Posts

Showing posts from January 21, 2016

Bahati Bukuku Aishiwa Nguvu

Image
Mwimba Injili mahiri Bongo, Bahati Bukuku akiwa na huzuni baada ya kufiwa na mama yake. DAR ES SALAAM: Pole! Mwimba Injili mahiri Bongo, Bahati Bukuku hivi karibuni aliishiwa nguvu wakati akimzika mama yake mzazi, Enea Bukuku aliyefariki dunia Januari 12, mwaka huu jijini Mbeya kwa ugonjwa wa shinikizo la damu (presha). Kwa mujibu wa shuhuda wetu, Bahati alikumbwa na hali hiyo mara baada ya kuuaga mwili wa mama yake, tayari kwa safari ya kwenda kuupumzisha kwenye Makaburi ya Mlima James jijini humo. …..Akiweka shada la maua. “Jamani kifo cha mama kinauma sana! Bahati amejikuta akiishiwa nguvu msibani. Nimemhurumia sana huyu dada, lakini naamini Mungu atamtia nguvu maana yeye ndiye aliyetoa na ndiye aliyetwaa, jina lake libarikiwe,” alisema shuhuda huyo. Akaendelea: “Lakini nimeona waimba Injili wenzake, nilimwona Bonny Mwaitege naye kutoka Dar amekuja kumzika mama wa mwimba Injili mwenzake. Bahati anahitaji uangalizi kwa siku mbili hizi, kwani muda mwingi namwona an

RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI AKIONESHA UMAHIRI KATIKA USHONAJI.

Image
 Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akionesha umahiri wake wa kutumia Cherahani na kushona nguo za wafanyakazi wakati alipofanya ziara ya kutembelea na kuvifahamu vitengo mbalimbali vya Ikulu jijini Dar es salaam Januari 20, 2016   Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kushona kwa ustadi wa hali ya juu Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akimalizia moja ya nguo za wafanyakazi wa Ikulu.

BREAKING NEWZZZ.....ZITTO KABWE AANDIKA UJUMBE MZITO KUHUSU KUIBIWA KWA KOMPUTA YA KAMISHNA WA TRA.

Image
 

RAIS DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI AONGOZA WAOMBOLEZAJI KUAGA MWILI WA MAREHEMU LETICIA NYERERE

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Rais mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho  Kikwete nyumbani kwa Baba wa Taifa  Msasani Dar es salaam wakati wa kuaga mwili wa aliyekua Mbunge wa Viti Maalum (Chadema) Marehemu Leticia Nyerere aliyefariki mwishoni mwa wiki Nchini Marekani alikokuwa akitibiwa leo Januari 20, 2016.   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na waombolezaji wakati wa kuaga mwili wa aliyekua Mbunge wa Viti Maalum (Chadema) Marehemu Leticia Nyerere aliyefariki mwishoni mwa wiki Nchini Marekani alikokuwa akitibiwa leo Januari 20, 2016.   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiweka saini katika kitabu cha maombolezo wakati wa kuaga mwili wa aliyekua Mbunge wa Viti Maalum (Chadema) Marehemu Leticia Nyerere aliyefariki mwishoni mwa wiki Nchini Marekani alikokuwa akitibiwa leo Januari 20, 2016.   Rais wa Jamhuri ya Mu

RUVU YAKUBALI KICHAPO CHA MABAO 2 -0 KUTOKA KWA SIMBA

Image
Mshambuliaji wa Simba, Daniel Lyanga akielekea kuifungia timu yake bao la pili dhidi ya JKT Ruvu baada ya kumtoka golikipa wa JKT Ruvu, Hamis Seif katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo. Simba ilishinda 2-0. (Picha na Francis Dande)  Patashka. Raha ya ushindi. Kutoka kushoto, Amis Kiiza, Daniel Lyanga na Kihongera Raphael wakishangilia bao la pili la timu ya Simba lililofungwa na Lyanga.

DK. JOHN POMBE MAGUFULI AMRUDISHA MANYARA MASWI BAADA YA KUMALIZA KAZI MAALUM TRA

Image