Posts

Showing posts from May 21, 2015

WACHEZAJI WA MANCHESTER UNITED WALIVYOTOKELEZEA NA WAKE ZAO KATIKA HAFLA YA KUCHAGUA MCHEZAJI WAO BORA 2014/15

Image
Kipa wa Manchester United, David De Gea (kulia) akiojiwa na Jim Rosethal (katikati) baada ya kushinda tuzo ya mchezaji bora wa mwaka 2014/15 wa Man Utd usiku wa kuamkia leo. David De Gea (katikati) alipokuwa akiwasili katika tuzo za Mchezaji bora wa mwaka wa Man Utd. Wayne Rooney akiwa na mke wake Coleen. Mshambuliaji wa Man Utd, James Wilson akiwa na mke wake. Marcos Rojo akiwa na rafiki yake Eugenia Lusardo. Ben Amos akiwa katika pozi na Dani Every. Tyler Blackett akiwa na mke wake Naomi Thomas. Phil Jones akiwa katika pozi na mpenzi wake Kaya Hall. Ander Herrera akiwa na mchumba wake Isabel Collado. Chris Smalling akiwa na mpenzi wake Sam Cooke. Jonny Evans akiwa na mke wake Helen. Michael Carrick akiwa na mke wake Lisa. Victor Valdes akiwa na mpenzi wake Yolanda Cardona. Radamel Falcao akiwa na mke wake Lorelei. Anders Lindegaard akiwa na mke wake Misse Beqiri. KIPA wa Manchester United, David de Gea ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka wa Man

VIUNGO VYA BINADAMU VYAKAMATWA HUKO SIMIYU

Image
WAKAZI wawili wa Kijiji cha Bukigi kilichopo Kata ya Malampaka mkoani Simiyu, wamefikishwa mahakamani kwa kosa la kupatikana na viungo vya binadamu. Waliofikishwa juzi katika Mahakama ya Wilaya ya Maswa mbele wa Hakimu Tumaini Marwa, ni Matheyo Yumbu (50) na Juma Mihangwa (28). Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Nassibu Swedy kuwa Mei 5, mwaka huu, saa 11 alfajiri katika Kijiji cha Bukigi, washitakiwa hao walikutwa wakiwa na viungo hivyo. Alidai viungo walivyokutwa navyo washitakiwa hao ni fuvu la kichwa, mifupa ya miguu na mikono ya binadamu wakiwa wamevihifadhi katika mfuko wa sandarusi katika nyumba waliyoishi. Hata hivyo, washtakiwa hao walikana kosa hilo na kunyimwa dhamana na walipelekwa mahabusu hadi hapo kesi itakapotajwa tena Mei 29, mwaka huu na upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika.

ASIMAMISHWA KAZI BAADA YA KUMTUMIA MESEJI RAIS JAKAYA KIKWETE

Image
Mhasibu wa Hospitali ya Rufaa KCMC,  Paul Mhumba  amesimamishwa kazi kwa tuhuma za kutuma ujumbe wa simu ya mkononi (sms) kwa Rais  Jakaya Kikwete. Kuvuja kwa ujumbe huo na nambari ya simu iliyotuma, kumeibua hisia tofauti kuhusu usiri wa ofisi ya Rais katika kushughulikia malalamiko nyeti ya wananchi na kuwaweka njiapanda watoa habari za siri. Mhumba, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Afya na Serikali Kuu  (TUGHE)  Tawi la KCMC anadaiwa  na Menejimenti ya KCMC kuwa ndiye aliyetuma ujumbe huo. Katika barua yake ya Mei 5, ilidai uchunguzi umebaini kuwa Mhumba ndiye mtumaji wa ujumbe huo. “Uongozi umepokea taarifa iliyotumwa mwishoni mwa Aprili na mwanzoni mwa Mei mwaka huu kwa njia ya ujumbe wa simu kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Jakaya Kikwete,”  . KCMC imedai katika barua hiyo, taarifa hiyo ya sms ilibeba ujumbe unaohusiana na matumizi mabaya ya fedha za hospitali hiyo unaofanywa na baadhi ya viongozi na Shirika la Msamaria M

JE, WAMJUA DADA YAKE NA DAIMOND?

Image
 

MADENTI MSINGI WAJIUZA SH.2000 HUKO MOROGORO!

Image
UKISTAAJABU ya Musa utayaona ya Farao! Kumekuwa na madai ya baadhi ya wanafunzi wa shule za msingi mjini hapa kujiuza kwa waendesha bodaboda kwa gharama ya shilingi elfu mbili tu. Mwanafunzi anayedaiwa kujiuza kwa waendesha Bodaboda. Kufuatia madai hayo, mwandishi wa kikosi cha Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ mjini hapa alifanyia kazi madai hayo na kufanikiwa kumnasa Ally Shabani (34) ambaye ni dereva wa bodaboda akiwa na mwanafunzi wa darasa la nne, Shule ya Msingi ya Kiwanja cha Ndege mkoani hapa (jina tunalo).Tukio hilo la kushangaza na kusikitisha pia, lilijiri Jumamosi iliyopita saa 7 mchana katikati ya mashamba ya mkonge yaliyopo Kihonda Kwachambo ambayo yanamilikiwa na Jeshi la Magereza jirani kabisa la Gereza la Kihonda MAMA MZAZI AISAKA OFM Awali, mama mzazi wa denti huyo, Mariam Jongo alimtafuta Kamanda wa OFM Mkoa wa Morogoro na kumweleza kuhusu tabia ya bodaboda huyo na mwanaye, alisema: ”Naomba msaada wako baba, kuna dereva wa bodaboda nimempa tenda ya kumpeleka m

MASOGANGE ACHAFUA HALI YA HEWA TENA

Image
   

AUNTY EZEKEI IMENIFANYA NISIENDE LONDON MOSE IYOBO AFUNGUKA!

Image
    Imelda Mtema MPENZI wa staa maarufu wa filamu Bongo Aunt Ezekiel, Moses Iyobo ambaye pia ni dansa mahiri wa mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amefunguka kuwa hakwenda kwenye shoo iliyokuwa ikifanyika katika Jiji la London kutokana na hali ya mpenzi wake. Akichezesha taya na Centre Spread, Mose alisema kuwa alishindwa kujumuika na wenzake akihofia hali ya mpenzi wake hivyo alipenda kuwa naye karibu hadi kwenye hitimisho lake la kumpata mtoto wao. “Unajua nashindwa kwenda mbali sana kutokana na hali ya mpenzi wangu kwa kuwa nakuwa na wasiwasi sana hivyo hata London nimeshindwa kwenda kwani natamani kuona hatua kwa hatua ya bebi wangu hadi kumpata mtoto wetu,” alisema Mose.

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS TAREHE 21.05.2015

Image
  MAGAZETI YA UDAKU LEO     MAGAZETI YA MICHEZO NA BURUDANI

COUTINHO MCHEZAJI BORA WA MWAKA LIVERPOOL, BALOTELLI AAAH!

Image
Mbrazil Phillipe Coutinho amewapiga bao wenzake na kuwa mchezaji bora wa mwaka wa Liverpool. Raia huyo wa Brazil mwenye umri wa miaka 22, ametwaa tuzo hiyo ambayo kura zake hupigwa na mashabiki. Pamoja na hivyo, Coutinho amebeba tuzo nyingine tatu zikiwemo za bao bora na aliyeoonyesha kiwango cha juu kwa mwaka mzima. Raheem Sterling ambaye anataka kuondoka Liverpool yeye amekuwa kinda bora wa mwaka. TUZO Player of the Year: Phillipe Coutinho  First Team Players' Player of the Year: Phillipe Coutinho Goal of the Year: Phillipe Coutinho  Performance of the Year: Philippe Coutinho  Young Player of the Year: Raheem Sterling  Ladies Players' Player of the Year: Fara Williams!  Bill Shankley Community Award: Chris Anders Supporters Club of the Year: OLSC London  Academy Players' Player of the Year: Joao Carlos