Posts

Showing posts from March 13, 2014

BEAKING NEWZ:"HATARI: VURUGU ZATOKEA ZANZIBAR, MAGARI YA SERIKALI YAPIGWA MAWE"

Image
Kwa mujibunnwa taarifa za mitandaoni huko Zanzibar kumetokea vurugu,kupiga mawe magari ya serikali huku wafanyakazi wa serikali wakijeruhiwa ..  Picha hapo juu inaonesha gari la Katibu mkuu wizara ya fedha na uchumi mheshimiwa Khamis Musa likiwa limepinduliwa, katika gari hakuwemo katibu huyo mkuu bali  alikuwemo dereva wake ambaye mpaka sasa hali yake inaendelea vizuri, Tutaendelea kuwapa taarifa zaidi.  Habari zaidi za matukio na picha zingine zaidi tutaendelea kuwaletea kama mwandishi wetu atakavyotujuza, endelea kujiunga nasi zaidi.

PINGAMIZI DHIDI YA MGOMBEA WA CHADEMA CHALINZE

Mimi  FABIAN L. SKAUKI, mgombea ubunge wa uchaguzi mdogo jimbo la CHALINZE kwa Ticket ya THE CIVIC UNITED FRONT (CUF) ninamwekea Pingamizi mgombea wa chama cha demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)  kwamba amepoteza sifa za kuwa mgombea kwa sababu zifuatazo. 1.       Ndugu MATHAYO. M. TORONGEY amejaza Taarifa za uongo kwenye Fomu yake kwamba kazi anayoifanya ni BIASHARA. Sio kweli, kwa sababu hajaweka vielelezo vya yeye kufanya hiyo kazi. Hajulikani anafanya kazi gani. 2.       Ndugu MATHAYO .M. TORONGEY amejaza  katika fomu kwamba anajua kusoma na kuandika Kiswahili na kiingereza. Taarifa hizi ni za uongo, mgombea huyu hajui kusoma wala kuandika Kiswahili wala kiingereza, na kwamba amedanganya na amepoteza sifa za kuwa mgombea. 3.       Ndugu MATHAYO .M.TORONGEY  amedanganya kwa kughushi/kufoji sahihi za wadhamini,ambao amewaorodhesha kwenye fomu ya kuomba kuthibitishwa kuwa mgombea. Ambapo katika fomu hizo wadhamini wote sahihi zao zimefojiwa na hazifanani

MIMI NI NOUMA...KATIKA MAPENZI ATAKAYENIOA ATAFAIDI MAHANJUMATI..."MAYA AFUNGUKA..!

Image
MWIGIZAJI mkongwe Bongo, Mayasa Mrisho ‘Maya’ amesema licha ya kuwa bado hajaolewa lakini atakayemuoa atafaidi mapishi yake kwani ni fundi wa kupika. Mayasa Mrisho ‘Maya’.   Maya alifunguka hayo juzikati wakati paparazi wetu alipombananisha juu ya uwezo wake kwenye ‘sekta’ ya mahanjumati ndipo alipofunguka kuwa yeye ni hodari katika eneo hilo.   “Wee… mi noma katika mapishi, siwezi kuachika kwa sababu ya kushindwa kupika, atakayenioa atafaidi mahanjumati ya ukweli kabisa, chezea mimi wewe!” alijisifia Maya.

WEMA NA AUNT EZEKIEL WACHEZEA KICHAPO CHA NGUVU...KISA?!!

Image
KIMEWAKA! Habari zilizothibitishwa zinaeleza kuwa, sura mbili za mauzo kwenye sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu na Aunt Ezekiel Grayson wanadaiwa kula kichapo kutoka kwa msanii mwenzao, Adam Kuambiana, Amani limeinyaka. Tukio hilo lililoshuhudiwa na ‘shushushu’ wetu lilijiri mchana kweupe maeneo ya Mikocheni, Dar, hivi karibuni baada ya kuibuka timbwili lenye ujazo wa kilo kadhaa baina ya mastaa hao.   ALIANZA WEMA Kwa mujibu wa chanzo, Wema ndiye aliyeanza kummwagia Kuambiana maneno ya shombo akimwambia kuwa ahakikishe siku hiyo haipiti bila kukata kucha za miguuni kwani ni ndefu na zinatisha. “Mwanzoni ilikuwa kama utani tu. Wema alimwambia Kuambiana akate kucha, tena itabidi atumie mkasi wa kukatia michongoma maana kwa wembe hazikatiki.   “Pia Wema alimwambia yeye hawezi kumwacha mpenzi wake na kucha ndefu kama hizo za Kuambiana,” kilisema chanzo chetu. Ilizidi kudaiwa kwamba wakati Wema akiendelea ‘kumpaka’ Kuambiana, Aunt aliyekuwa amejilaza chini alida

ANGALIA PICHA UKATILI DHIDI YA WATOTO BADO NI TISHIO MBEYA

Image
 Mtoto Anjela Rashid[4]amechomwa moto mikono yote miwili  na baba yake mzazi baada ya kula finyango mbili za nyama zilizopikwa na Baba yake huyo John Msumba[3]ambaye amekuwa akipigwa mara kwa mara na wakati wote kufungiwa ndani kwa kufuli pia kunyimwa chakula na shangazi yake  ANGALIA PICA ZAIDI HAPA

MAAJABU YA DUNIA; HUYU NDIYE MCHINA ANAYEKULA NYAMA ZA WATOTO BINAADAMU!!

Image
  ANGALIA PICHA ZAIDI  

HIZI NDIZO DALILI 10 ZA MWANAUME ULIYE NAYE SI WAKO PEKE YAKO

Image
Wakati mwingine ni vigumu kuamini, lakini jambo hili huwatokea wanawake wengi kwamba wanaume wanaotoka nao kuna uwezekano mkubwa wakawa wanatoka na wanawake wengine kwa nyakati tofauti na hufanya hivyo kwa siri sana. Inaweza ikawa ni mitoko ya kawaida lakini miongoni mwa hao wanaotoka nao wapo ambao watakuwa wanashiriki tendo na wakawa wameahidiwa kuolewa. Hapa chini nitaeleza dalili zinazoweza kuwafanya wanawake kujua kwamba mwanaume anayetoka naye sio wakwake peke yake bali kuna wengine wanadanganywa huko waliko kama yeye. 1. Mnakuwa na ratiba ya kukutana siku maalum Baada ya kujuana unagundua kwamba bwana uliye naye anakuwa na kawaida ya kukutana na wewe kwa siku maalum tena anazopanga yeye, mwanaume anakuwa hana nafasi ya kushtukizwa miadi na akipanga ratiba yake hawezi kuibadilisha kirahisi. Anaweza kukupangia muwe mnakutana mara mbili kwa wiki na siku nyingine anasema yuko bize. Hapa inabidi ujiulize mara mbili. 2. Ugumu katika kukubali miadi: Kama inatokea

NILIMKANYA SANA BINTI KIZIWI KUHUSU ISSUE YA MADAWA YA KULEVYA ILA HAKUNISIKIA”…Z-ANTO

Image
Muimbaji wa muziki aliyewahi kuhit na wimbo wake ‘Binti Kiziwi’ Z-Anto amesema aliwahi kumkanya aliyekuwa mke wake, Sandra (msichana aliyeigiza kwenye video ya wimbo wake Binti Kiziwi), kuachana na makundi hatarishi aliyoanza kuwa nayo baada kupata umaarufu ambayo yalimfelisha kimaisha ikiwemo kufungwa jela nchini China baada ya kukamatwa na madawa ya kulevya. “Alishindwa kujicontrol na maisha ya ustaa hiyo ndio ikawa shida, akapata kampani za ajabu ajabu,” Z-Anto alimwambia jana mtangazaji wa kipindi cha Mseto cha Radio Citizen ya Kenya, Willy M Tuva. Muimbaji huyo amekumbushia kuwa wiki moja kabla ya msichana huyo kusafiri kwenda China, ndio kipindi ilipotokea ajali ya Sharo Milionea, na kulikuwa na tetesi pia kuwa Sandra naye alipata ajali na kupoteza maisha na hivyo kumlazimu kufuatilia undani wake. “Mwisho wa siku kama siku tatu nikampata, akaniambia ‘mbona mimi niko fresh’, nikamuuliza ‘mbona nimesikia umepata ajali’ akasema ‘hapana mimi niko sawa

HAYA NDIO MAMBO NANE(8) AMBAYO HUTAKIWI KUYASEMA KWENYE VIKAO

Image
Kama unaingia kwenye kikao, unatakiwa uonyeshe uwezo wako wa kuchangia ili mambo yaende vizuri na kuwa bora zaidi, usiongee vitu vya kukatisha tamaa au visivyokua na tija. 1. Ngoja nikupe rejea kuhusu jambo hilo.. . Rejea sio jambo baya kama ni nzuri na imefanywa vizuri inasaida kundi kupata suluhisho la jambo fulani, lakini wakati mwingi mtu akisema anataka kutoa rejea ya kitu fulani ni kujaribu kutupilia mbali maswali, kama hauko tayari kutoa suluhisho ya jambo fulani ruhusu mazungumzo yaendelee mbele na rejea hiyo kaa nayo mwenyewe. 2. Nimeshatuma Barua Pepe Mazungumzo ya Uso kwa Uso hayatakuwa na maana kama ukisema umeshatuma barua pepe na kila mmoja akasome. Badala yake ongelea kwa muhtasari suala hilo ili kila mmoja ajue ni kitu gani kinaendelea. 3. Hilo si jambo la msingi sana. Maneno kama hayo hutokea mara nyingi, ukisema jambo si la msingi, kwanini? Hata kama jambo linaloletwa mezani si la wakati huo haimaanishi lisichuKUliwe u

MEZA YETU YA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI TAREHE 13.03.2014

Image
MAGAZETI YA UDAKU LEO MAGAZETI YA MICHEZO NA BURUDANI

Taarifa ya mahakama juu ya ghorofa ambalo liliporomoka jijini Dar siku za nyuma

Image
Kama unalikumbuka Ghorofa lililowahi kuingia kwenye headline kwa kuporomoka likiwa bado linaendelea na ujenzi sasa leo Mkurugenzi wa zamani wa Manispaa ya Ilala Gabriel Fuime na wenzake 11 wamesomewa upya mashtaka 27 ya mauaji katika ajali ya kuporomoka kwa jengo hilo la ghorofa 16 Dar. Mkurugenzi huyo wa Mashitaka Nchini (DPP) amemfutia mashitaka aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Gabriel Fuime (61) na kisha kumuunganisha na wenzake 11 na kuwasomea upya mashtaka 27 ya mauaji yaliyotokea katika mtaa wa Indira Gandh yaliyosababishwa na kuporomoka kwa Ghorofa hilo. Mbali na Fuime washtakiwa wengine ni Diwani wa Kata ya Goba Ibrahim Mohamed maarufu kama Kisoki,Raza Ladha,Goodluck Mbanga,Willbroad Mugyabuso,Mohamed Abdulkarim,Charles Ogare,Zonazea Oushoudada,Vedasto Ruhale,Michael Hema,Albert Mnuo na Joseph Ringo. Washtakiwa hao wamesomewa hati mpya ya mashitaka baada ya kuondolewa hati ya zamani ya mauaji ya bila kukusudiwa na kuunganishwa Fuime na i

Mabaki kama ya ndege yaonekana baharini

Image
Picha zilizonaswa na mtambo wa satellite Serikali ya Uchina imechapisha picha zilizonaswa na mtambo wake wa satelite zikionyesha mabaki ya kitu kipana kikielea katika bahari ya Kusini mwa Uchina.Picha hizo zilipigwa siku ya Jumapili, saa ishirini na nne baada ya ndege ya abiria ya Malaysia kutoweka ikiwa na abiria 239, lakini haijabainika ikiwa vifaa hivyo ni vya ndege hiyo.Huku ikiwa na raia wake 154, ambao walikuwa abiria kwenye ndege hiyo ya Malaysia, serikali ya Uchina imetuma mitambo kumi ya satellite kusaidia katika harakati za kutafuta ndege hiyo.Picha za vifaa hivyo vitatu, ambavyo moja ina upana wa takriban mita 24 kwa 22, zilichukuliwa siku ya Jumapili, siku moja tu baada ya ndege hiyo kupotea, lakini zilichapishwa siku ya Jumatano. Picha zilizonaswa na mtambo wa satellite Ubawa wa ndege hiyo iliyopotea ina upana wa mita sitini na moja. Picha hizo za satellite zimeweka vifaa hivyo takriban maili mia moja kutoka kwa njia iliyotarajiwa kutumiw

LIGI YA MABINGWA ULAYA : FC BARCELONA WAICHAPA MAN CITY NA KUTUPWA NJE

Image
Jubilant: Lionel Messi celebrates with his team-mates after giving the hosts the lead on the night Dink: Messi slips the ball over Joe Hart to give Barcelona a 3-0 aggregate lead Thanks: Messi celebrates in front of the Nou Camp crowd after his opening goal Off you go: Pablo Zabaleta was sent off for a second booking for disputing a penalty appeal with the referee Down and out: City crashed out 4-1 on aggregate, and had two player sent off over both legs Gutted: Edin Dzeko and his team-mates look dejected after conceding the opening goal Winner: Alves blasts home for the winning goal on the night past Joe Hart Rough and tumble: Substitute Dzeko is roughly handled by Pique at the Nou Camp The quadruple is now the Capital One Cup and an uphill climb to wrest first spot off Chelsea.  City enjoyed moments of brightness here, but a 4-1 aggregate defeat by what Jose Mourinho regards as the worst Ba