Posts

Showing posts from May 20, 2016

Sakata la Mauaji Msikitini Mwanza: Kundi la Kigaidi la ISIS lahusishwa

Image
YADAIWA ni kisasi baada ya Polisi kuwakamata wanaharakati wa IS saa 24 kabla. "baada ya swala kumalizika, watu hao waliingia na kuwaamuru kulala chini huku wakitoa bendera nyeusi na maandishi ya meupe ya Kiarabu kisha kumtaka Imamu wa msikiti kujitokeza mbele, bendera hiyo ni kama ile inayotumiwa na kundi la kigaidi la IS" "Imamu alipojitokeza huku tukiwa tumelala chini, watu hao walisikika wakisema 'Kwa nini mnaswali wakati wenzetu wamekamatwa na polisi, wengine wanapigana 'jihad'...hali hiyo ilitushtua zaidi baada ya Imamu kuanza kuchinjwa kwa panga," "Ghafla wakatuamuru kulala kifudifudi na kudai wao ni IS wamekuja kufanya kazi yao, kisha wakaanza kutushambulia na kujeruhi. Mwenzangu niliyekuwa naye pembeni alikatwa panga na kuangukia juu yangu, hali hiyo ilinifanya nionekane kama nimekufa," Habari za uhakika ambazo Nipashe imezipata zinasema. Imam huyo na wafuasi wake, waliuwawa na kundi la watu wanane waliokuwa na bu

SAKATA LA ESCROW, IPTL LAIBUKA UPYA BUNGENI

Image
Kambi ya upinzani imeliibua upya bungeni sakata la Escrow, Richmond na umiliki wa kampuni ya IPTL, huku ikihoji sababu za Rais John Magufuli kutoheshimu maazimio ya Bunge ya kumwajibisha Sospeter Muhongo, badala yake kumteua tena kuwa Waziri wa Nishati na Madini. Hoja hizo ziliibuliwa na Waziri Kivuli wa Nishati na Madini, John Mnyika wakati akiwasilisha maoni ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2015/16 na makadirio ya matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka 2016/17. Muhongo alikuwa akiiongoza wizara hiyo wakati kashfa ya uchotwaji wa zaidi ya Sh300 bilioni kutoka kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow iliyofunguliwa kuhifadhi fedha za malipo umeme kusubiri kumalizika kwa mzozo wa kimkataba baina ya kampuni ya IPTL, inayozalisha umeme na Shirika la Umeme (Tanesco). Bunge lilimuona Profesa Muhongo kuwa alishindwa kuwajibika na kusababisha Serikali kupoteza mapato. Profesa Muhongo alilazimika kujiuzulu wadhifa huo saa chache kabla ya Rais wa Serikali ya Awamu ya Nne, Jakaya Kikwet

Msichana mwingine kati ya wale 276 waliotekwa na Boko Haram apatikana

Image
Baada ya miaka miwili tangu kutekwa kwa wasichana zaidi ya 276 wa shule na kupatikana kwa mmoja May 18 2016 msichana mwingine  Serah Luka  amepatikana kaskazini mashariki mwa jimbo la Borno. Mkuu wa jeshi la polisi Nigeria ametibitisha taarifa hizo japo hakutoa maelezo mengine ya ziada.  Taarifa zimeripotiwa siku mbili baada ya kupatikana kwa msichana mwingine wa kundi hilo la Chibok girls Amina Ali . Amina Ali  ambaye alipatikana May 18 2016 alialikwa na Rais wa Nigeria nyumbani kwake akiwa pamoja na mama na mtoto wake aliyejifungua wakati akiwa mateka wa kundi la kigaidi la Boko Haram,  anasema kati ya wanafunzi wenzake, sita walipoteza maisha walipokua mateka.

KESSY AMVAA JOHN MNYIKA

Image
Jina la aliyekuwa mgombea wa urais kwa tiketi ya Chadema akiungwa mkono na vyama vya upinzani vilivyounda Ukawa, jana liliingia tena katika Bunge la Kumi na Moja na kuzua mvutano. Lowassa alitajwa na Mbunge wa Nkasi Kaskazini, Ally Keissy (CCM), wakati akijibu hoja za Mbunge wa Kibamba, John Mnyika aliyekuwa akihoji na kuonesha kushangazwa na uteuzi wa Profesa Sospeter Muhongo kuwa Waziri wa Nishati na Madini wakati alijiuzulu bungeni hapo baada ya kuelemewa na kashfa ya akaunti ya ‘Tegeta Escrow’. Akijibu hoja hizo, Keissy ambaye siku zote ni mbunge mwenye hoja machachari alimvaa Mnyika  na kuhoji mbona wao ( UKAWA) walimchukua  Lowassa na kumfanya  kuwa mgombea wao wa Urais  wakati alijiuzulu uwaziri Mkuu kwa kashfa ya Richmond. “Mnabeza  uteuzi wa Muhongo wakati Lowassa alivyojiuzulu hapa hapa bungeni mlimchukua mkamtembeza nchi nzima. Leo angekua Rais mgesema nini?"  Alihoji Keissy . Mnyika alikuwa alisoma hatuba ya kambi ya upinzani kwa Wizara ya Ni

DIAMOND PLATINUMS ATAJWA KUWANIA TUZO ZA BET . Tuzo hizo zitatolewa mwishoni mwa mwezi Juni nchini Marekani. Mwananmuziki Diamond Platnumz ametajwa kwa mara ya pili kuwania tuzo za BET katika kipengele cha Best International Act: Africa. Wakali wengine wanaowania tuzo hiyo ni pamoja na Wizkid, Yemi, AKA na wengineo

Image
Tuzo hizo zitatolewa mwishoni mwa mwezi Juni nchini Marekani. Mwananmuziki Diamond Platnumz ametajwa kwa mara ya pili kuwania tuzo za BET katika kipengele cha Best International Act: Africa. Wakali wengine wanaowania tuzo hiyo ni pamoja na Wizkid, Yemi, AKA na wengineo

Kigogo wa CCM Ataka Maalim Seif Sharif Hamad Akamatwe

Image
Kigogo wa CCM aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Sukwa Said Sukwa amevishauri vyombo vya dola visiwani Zanzibar kumchukuliwa hatua haraka Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad kwa kauli yake aliyoihusisha na kosa la uhaini. Sukwa aliitaja kauli ya Maalim Seif aliyoitoa alipokuwa akihutubia katika mkutano wa hadhara kisiwani Pemba kuwa Dk. Ali Mohamed Shein hatamaliza kipindi chake cha urais mwaka 2020 na kwamba ni dikteta. Sukwa amesema kuwa kauli hiyo ya Maalim Seif haipaswi kupuuzwa hata kidogo kwakuwa kauli kama hizo ni zaidi ya sumu. “Sivilazimishi vyombo vya dola kufanya ninavyotaka, lakini tunashauri tu visipuuze ushauri wetu kwa sababu ulimi wa mtu unaweza kuwa sumu hatari kuliko matendo yake,” Sukwa aliliambia gazeti la Raia Tanzania. Maalim Seif amekuwa akifanya mikutano kuwataka wananchi kumuunga mkono kuikataa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na Rais Sh

BREAKING NEWS: GARDNER AMJIBU LADY JAY DEE ,AGOMA KUOMBA RADHI HADHARANI

Image
Hatimaye mtangazaji wa Clouds Fm, Gardner G. Habash amemjibu aliyekuwa mkewe, Lady Jay Dee, aliyemtaka aombe radhi ndani ya siku saba kwa kauli aliyoitoa iliyodaiwa kuwa imelenga kumdhalilisha. Katika majibu yake amekana madai hayo. Siku chache zilizopita, Gardner alionekana katika kipande cha Video akisherehesha tukio la kumsaka mrimbwende wa chuo cha Tanzania Institute of Accountancy (TIA) jijini Dar es Salaam, ambapo alisema kuwa “yule binti sina tatizo naye, nimeshamkojoza kwa miaka kama 15 hivi…”, kisha wimbo wa ‘Ndindindi’ wa Jay Dee ukachezwa na DJ. Kama ilivyokuwa kwa Lady Jay Dee aliyetoa siku saba za kuombwa radhi kupitia kwa mwanasheria wake Amani Tenga, Gardner amejibu kupitia mwanasheria wake Stephen Axwesso. Katika barua yake kwa mwanasheria wa Lady Jay Dee, mwanasheria huyo wa Gardner amekiri kuwa ni kweli mteja wake alizungumza maneno hayo alipokuwa katika shughuli iliyotajwa, lakini alidai kuwa hakuna sehemu aliyomtaja mkewe huyo wa zamani. Alisema