwenye watoto watatu kuwa na nguvu zaidi na ndio maana couple yao inaweza kufananishwa na ya Kanye West na Kim Kardashian. Kama ilivyo kwa Kimye, Zari na Diamond wana sumaku ya skendo. Ni hivi juzi tu mkanda wa ngono wa Zari ulisambaa mtandaoni ambao uliisha kulikuza tu jina na umaarufu wake. Kwa sasa wawili hao wameanza kuongozana kama kumbikumbi. Baada ya kumsindikiza Diamond kwenye tuzo za Channel O kish

MACHOZI YAWATOKA DIAMOND NA ZARI BAADA YA KUONA MABAKI YA MIILI KATIKA VITA YA KIMBALI NCHINI RWANDA

Image

KUNDI LA ISIS LAWACHINJA WAPIGANAJI WAKE ZAIDI YA 120 KWA KUJARIBU KUTOROKA

Image
Wapiganaji wa ISIS wakiua kundi la watu kwa risasi©RT Kundi hatari linalodai kutetea na kufuata haki za dini ya kiislamu linalopigana nchini Iraq na Syria la Islamic State limewanyonga wapiganaji wake wa kigeni zaidi ya120 kufuatia wapiganaji hao kutaka kuondoka na kurudi makwao na kuachana na kundi hilo. Wapiganaji waliouwawa ni waliokuwa wakitumikia kundi hilo katika mji wa Raqqa nchini Syria walikamatwa wakijaribu kutoroka kurudi makwao kama chanzo cha taarifa hii kilipozungumza na mwandishi wa  The Financial Times  ambaye amedai watu wanaopinga vitendo vya ISIS na utawala wa Rais Bashar al-Assad amesema watu waliouwawa walikuwa wakijaribu kutoroka baada ya ISIS kutoa mwongozo mpya wa wapiganaji wake katika kuwazuia kukimbia. Ingawa kuna wapiganaji wengi kutoka sehemu mbalimbali duniani wanaojiunga na kundi hilo kwakuhadaiwa kwamba ISIS itawasaidia kuielewa vyema dini ya kiislamu na mara baada ya kujiunga wanajikuta walidanganywa na matokeo yake wanajiing

JB WA BONGO MUVI AAMUA KUJIPOTEZA!

Image
Muigizaji mkongwe kwenye filamu nchini, Jacob Steven ‘JB’. MUIGIZAJI mkongwe kwenye filamu nchini, Jacob Steven ‘JB’ ameamua kujipoteza kwa makusudi katika uigizaji akiwa na lengo la kuweka mbele kazi zinazofanywa na kampuni yake ya uzalishaji sinema ya Jerusalemu.Akipiga stori na gazeti hili, JB alisema mwaka 2014 filamu zake tatu za Bado Natafuta, Wageni Wangu na Chausiku zilifanya vizuri sokoni.  “Kwa asilimia 80 mwaka huu kwangu umekuwa mzuri kikazi, nimefanya kazi nzuri bila mimi kuonekana kwa sababu nataka Jerusalemu ianze halafu mimi baadaye ndiyo sababu kubwa iliyofanikisha muvi zangu zote kufanya vizuri, sitaki kuwa naonekana mara kwa mara kwenye filamu,” alisema.

TAZAMA WANAUME WAOANA MBELE YA MAELFU YA WATU KATIKA KANISA LA ...MBELE YA PADRI MARKOS THONG

Image
"Dunia hii itafanywa tupu kabisa, na kuharibiwa kabisa; maana BWANA amenena neno hilo. Dunia inaomboleza inazimia; ulimwengu unadhohofika unazimia; watu wakuu wa dunia wanadhoofika. Tena dunia imetiwa unajisi kwa watu wanaoikaa, kwa maana wameziasi sheria, wameibadili amri, wamelivunja agano la milele". ISAYA 24:3-5. Mambo 3 yamezungumziwa ktk msitari wa 5 ambayo ndiyo sababu ya dunia hii kuwa ktk hali hii mbaya: 1. KUZIASI SHERIA - Hii inamaanisha ni kutenda kinyume na sheria za Mungu zinavyosema 'KUTOKA 20:3-17. 2. KUIBADILI AMRI - Hii inamaanisha kuna amri moja iliyobadilishwa maana inazungumzia uchache. Na ukiangalia leo amri ya 4 ndiyo iliyobadilishwa 'KUTOKA 20:8-11, hata Daniel naye alitabiri kuhusiana na jambo hili "DANIEL 7:25". 3. KUVUNJA AGANO LA MILELE - Agano hili la milele lilivunjwa ni Sabato ya Bwana 'KUTOKA 31:16 "Dunia hii itafanywa tupu kabisa, na kuharibiwa kabisa; maana BWANA amenena neno hilo. Duni

DIVA MWENYE SHEPU YA HATARI BONGO MUVI, MATILDA APIGWA MIMBA TENA FASTA FASTA!

Image
Msanii wa filamu Bongo mwenye shepu ya hatari sana, Wellu Sengo, ‘Matilda’. IMEVUJA! Msanii wa filamu Bongo, Wellu Sengo, ‘Matilda’, licha ya kuwa na mtoto mdogo ambaye hajafikisha hata mwaka, inadaiwa tayari amenasa ujauzito mwingine.Chanzo makini kinaeleza kuwa ujauzito huo ni wa mmoja wa wasanii wenye majina maarufu hapa nchini, ambao wamekuwa katika uhusiano kwa muda mrefu sasa.Katika mawasiliano kwa njia ya simu, Wellu baada ya kubabaika, alikiri kuwa na ujauzito na kumtaja msanii huyo kama ndiye mwenye mzigo, lakini jina lake linahifadhiwa kwa sasa kwa vile mwenyewe hakupatikana ili kuzungumzia madai hayo.  “Haa, wewe nani kakuambia habari hizi, lakini aah, ni kweli bwana nina ujauzito na mwenyewe ni (anamtaja jina). Si unajua tena mambo ya kawaida haya,” alisema muigizaji huyo.  Msanii huyo anayetajwa kuhusika na jambo hilo, ambaye hata hivyo ni mume wa mtu, amekuwa akionekana kuwa Wellu karibu katika maeneo mengi ya starehe na kijamii akiwa. Baadhi ya w

BREAKING NEWS : MTUHUMIWA WA MADAWA YA KULEVYA APIGWA RISASI KATIKA HARAKATI ZA KUTAKA KUTOROKA MAHAKAMANI

Image
Mtuhumiwa wa madawa ya kulevya raia wa Sierra Leone akiwa amepigwa risasi baada ya kutaka kuwatoroka askari magereza katika Mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam.