Posts

Showing posts from November 16, 2013

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI TAREHE 16.11.2013

Image
MAGAZETI YA MICHEZO NA BURUDANI MAGAZETI YA UDAKU LEO  

U.S. blocks report telling how UK went to war with Iraq

Image
A draft report challenged the official story of the UK’s entry into the Iraq war, mainly related to exchanges with then-PM Tony Blair and former president George W. Bush.  Four-year inquiry into UK’s role in Iraq war by British government blocked by White House and U.S. State Department officials The United States is behind the delaying a key report’s release showing how the UK went to war with Iraq, London-based daily The Independent reported on Wednesday.White House and State Department officials are behind the blocking of the four-year Chilcot inquiry, which the UK’s Cabinet Office has been criticized for halting.The newspaper saw drafts of the report earlier this year which challenged the official story of the UK’s entry into the Iraq war, mainly related to exchanges with then-PM Tony Blair and former president George W. Bush. A diplomatic source quoted by the independent said that the U.S. is “highly possessive when documents relate to the presence of

RONALDO AING'ARISHA URENO DHIDI YA SWEDEN YA IBRAHIMOVIC KOMBE LA DUNIA

Image
Cristiano Ronaldo akishangilia baada ya kuifungia bao pekee la ushindi Ureno. BAO pekee la Cristiano Ronaldo dakika ya 82 limeipa usindi wa 1-0 Ureno katika mchezo wa kwanza wa mchujo wa kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunai usiku huu dhidi ya Sweden, Uwanja wa  Estadio da Luz. Ureno sasa itahitaji kuulinda ushindi huo katika mchezo wa marudiano Jumanne mjini Stockholm ili kukata tiketi ya Brazil. Kikosi cha Ureno kilikuwa: Patricio, Pereira, Coentrao, Veloso, Pepe, Regufe Alves, Meireles/Josue dk78, Moutinho, Postiga/Almeida dk66, Nani na Ronaldo Sweden: Isaksson, Lustig, Olsson, Elm/Wernbloom dk72, Nilsson, Antonsson, Larsson, Kallstrom/Svensson dk77, Ibrahimovic, Elmander/Gerndt dk88 na Kacaniklic. Vita ya wakali: Cristiano Ronaldo w Ureno (kushoto) na Zlatan Ibrahimovic wa Sweden wakisalimiana kabla ya mechi

MWILI WA MAREHEMU DK.MVUNGI WAPOKELEWA KWA MAJONZI JIJINI DAR ES SALAAM NAKUTOLEWA RATIBA KAMILI YA MAZISHI

Image
 Mwili wa Marehemu Dk. Sengondo Mvungi ukifanyiwa maombi mara baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo.  Wanachama wa NCCR-Mageuzi wakiwa wamelibeba sanduku lililohifandhi mwili wa kiongozi huyo wa NCCR-Mageuzi na Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya.  Waombolezaji waliofika uwanjani hapo kuupokea Mwili wa Dk. Mvungi................  Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba akiwa uwanjani hapo.  Baadhi ya waombolezaji waliofika uwanjani hapo. Mjane wa Marehemu, Bi Anna Mvungi akiwa uwanjani hapo kuupokea mwili wa mumewe Ndugu wakilia kwa uchungu... Na Father Kidevu Blog Mwili wa aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya mabadiliko ya Katiba mpya na  Mkurugenzi wa Katiba, Sheria na Haki za Binadamu wa  NCCR-Mageuzi, Marehemu Dk. Sengondo Mvungi umewasili nchini kutoka Afrika Kusini. Makumi ya wakazi w

Duma wakiona cha mtema kuni nchini Kenya wakimbizwa na kukamatwa

Image
Duma waliokamatwa na kukabidhiwa maafisa wa huduma za wanyamapori Wanakijiji Kaskazini Mashariki mwa Kenya wamewakimbiza Duma wawili ambao wamekuwa wakiwaua Mbuzi wao na kuwakamata.   Wakaazi hao wanaoishi karibu na mji wa Wajir walisubiri hadi majira ya joto nyakati za mchana kuwafukuza Duma hao ambao baada ya kilomita sita walichoka na kusalimu amri. Jamaa aliyeongoza uwindaji huo amesema aliamua kuchukua hatua baada ya Duma hao kuwaua mbuzi wake 15.   Duma hao walikamatwa wakiwa hai na wamekabidhiwa shirika la wanayapori KWS huku wana kijiji hao wakitaka kulipwa fidia ya mbuzi waliouawa.   Wanakiji hao waliambia BBC kuwa wanyama hao walikuwa wakiwashika Mbuzi wao mmoja baad ya mwingine kila siku.   "Nahitaji kulipwa fidia kwa sababu Duma hawa waliwala mifugo wangu wengi,'' alisema Nur Osman Hassan.  Mifugo ndio njia kubwa zaidi ya kujikimu katika jamii ya wasomali wakenya wanaoishi Kaskazini Mashariki mwa nchi ambako ukame ndio hali

MAJIBU YA "NGOMA" YA IRENE UWOYA HAYA HAPA

Image
Sio tu watu maarufu bali binadamu wengi huingiwa na uoga kila wanapofikiria swala la kwenda kupima kama wana maambukizi ya virusi vya ukimwi au la na hata akifanikiwa kupima pia ugumu huja pale mtu anapofikiria kwenda kuchukua majibu. Mama Krish “Irene Uwoya” best actress wa bongomovie awards 2013 ameweka wazi majibu yake ya vipimo vya VVU na kuhamasisha watu wengine wafanye maamuzi ya kwenda kupima afya zao, cheti na maneno ya kuhamasisha watu wengine kupima vyote ndio hivi hapa chini….

Tattoo na muonekano mpya wa Ray, vyawachefua mashabiki wake....wengi wasema amechemka.

Image
Huu  ni  muonekano  mpya wa  Vicent  Kigosi ambao ni moja ya maandalizi ya movie  yake  mpya ... Ni  muonekano  ambao  kwa  kiasi  flani  umewachefua  mashabiki  wake  ambao  dakika  chache  baada  ya  picha  hizo  kuwekwa  walijimwaga  kwa  comment  ambazo hazikumuunga  mkono  kwa  asilimia  zote.  “Je nageukia bongoflava au kuna nini kinakuja?”. Aliadika  Ray  kwenye  moja  ya  picha  zake.