Posts

Showing posts from August 9, 2013

SHEHA ALIYEKUTWA NA BANGI ATIMULIWA KAZINI HUKO UNGUJA

Image
SERIKALI katika mkoa wa Kusini Unguja, imemtimua kazi Sheha wa Kitumba, Mtwana Kificho, ambaye wiki iliyopita nyumbani kwake alikutwa na majani makavu yanayosadikiwa kuwa bangi baada ya polisi kufanya ukaguzi.   Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja, Dk Idrissa Muslim Hijja, jana aliwateuwa masheha wawili na kuwaapisha kuongoza shehia hizo, pamoja na sheha mpya wa Kitumba, Makame Chum.   Akizungumza na masheha hao katika eneo la Tunguu katika mkoa wa Kusini Unguja, Dk Hijaa, aliwataka masheha hao kutekeleza majukumu yao ya kuongoza kwa busara katika maeneo yao kwa mujibu wa sheria.   Alisema masheha ni watendaji na wasimamizi wa majukumu ya wananchi, ambapo matatizo yao wanatakiwa kuwasilishwa mbele ya Serikali Kuu kupatiwa ufumbuzi.   “Majukumu ya kazi kwa masheha ni kusimamia matatizo ya wananchi na kuyaelekeza kwa Serikali Kuu kwa ajili ya kupatiwa ufumbuzi na sio kuchochea mifarakano katika jamii,” alisema.   Kwa mfano Mkuu wa Mkoa

POMBE ZAWAFANYA WAKINA DADA WAMWAGE RADHI!

Image
wahenga walisema pombe si maji na ukizivagaa ni lazima zikuhadhiri Ama kweli pombe mwanaharamu, baada ya watu kupiga tungi, wata wakaanza kujiachia na kuchezacheza bila ya muelekeo mwisho wa siku hayoapo juu ndo yaliyotokea!

muonekano wa Irene Uwoya akiwa katika mavazi ya mafundi ujenzi akiandaa show yake

Image
Irene Uwoya ameshaanza mpango mzima wa kutembelea nyumba na kuzifanyia ukarabati akiwa kwenye harakati za ku-shoot show yake. Unaambiwa Irene kwenye show anaonekana kama mkandarasi kabisa akiwa amevaa overall na kofia ya wajenzi.  at Friday, August 09, 2013 Email This BlogThis! Share to Twitter Share to Facebook

DUNIA YACHARUKA SAKATA LA TINDIKALI ................................

Image
UTHIBITISHO NI HAYA MAONI YA WASOMAJI WA MTANDAO WA SKYNEWS JUU YA TUKIO LA RAIA WAWILI WA UINGEREZA WALIOMWAGIWA TINDIKALI MJINI ZANZIBAR JUZI           Hizi ni baadhi ya maoni ya wasomaji wa mtandao wa Skynews.com juu ya tukio la wasichana wawili wenye asili ya uingereza waliomwagiwa tindikali katika kisiwa cha Zanzibar juzi.Wengi wao ni Waingereza wameonyeshwa kukerwa na tukio la kinyama dhidi ya raia hao wa uingereza at Friday, August 09, 2013

MHADHIRI UDSM AUAWA KIKATILI, WAZUNGU WAWILI WAMWAGIWA TINDIKALI ZANZIBAR

Image
Mauaji, mashambulizi ya kudhuru mwili na uporaji vimeendelea kuchafua taswira ya Tanzania baada ya juzi, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), kuuawa kwa kupigwa risasi na watu ambao hawajafahamika, raia wawili wa Uingereza kumwagiwa tindikali na mfanyabiashara kuporwa zaidi ya Sh40 milioni.  Jana, Rais Jakaya Kikwete alikwenda Hospitali ya Aga Khan kuwajulia hali raia hao wawili wa Uingereza waliomwagiwa tindikali huko Zanzibar, Kate Gee (18) na Kirstie Trup (18) akisema tukio hilo limetia aibu kwa mataifa ya nje na kuliamuru Jeshi la Polisi kuhakikisha linawakamata na kuwafungulia mashtaka wote waliohusika. Mauaji Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Camillius Wambura alisema jana kuwa mauaji ya Mhadhiri huyo Msaidizi katika Idara ya Uhandisi na Teknolojia, Patrick Rweyongeza (32) yalitokea juzi saa saba mchana maeneo ya Magomeni Tanesco, Dar es Salaam, wakati marehemu

"MAPAJA YANGU NDO KILA KITU CHENYE MVUTO KWANGU" DIVA WA CLOUD FM

Image
Loveness Diva  sasa  kaamua  kuyapromote  mapaja  yake baada ya  kuchoka  kumpaisha  mpenzi  wake..... Kupitia  account  yake  ya  instagram, jana  Diva  alitupia  picha  ya  paja  lake  na  kuwaacha   mashabiki  wake  wafunguke  kama  paja  lake  ni  zuri  au  baya....

ZIWA NYASA LOTE NI MALAWI, TANZANIA HAINA HATA PUNJE YA ENEO".... MGOMBE URAIS NCHINI MALAWI AFUNGUKA

Image
Mgombea Urais wa Democratic Progressive Party (DPP) nchini Malawi, Peter Mutharika, amesema hakuna sababu za kufanya majadiliano kuhusu Ziwa Malawi ambalo Tanzania wanaliita Ziwa Nyasa.    Mutharika, ambaye ni mwanasheria, aliyasema hayo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika juzi  Mkoa wa Kati. Akikaririwa na gazeti la   Nyasa Times , Mutharika  alisema Tanzania haina cha kuambulia kwa Ziwa Malawi. Kiongozi huyo ambaye hakuwapo katika mkutano wa Rais Joyce Banda na wapinzani kuzungumzia mustakabali wa ziwa, aliwahakikishia Wamalawi kuwa wasiwe na wasiwasi wa mvutano huo. Mutharika ziwa lote ni mali ya Malawi na  akisisitiza kuwa, Tanzania haina hata punje ya eneo. “Hakuhitajiki majadiliano, Ziwa Malawi ni mali ya Malawi, litakuwa la Malawi,” alisema Mutharika ambaye alichukua masomo ya Sheria Tanzania.    “Tanzania inatumia nafasi ya udhaifu wa uongozi wetu, lakini ukweli

RAIS KIKWETE ASALI IDD KINONDONI LEO

Image
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akingia katika msikiti wa Kinondoni Muslim tayari kuhudhuria swala ya Iddi leo asubuhi,jijini Dar es Salaam --Baadhi ya waumini ya dini ya kiisalmu wakiswali swala ya Iddi katika msikiti wa Kinondoni Muslim jijini Dar es Salaam leo jioni(picha na Freddy Maro)