Posts

Showing posts from December 2, 2015

MHE. BALOZI SEFUE AENDELEA KUWASISITIZA WATUMISHI WA UMMA KUVAA BEJI ZINAZOWATAMBULISHA MAJINA YAO WANAPOKUWA KATIKA MAENEO YA KAZI

Image
Katibu Mkuu Kiongozi  Mhe. Balozi Ombeni Sefue akiwaonyesha waandishi wa Habari (hawapo pichani) beji yenye jina lake ambayo amewaagiza watumishi wa Umma kuivaa wanapokuwa  katika maeneo  yao ya  kazi. Balozi Sefue alifanya mkutano na waandishi wa habari Ikulu jijini Dar es Salaam jana na kutoa taarifa ya Serikali kuhusu kesi ya Serious Fraud Office (SFO) dhidi ya Standard Bank . Na Anna Nkinda – Maelezo Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi Ombeni Sefue ameendelea kuwasisitiza watumishi wa Umma kuvaa beji zinazowatambulisha majina yao wanapokuwa  katika maeneo  ya  kazi. Mhe. Balozi Sefue aliutoa mwito huo jana wakati akijibu swali la Mwandishi wa Habari aliyemuuliza ni kwanini alikuwa amevaa beji yenye jina lake ambayo imemfanya kuonekana tofauti na siku zingine. Alisema mwishoni mwa mwezi wa kumi na moja alifanya ziara ya kutembelea Hospitali ya Taifa Muhimbili na kuagiza  watumishi wote wa Umma kuvaa beji zinazowatambulisha majina yao. “Nimeamua kuonyesha mfano kwa vitendo

Mwanamikakati wa Lowassa Ahusishwa na Wizi Mkubwa Stanbic

Image
 Bw. Bashir Awale Kulia Mwenye Tshirt ya Njano Akisalimiana na Lowassa Siku chache baada ya uchaguzi serikali ya Tanzania ilimfukuza mtu aliyejulikana alikuwa mashauri wa Kimkakati wa Mgombea Urais kupitia Chadema, Bw. Bashir Awale (Mkenya ashikiliwa na Polisi nchini TZee kwa kumpigia debe Lowassa kipindi cha campaigns), kwa kuishi kimakosa nchini. Pia, ilijulikana kuwa kabla ya kuanza kujihusisha na siasa, hasa kuwa mshauri wa Ndugu Lowassa katika kuusaka urais alikuwa mmoja wa Maofisa Wandamizi wa Benki ya Stanbic. Katika sakata linalohushisha benki ya Stanbic kufanya udanganyifu mkubwa wa kujipatia fedha na kushitakiwa na Idara ya Makosa ya Uingeleza huyu jamaa katokea. Na imeonyesha alifukuzwa katika wakati huu baada ya kufanya wizi huu kwa kushirikiana na ndugu wa karibu wa Lowassa na aliyekuwa Miss Tanzania 1996, Shose Sinare. Kwa mjibu wa serikali, tayari uchunguzi umeanza kufanyika ili kubaini aliyefaidika na pesa hizo. Aidha, hukumu iliyofanyika jana imeamuru serikal

BREAKING NEWZZZZZ!!!! DR.SLAAA ATOA KAULI HII NZITO MDA HUU KWA RAIS MAGUFULI

Image
 Katibu Mkuu wa zamani wa Chadema, Dk. Wilbroad Slaa amesifia kasi ya rais John Magufuli hasa katika kupambana na ufisadi nchini. Dk. Slaa amesema kuwa alichowahi kukizungumzia awali kimetimia kwa kuwa nchi hii ilihitaji mtu kama Magufuli. “Nadhani sasa unaelewa niliposhikilia msimamo wangu. Katika mazingira ya sasa Magufuli ni bora zaidi. Niliwahi kusema kuwa hii nchi kwa siku za mwanzo inahitaji udikteta kuirudisha kwenye mstari ulioonyooka, nimefurahi sana,” Dk. Slaa ameliabia gazeti la Raia Mwema. Amesema kuwa Bunge linatakiwa kufanya kazi ya kuudhibiti udikteta huo ili usivuke mipaka lakini limuunge mkono kwa hatua anazochukua. Katika hatua nyingine, Dk. Slaa amemshauri Rais Magufuli kuiangalia Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na kuifumua. “Pasipo kuchukua hatua ya kuifumua Takukuru, sina hakika kama matarajio yatafikiwa,” alisema Dk Slaa na kuongeza kuwa hatua hizo zinapaswa kuchukuliwa haraka.

Bi harusi amuua bwana harusi kwa kisu

Image
Marehemu Geofrey enzi za uhai wake. Na Makongoro Oging’ MADAI MAZITO!   Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni, Dar limesema linamshikilia mwanadada Rhoda Daudi kwa tuhuma ya kumuua kwa kumchoma kisu, Geofrey Valeli Kapulula (37) aliyetarajia kufunga naye ndoa hivi karibuni, Uwazi lina mkasa wote. Tukio hilo la kutisha na ambalo limeacha maswali, lilijiri maeneo ya Ubungo National Housing (NHC) jijini Dar es Salaam, Novemba 23, mwaka huu. Bi harusi anayetuhumiwa kwa kosa la kumchoma kisu   Geofrey. UWAZI ENEO LA TUKIO Mwandishi wa habari hii, alifika katika eneo la tukio na kuzungumza na majirani ambao walisema kwamba siku ya tukio walisikia sauti ya marehemu akiomba msaada lakini hata hivyo, hawakujali kutokana na kuzoea wawili hao kugombana mara kwa mara na kisha kupatana. Mmoja wa majirani hao ambaye hakupenda jina lake kuandikwa gazetini, alisema siku ya tukio, wapendana hao walikuwa wakinywa kwenye baa moja na marafiki zao huku wakibadilishana mawazo lakini kukatokea

Basi lagongana na lori na kuua watu Singida

Image
Habari zilizotufikia hivi punde ni kwamba watu kadhaa wamepoteza maisha katika ajali mbaya iliyotokea baada ya basi la abiria la Takbir lenye namba za usajili T 230 BRJ lililokuwa likitokea jijini Dar es Salaam kwenda Mwanza kugongana uso kwa uso na lori eneo la Shelui mkoani Singida usiku huu.

MISS TANZANIA USA 2015-2016 AEESHA KAMARA ASHINDA KUWA COVER GIRL KWENYE CALENDA YA MISS AFRICA USA 2015-2016

Image
 Miss Tanzania USA 2015-2016 Aeesha Kamara (kushoto) akiibuka mshindi na kuwa Cover Girl kwenye Kalenda ya Miss Africa USA 2015-2016 shindano ililofanyika New York siku ya Jumamosi Novemba 28, 2015.  Mamiss wengine walioshiriki shindano hilo wakipita mbele ya majaji.  Wadau wakipata picha na mamiss wakati mratibu wa mashindano ya miss Africa Lady Kate alipokua akitangaza shindi. Ma Winny Casey (gauni jeusi) pamoja na Lady Kate (mwenye miwani) wakiwa na mamiss.

Dereva achinjwa kikatili

Image
Salum Masoud enzi za uhai wake. Na Boniphace Ngumije INASIKITISHA! Salum Masoud (35), mkazi wa Kijichi, Rufiji mkoani Pwani ambaye alikuwa dereva wa magari ya kubeba mizigo mkoani humo ameuawa kikatili kwa kuchinjwa na watu wasiojulikana na ifuatayo ni simulizi ya kusikitisha kutoka kwa dada wa marehemu aitwaye Hawa Masoud, mkazi wa Mbagala, Dar. Akifuta machozi na kuzungumza kwa kwikwi na gazeti hili hivi karibuni, Hawa alisema mazingira ya tukio la kuchinjwa kwa ndugu yake yamejaa utata. “Taarifa za kuuawa kwa kaka yetu zilitufikia Novemba 10, mwaka huu baada ya watu wasiojulikana kumpigia simu dada wa mke wa marehemu na kumtaarifu. “Binafsi nilishtushwa sana. Ilikuwa vigumu kuamini. Lakini hatukuwa na budi kukubaliana na hali halisi, tukaamua kukusanyana na kwenda eneo la tukio kufahamu nini kilitokea mpaka Salum akauawa kikatili namna hiyo. “Tulipofika tulimkuta bosi wa marehemu aitwaye, Salum Bakari Mnolage akifanya taratibu za mazishi. Tulimkataza lakini akatuiti

MAGAZETI YA LEO JUMATANO ya trh 02/12/2015

Image
. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

KILA WAZIRI ATASAINI MKATABA KABLA AJAANZA KAZI - MAGUFULI

Image
Kusuasua kwa Rais John Magufuli, kutangaza Baraza la Mawaziri kunatokana na msimamo wake wa kuwachambua watu anaotarajia kuteua katika nafasi hiyo huku akiaandaa mikataba ya makubaliano itakayokuwa mwongozo kwa mawaziri hao. Nia ya Rais, hadi kufikia hatua hiyo imetafsiriwa kwamba anataka kupata mawaziri ambao wataweza kwenda sambamba na kasi yake pamoja na wawajibikaji. Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kinaeleza kwamba kwa sasa Rais Magufuli, anasuasua kutangaza baraza lake kutokana na kile kinachodaiwa ni kuandaa mikataba ambayo mawaziri baada ya kuteuliwa watalazimika kuisoma kwa muda wa siku mbili kabla ya kukubali uteuzi huo. Chanzo hicho, kilieleza kwamba wale watakaokubali itabidi wasaini mkataba huo ili kukukabiliana na matakwa ya mkataba huo. “Kwa sasa huyu jamaa anaandaa mikataba kwa ajili ya kuwapatia Mawaziri na Manaibu wake na wanatakiwa kuisoma ndani ya siku mbili na yeyote atakayekubaliana na mkataba huyo atalazimika kuisaini. “Mikataba

Kashfa nzito

Image
Wasomali wakiwa chini ya ulinzi. WAMENASWA! Jeshi la Polisi Kituo cha Buguruni kwa kushirikiana na Serikali ya Mtaa wa Machimbo, Kata ya Segerea, Ilala jijini Dar es Salaam wamewanasa watu 105 raia wa Somalia wakidaiwa kuwa safarini kwenda nchini Afrika Kusini, Uwazi linakupa kwa undani. Tukio hilo la kushangaza lilitokea saa 11 alfajiri ya Alhamisi iliyopita kwenye nyumba ya kigogo mmoja aliyekuwa mfanyabiashara mkubwa Dar (jina lipo) ambaye ni marehemu. Nyumba hiyo iliyopo Tabata Segerea kwa sasa inasimamiwa na mtoto wa marehemu aitwaye Mariam. Polisi wakiwa katika eneo la tukio. Waadishi wa habari hii walifika eneo la tukio muda mfupi baada ya kukamatwa kwa watu hao ambapo zoezi hilo lilikuwa likiongozwa na Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Kipolisi Buguruni, Ibrahim Nkindwa na Mkuu wa Kituo cha Polisi Tabata Shule, Bakar Goti baada ya kutonywa kuwepo kwa watu hao katika nyumba hiyo iliyopangishwa kwa Zabibu Umwiza raia wa Burundi ambaye ndiye anadaiwa kuwahifadhi w