Posts

Showing posts from November 24, 2013

IZZO B AKUMBWA NA BALAA LA KUKOMBWA KILA KITU ... ISHU NZIMA HII HAPA

Image
Rapper Izzo Bizness asubuhi ya leo ametoa taarifa kuwa internet cafe yake iliyopo Mbeya eneo la chuo cha TEKU imevunjwa na wezi na computer sita zimeibiwa. Ameomba raia wa Mbeya kutoa taarifa wanaposikia mtu anauza computer pasipo njia halali. Soma Hapa Alichoandika Izzo B. #PoleBro

tff yaunda KAMATI NDONGONDOGO

Image
  Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ametangaza wajumbe wa kamati ndogongo (standing committees) wakati zile za haki (judicial organs) na uchaguzi zitaundwa baadaye. Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kikao cha Kamati ya Utendaji kilichofanyika leo (Novemba 23 mwaka huu) jijini Dar es Salaam, Rais Malinzi alisema kamati hizo zimeundwa kwa mujibu wa katiba ili kuisaidia Kamati ya Utendaji. Pia ametangaza wajumbe wanne wa Kamati ya Utendaji aliowateua. Wajumbe hao ni Richard Sinamtwa na Ramadhan Nassib, wakati wengine wanaoingia moja kwa moja kwenye Kamati ya Utendaji kutokana na kamati wanazoziongoza ni Dk. Paul Marealle na Saloum Umande Chama. Kamati ya Fedha na Mipango inaongozwa na Makamu wa Rais wa TFF, Wallace Karia wakati wajumbe ni Francis Ndulane (Makamu Mwenyekiti), Omari Walii, Eliud Mvella, Said Muhammed, Geofrey Nyange, Kidao Wilfred, Ayoub Nyenzi, Lina Kessy na Cyprian Kuhyava. Geofrey Nyange anaongoza Kam

BREAKING NEWS: GARI LILILOBEBA MABOMBA YA GESI LAPATA AJALI NA KUPINDUKA HUKU MTU MMOJA AKIRIPOTIWA KUFARIKI DUNI

Image
  Mmoja ya malori yanayofanya kazi ya kusimba mabomba ya gesi kati ya Lindi na Mtwara imepata ajali katika kijiji cha Mnolewa na mtu mmoja ameripotiwa kufariki dunia. chanzo lindiyetu.  

ZITTO KABWE: SIONDOKI CHADEMA NG'O

Image
Zitto Kabwe akielezea kwa wanahabari kuwa haondoki Chadema kamwe. Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chadema na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe amesema haondoki Chadema ng'o. Adai yeye ni mwanachama halali wa chama hicho, amejiunga na Chadema akiwa na umri wa miaka 16, maisha yake yote ameyatoa kwa ajili ya kukitumikia chama hivyo hawezi kuondoka Chadema. Ameyasema hayo muda huu wakati akiongea na wanahabari katika chumba cha mkutano kilichopo katika Hoteli ya Serena Posta jijini Dar es Salaam. Dk. Kitila Mkumbo akiwaeleza wanahabari kuwa Zitto Kabwe hausiki na 'Waraka wa Siri'. Naye Dk. Kitila Mkumbo aliyevuliwa ujumbe wa Kamati Kuu Chadema amekubali kuwa 'Waraka wa Siri' uliosomwa kwa wanahabari na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu juzi na kusababisha kuwavua vyeo Zitto Kabwe, yeye na Samson Mwigamba ni yeye aliyeuandaa lakini Zitto Kabwe hausiki

WAREMBO WALIVYOPAGAWA KWA P-SQUARE, MMOJA APACHIKWA JINA LA 'ONYINYE' NA KUZAWADIWA SAA YA BEI MBAYA!

Image
Mrembo aliyechunukiwa na Peter akiwa jukwaani baada ya kuitwa na kujitokeza ....akinyoosha mkono… Mrembo aliyechunukiwa na Peter akiwa jukwaani baada ya kuitwa na kujitokeza ....akinyoosha mkono ...akivishwa saa ya bei mbaya na Peter, ambaye alisema ameoa Nigeria wiki iliyopita na Bongo anaoa pia..... ....sogea nikubusu my 'Beautiful Onyinye....! ....mmmwaaaa!!! ....ni kama anamnong’oneza ‘jamani Peter wewe si unanitafutia balaa na mkeo’....hahahahaha!!! ....this is my beautiful Onyinye oooo!!  ".....oooo 'tank' you 'tank' you my Onyinye......!!" .....Mr. P is getting back to business now, lol!!  .....akiimba kwa hisia kali! ...o!o!o!o!, this guy yooo, is crying oohhh!!!  .......jukwaa lilikuwa lao, walilitawala walivyotaka!  ...hapa kazi ni kazi tu! 

TAARIFA YA ZITTO ZUBERI KABWE (MB) KUHUSU KUVULIWA NAFASI ZA UONGOZI NDANI YA CHAMA CHANGU CHA CHADEMA

Image
1. Utangulizi  Katika kikao chake cha siku mbili kilichofanyika tarehe 20 - 22 Novemba 2013, Kamati Kuu ya CHADEMA, pamoja na mambo mengine, iliazimia kunivua nafasi zangu zote za uongozi ndani ya chama. Kwa mujibu wa taarifa ya chama iliyotolewa katika mkutano na waandishi wa habari siku ya Ijumaa tarehe 22 Novemba 2013, ilielezwa kwamba sababu za kuvuliwa uongozi mimi na Dk Kitila Mkumbo ni uhaini na hujuma kwa chama kutokana na waraka unaojulikana kama mkakati wa uchaguzi 2013. Ukweli ni kwamba waraka uliotajwa si sababu ya mimi kuvuliwa nafasi zangu za uongozi kama ilivyojadiliwa katika Kikao cha Kamati Kuu . Sababu za kufukuzwa kwangu kama zilizojadiliwa katika kikao cha Kamati Kuu ni tuhuma lukuki ambazo si mara yangu ya kwanza kuzisikia zikijadiliwa ndani na nje ya vikao vya chama. Hitimisho la tuhuma hizi ni kwamba mimi nimekuwa nikikisaliti chama kwa kutumika na CCM na Usalama wa

MISS ILALA 2013 DORICE MOLLEL HANDS OVER 132 STORY BOOKS WORTH 200,000 TO UKONGA PRIMARY SCHOOL

Image
Mkuki wa Nyota Editor Godance Mkuki (right) hands over 132 story books to Miss Ilala 2013 Doris Mollel at the Ukonga primary school premises in Dar es Salaam during the climax celebration of the International Children’s day. In an efforts to promote a reading culture in the country Mkuki wa Nyota publishers recent during the international children day decided to give 132 story books worth 200,000 to Miss Ilala 2013 Doris Mollel who hands over to Ukonga Primary school. Miss Ilala 2013 Doris Mollel finally hands over story books worth Tsh 200,000 to academic teacher of Ukonga Primary school during the International Children day in Dar es Salaam.

NILIKUWA NAOMBA MUNGU KILA SIKU ILI AFUKUZWE CHADEMA’ - MAMA ZITTO

Image
Siku moja baada ya Kamati Kuu ya Chadema kumvua uongozi aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Taifa wa chama hicho, Zitto Kabwe, mama yake mzazi, Shida Salum ametoa ya moyoni akieleza kuwa kilichomkuta mwanaye kimefunika mabaya mengi yaliyopangwa afanyiwe. "Kwa upande wangu naona kama ni ushindi kwa Zitto kutokana na jinsi ninavyojua hali ilivyo, mambo yalikuwa ni mengi mno na nikwambie tu, Zitto kuvuliwa uongozi kumefunika hayo yaliyokuwa yamekusudiwa kufanywa dhidi yake. Nilikuwa naomba Mungu kila siku ili afukuzwe Chadema," alisema mama huyo wakati akizungumza na gazeti hili nyumbani kwake Tabata, Dar es Salaam. Shida Salum alisema kuwa Mungu amemnusuru mwanaye na kusisitiza, "Watu walikaa na kutengeneza ripoti ya siri kuhusu Zitto na kuiweka kwenye mtandao kisha kuituma kwa wanachama wa Chadema wanaowafahamu. Mpaka wanafikia hatua hiyo maana yake ni kwamba wamejaribu njia zote za kummaliza, lakini wameshindwa. Alisema kutokana na

REAL MADRID WAUA GOLI TANO BILA DHIDI YA ALMERIA

Image
Kings of Spain: Cristiano Ronaldo and Gareth Bale celebrate after Real Madrid score their first Cristiano Ronaldo scored the first as Real Madrid stormed to a easy victory against Almeria but had to come off in the second half due to a hamstring injury. The official line was that the substitution was made as a precaution, but it will no doubt worry Madrid fans ahead of their Champions League math with Galatasaray on Wednesday. After the game, Carlo Ancelotti said: 'Cristiano has a problem with the hamstring but it appears to be a just a strain; nothing serious.' Still going: Real are trying to keep pace with Barcelona at the top of La Liga Almeria made the goals smaller ahead of their meeting but it didn’t stop Ronaldo and Gareth Bale both scoring. Simple finish: Bale scored the third for Madrid and his fifth in Real colours Pace and power: Real Madrid&#

Ridhiwani Kikwete alaani siasa za Chuki n Ukanda zilizowatoa madarakani Zitto Kabwe na Dr. Kitila Mkumbo.

Image
Baadhi  ya watu maarufu  nchini akiwemo  mtoto wa Rais Kikwete, Ridhiwan wamezipokea taarifa za kuvuliwa wadhifa  wa unaibu Katibu Mkuu wa CHADEMA kwa Zitto Kabwe kwa mitazamo tofauti. Zitto alivuliwa uongozi wa Naibu Katibu Mkuu Taifa na Naibu Kiongozi  wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwa tuhuma za kukisaliti chama hicho. Haya  ni maoni  ya  Ridhiwani  Kikwete  aliyoiweka  katika ukurasa  wake  wa  facebook na  twitter kuhusiana  na  sakata  hilo: Naendelea kujifunza matunda ya Siasa za Chuki na Ukanda zinavyoumiza  siasa za Tanzania. Mungu anatuasa kupitia vitabu vitakatifu kuwa ” ili  kuepusha balaa dogo kutokea, basi liwe balaa kubwa zaidi ya hilo.”.  Imani kuwa aliloandika limetimia…     Zitto Kabwe pamoja na Dk Kitila Mkumbo watakutana na wahariri na waandishi wa habari  LEO Jumapili  kuzungumzia hatua hiyo.