Posts

Showing posts from August 23, 2016

GARI ALILO PEWA ZAWADI MSANII RAYMOND KATIKA BIRTHDAY YAKE,LINA THAMANI YA TSH. MILIONI 20 0

Image

Exclusive: Vijana Waiba Baraghashia ya Mzee Akilimali, Achimba Mkwara Mzito

Image
Mzee Ibrahim Akilimali maarufu kwa jina la Mzee Akilimali. Taarifa zilizotufikia ni kuwa Mzee Ibrahim Akilimali maarufu kwa jina la Mzee Akilimali ambaye ni katibu wa Baraza la Wazee wa Klabu ya Yanga, amelalamika kuwa kofia yake aina ya baraghashia imeibiwa na mtu ambaye hajajulikana. Baada ya kuibiwa Mzee Akilimali ametoa mkwara mzito kwa yeyote ambaye amehusika kuiiba kofia hiyo ambayo muda wote amekuwa akionekana hadharani ameivaa. Mtu wa karibu wa Mzee Akilimali amesema kuwa mzee huyo alikutwa na mkasa huo jana alipokuwa ameenda kumtembelea mzee mwenzake aliyemtambulisha kwa jina la Mzee Mwika. “Sasa alipofika pale wakawa wamekaa wanapiga soka za hapa na pale, baada ya muda wakatengewa chain a vitumbua lakini Mzee Akilimali yeye huwa anapendelea mihogo na siyo mlaji wa vitumbua, akiwa amevua kofa yake, akaenda jirani kununua mihogo,” alisema mtu huyo wa karibu na mzee huyo. Mtu huyo wa karibu akaendelea kusimulia kuwa: “Aliporejea hakuikuta kofia yake hata

Prof. Lipumba Akana Kuhusika na Vurugu Mkutano wa CUF

Image
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba amesema kuwa hausiki na vurugu zilizoibuka katika mkutano mkuu wa chama hicho uliovunjika juzi Jumapili, Agosti 21, wakati wa uchaguzi wa kujaza nafasi zilizo wazi. Akieleza hayo jana Jijini Dar es Salaam, Prof. Lipumba amekiri kuwa hakualikwa katika mkutano huo lakini aliombwa na baadhi ya wajumbe kwenda kutoa maelezo ya kwanini aliachia nafasi hiyo ya uenyekiti jambo ambalo viongozi waliokuwepo ukumbini hapo hawakulitaka. Prof. Lipumba amesema kuwa anaheshimu maamuzi ya pande zote mbili kwa wanaomtaka arejee nafasi ya uenyekiti lakini pia maamuzi ya chama endapo utaratibu utafuatwa kwa kufuata katiba ya chama na demokrasia ya kweli ndani ya chama hicho. Prof. Lipumba amekataa kuhusika na kukana kutumika na kisiasa na baadhi ya watu ili kukivuruga chama hicho na kusema kuwa viongozi wa chama hicho waepuke maneno ambayo yataweza kukigawanya chama hicho na badala yake wajikite katika kudumi