Posts

Showing posts from September 11, 2015

WASIRA ,BULAYA WALALAMIKIA HUJUMA

Image
Bunda. Wagombea ubunge Jimbo la Bunda Mjini, Stephen Wasira (CCM) na Ester Bulaya (Chadema), wameomba vyombo vya ulinzi kusimamia amani kipindi hiki cha kampeni inayoonekana kuvurugwa na baadhi ya wafuasi wa vyama hivyo. Kauli hizo zilitolewa na wagombea hao kwa nyakati tofauti kwenye mikutano yao na waandishi wa habari juzi. Walidai baadhi ya wafuasi hutishiana maisha na wengine kupigana hadi kujeruhiana. Juzi saa tatu asubuhi, Bulaya aliitisha mkutano na waandishi wa habari akilalamikia wafuasi wa chama hicho kupigwa hadi kujeruhiwa, huku mikutano yake ya kampeni ikifanyiwa fujo na watu wanaodaiwa ni wafuasi wa CCM na vyombo vya dola havikuchukua hatua. Wasira aliomba vyombo vya ulinzi na usalama hususan polisi, kutamka wazi kama wamezidiwa na kazi, ili aombe kwa mamlaka za juu kuongeza polisi watakaosaidia kuimarisha amani na utulivu kwenye mikutano yake ya kampeni. Wasira alisema wajibu wa polisi ni kulinda usalama wa raia na mali zao, lakini hawafanyi hivyo. Watu

MBUNGE MWINGINE CCM ANUSURIKA KICHAPO BAADA YA KUVAMIA MKUTANO WA ACT-WAZALENDO, SOMA HAPA

Image
Mbunge wa Nkasi Kaskazini (CCM), aliyemaliza muda wake, Ally Keissy jana aliibuka kwenye mkutano wa kampeni wa chama cha ACT-Wazalendo na kupinga maelezo kwamba mshahara wake wa ubunge ni zaidi ya Sh10 milioni. Keissy aliwasili kwenye mkutano huo uliokuwa wa mgombea urais wa ACT-Wazalendo, Anna Mghwira na mgombea mwenza wake, Hamad Yusuph Mussa uliofanyika Kijiji cha Namanyere, akiwa kwenye gari lake aina ya Toyota Land Cruiser. Mgombea mwenza, Mussa alipopanda jukwaani, alianza kuhutubia kwa kuwaeleza wananchi kwamba mbunge wao, Keissy anayemaliza muda wake ameshindwa kuwaletea maendeleo, hivyo mwaka huu wasimpe kura zao. “Niwaambie kitu, wabunge wenu akiwamo Keissy wanapata mshahara wa zaidi Sh10 milioni ndiyo maana akiwa bungeni kazi yake ni kupiga makofi kwa kushangalia kupitisha kwa bajeti ambayo haina masilahi kwa wananchi wa jimbo lenu,” alisema Mussa na kushangiliwa na umati ambao mmoja alisikika akisema: “Sema baba sema, ujumbe umefika na mwenyewe yupo hapa.”

UNESCO WAKABIDHI KITABU CHA MAFUNZO YA TEHAMA KWA SERIKALI NCHINI

Image
Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Zulmira Rodrigues (kulia) akitoa neno la ukaribisho kwa wadau wa sekta ya elimu wakati wa hafla ya kukabidhi kitabu cha mafunzo ya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu nchini kwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi. Katikati ni mgeni rasmi Kamishina wa Elimu, Profesa Eustella Bhalalusesa aliyemwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Prof. Sifuni Mchome. Kushoto ni Ofisa wa Ubalozi wa China, LIU Yun.(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog ) Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), limekabidhi rasmi kitabu cha mafunzo ya Tehama kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu nchini kwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi. Makabidhiano hayo yamefanyika jana jijini Dar es salaam katika hafla iliyohudhuriwa na wadau walioshiriki katika uandazi wa kitabu hicho, ikiwamo serikali ya China.

TEAM YA WASANII WA MABADILIKO WALETA MAFURIKO MTWARA

Image
Msanii Walter Chilambo akiimba katika Tamasha la Wasanii wa Mabadiliko lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita mjini Mtwara. Lengo la Tamasha hilo ni kuwahimiza wananchi kujitokeza kupiga kura Oktoba 25, 2015. Msanii Mkoloni akiimba katika Tamasha la Wasanii wa Mabadiliko lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita mjini Mtwara. Lengo la Tamasha hilo ni kuwahimiza wananchi kujitokeza kupiga kura Oktoba 25, 2015. Wananchi waliojitokeza katuka Tamasha la Mabadiliko ililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita mjini Mtwara. Lengo la Tamasha hilo ni kuwahimiza wananchi kujitokeza kupiga kura Oktoba 25, 2015. Msanii Sogy Dog akiimba katika Tamasha la Wasanii wa Mabadiliko lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita mjini Mtwara. Lengo la Tamasha hilo ni kuwahimiza wananchi kujitokeza kupiga kura Oktoba 25, 2015. Wasanii wa Bongo Movie wakiwasha moto katika Tamasha la Wasanii wa Mabadiliko lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita mjini Mtwara. Lengo la T

LOWASSA AENDELEA NA ZIARA YAKE YA KAMPENI MKOANI DODOMA

Image
Chopa ya Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, ikitua kwenye Uwanja wa Taifa wa Gairo Mkoani Morogoro, ikiwa ni sehemu wa muendelezo wa ziara zake za Kampeni anazoendelea, kwenye maeneo mbali mbali hapa nchini. Mh. Lowassa leo amefanya Mikutano yake hiyo katika Majimbo ya Gairo,Kibakwe, Mpwapwa na Kibaigwa Mkoani Dodoma. Mh. Lowassa na Mh. Sumaye wakielekea eneo la Mkutano. Meneja wa Kampeni, John Mrema akisisitiza jambo kwa wananchi wa Mji wa Gairo. Wakazi wa Gairo, wakifatilia kwa Makini sera za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa. Akiwasalimia wananchi wa Gairo. Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akimsikiliza Mgombea Ubunge wa Ukawa kupitia CHADEMA wa Jimbo la Gairo, Salum Mpanda, wakati akimuelezea ch