Posts

Showing posts from March 30, 2016

ORODHA YA WATUMISHI HEWA NCHI NZIMA YATUA SERIKALINI

Image
HATIMAYE wakuu wa Mikoa yote nchini wametii agizo la Rais John Magufuli lilokuwa linawataka wasilishe ripoti ya idadi ya watumishi hewa kwenye mikoa husika. Wakuu hao wa mikoa wapya wamewasilisha ripoti za watumishi hao leo Jijini Dar es Salaam,Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa,Georgy Simbachawene ili kuchukuliwa hatua za kisheria  kwa watumishi waliohusika katika kashfa hizo,   Mkoa wa Dar Es Salaam . Akiwasilisha ripoti ya watumishi hewa.Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema katika mkoa wake baada ya kufanya uchunguzi kwa kushirikiana na kamati mbali mbali wamebaini kuwepo kwa watumishi hewa 73 ambao watumishi hao hewa wamepelekea serikali kupotea pesa zaidi ya Milioni 316 kwa mwaka mmoja. “Katika mkoa huu tumepata watumioshi hewa 73,ila wengi watahoji mkoa huu mkubwa kwanini unakuwa na watumishi hewa wachache,nakata kukwambia Waziri, bado tunaendelea na uchunguzi wa kina”amesema Makonda . Mkoa wa Arusha.

MWANASAIKOLOJIA ANT SADAKA AONGEA NA WANAWAKE WA DODOMA KWENYE MAFUNZO YA WAJASIRIAMALI YANAYOENDESHWA NA TAASISI YA MANJANO FOUNDATION

Image
Mwanasaikolojia Anti Sadaka akitoa Mada kwenye Mafunzo ya ujasiriamali kwa wanawake wa Mkoa wa Dodoma yanayoendesha na Taasisi ya Manjano Foundation yanaoendelea kwenye ukumbi wa LAPF House. Mwanasaikolojia Anti Sadaka amewafunda wanawake waDodomawanaoshiriki mafunzo ya ujasiriamali ya kujikita katika biashara ya Vipodozi vya LuvTouch Manjano. Mafunzo hayo yanaendeshwa na wataalamu kutoka taasisi ya Manjano Foundation na mkufunzi wa maswala ya Biashara mjini Dodoma yanayoendelea kwa wiki nzima.  Washiki Kutoka Mkoani Dodoma na Maeneo Jirani wakiliskiliza kwa Makini Wakati wa Mafunzo hayo Leo. Anti Sadaka amewataka wanawake hao kujitambua kwa lengo la kufikia malengo yao waliojiwekea. Akieleza zaidi katika semina hiyo amewataka wanawake hao kujitambua wao ni nani, wajiamini, watambue vyeo vyao katika familia, wana nafasi gani kwenye jamii inayowazunguka, kufanya kazi kwa bidii na kudumisha nidhamu yao kwa kila wakifanyacho kwa lengo la kufikia malengo y

Waliompiga Daktari Mkoani Mtwara Wakamatwa Wakijiandaa Kutoroka Kwenda Nje ya Nchi

Image
Kufuatia tukio la ndugu wa mgonjwa kumpiga Daktari Mkoani Mtwara, tayari jeshi la Polisi Mkoani humo linawashikilia watu kadhaa kwa kitendo hicho cha kumpiga Daktari wakati akiwa katika majukumu yake ya kikazi. Kamanda wa Polisi mkoa wa Mtwara,Henry Mwaibambe (Pichani) amesema hadi sasa watu 2 wanaotuhumiwa kumpiga daktari hospitali ya Mkoa wamekamatwa usiku wa kuamkia jana wakitoroka nchini huku wengine 3 wakiendelea kusakwa. Awali wauguzi na Madaktari wa Hospitali hiyo waligoma kufanya kazi hadi hapo watakapohakikishiwa usalama wao ndipo wafanye kazi Jana, Waziri wa Afya Ummy Mwalimu aliweza kufika Hospitalini hapo na kusuluhisha mgogoro huo huku akiomba Jeshi la Polisi kuongeza usalama kwa watumishi hao wa Afya.

WAFANYAKAZI 3 TANESCO WATIWA MBARONI KUFUATIA KIFO CHA MFANYAKAZI MWENZA

Image
Wafanyakazi watatu wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) mkoani Morogoro, wanashikiliwa na Polisi wakihojiwa kutokana na kifo cha mfanyakazi mwenzao, Deo Elias (30), mkazi wa Mazimbu, Manispaa ya Morogoro kwa kunaswa na umeme juu ya nguzo. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 5.30 asubuhi maeneo ya Mafiga, wakati Elias akiwa na wafanyakazi wenzake katika eneo la kazi. Kamanda Matei alisema Elias alipokuwa na wenzake katika eneo hilo wakirekebisha umeme, alinaswa na kufa papo hapo. Meneja wa Tanesco Mkoa wa Morogoro, Mhandisi John Bandiye akizungumzia tukio hilo ofisini kwake jana, alisema Elias alikuwa katika kazi za kawaida kama fundi na tukio hilo limetokea kwa bahati mbaya. Mhandisi Bandiye alisema mfanyakazi huyo alikuwa akirekebisha njia ya umeme ya Ngazengwa iliyopo eneo la Mafiga na ilikuwa imezimwa, lakini cha kushangazwa ilikuwa na umeme uliosabab

EMPLOYMENT OPPORTUNITIES

Image
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA MINISTRY OF HEALTH, COMMUNITY DEVELOPMENT, GENDER, ELDERLY AND CHILDREN PRIVATE HEALTH LABORATORIES BOARD EMPLOYMENT OPPORTUNITIES Private Health Laboratories Board (PHLB), is the Government Institution under the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children which registers and manages all Private Health Laboratories in Tanzania (Mainland), Vacancies exist at the Board`s Head Office in Dar es Salaam and applications from suitably qualified and competent persons are invited to fill the following posts:- 1.    Laboratory Quality Assurance Officer (1 post) Duties and Responsibilities •    To implement activities involved in Laboratory Quality Assurance Framework, Laboratory Standard Guidelines, training curriculum and modules so that they meet International standards requirements. •    To monitor quality of health Laboratory Services in supporting the provison of essential intervention health packages in the

RAIS MAGUFULI APOKELEWA KWA SHANGWE ALIPOTUA MWANZA KWA MUDA AKIELEKEA CHATO

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na umati wa watu uliojitokeza kumlaki baada ya kutua kwa muda uwanja wa ndege wa Mwanza akiwa anaelekea nyumbani kwake Chato mkoani Geita leo Machi 29, 2016.   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiburudishwa na ngoma za Utamaduni baada ya kutua kwa muda uwanja wa ndege wa Mwanza akiwa anaelekea nyumbani kwake Chato mkoani Geita leo Machi 29, 2016.   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Askari wa Kikosi cha  Zimamoto na Uokoaji wa Uwanja wa ndege wa Mwanza baada ya kutua kwa muda  akiwa anaelekea nyumbani kwake Chato mkoani Geita leo Machi 29, 2016  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na wafanyakazi wa Uwanja wa ndege wa Mwanza baada ya kutua kwa muda  akiwa anaelekea nyumbani kwake Chato mkoani Geita leo Machi 29, 2016.  Rai