Posts

Showing posts from August 3, 2016

Lowassa, Sumaye Hatarini Kushtakiwa

Image
KAMISHNA wa Sekretarieti ya Maadili kwa Viongozi wa Umma, Jaji mstaafu Salome Kaganda, amewataka viongozi wastaafu kuacha kutoa siri za serikali kwani bado wapo kwenye kiapo na kuonya wakikaidi, watachukuliwa hatua. Bila kuwataja kwa majina wala siri walizotoa, Jaji Kaganda alisema: “Tusiweke maslahi binafsi mbele kwa kutoa siri za mikataba kwa kuangalia manufaa binafsi, jambo ambalo limelifikisha taifa pabaya. Viongozi wastaafu wafunge midomo yao kwani bado wako ndani ya kiapo hata kama wamestaafu.” Waziri mstaafu, Frederick Sumaye. Jaji Kaganda alisema wapo wastaafu ambao wameingia kwenye nyanja mbalimbali ikiwamo siasa, ambapo hutumia majukwaa kutoa siri za serikali na kwamba wanapaswa kukumbuka wanaweza kuchukuliwa hatua za kisheria. Jaji Kaganda aliyasema hayo juzi alipokuwa akihojiwa kwenye kipindi cha dakika 45 kinachorushwa na Kituo cha Runinga cha ITV. Kwa siku za karibuni, mbali na watumishi wa umma walioacha kazi zao na kushiriki siasa ikiwa ni pamoja na ku

Mwalimu aliyetuhumiwa kujihusisha kimapenzi na wanafunzi auawa

Image
MWALIMU Daniel Msalika (42) wa shule ya msingi Nyasosi, wilayani Bariadi, mkoa wa Simiyu amefariki dunia katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando alikokuwa amelazwa akitibiwa majeraha. Majeraha hayo yalitokana na kushambuliwa na baadhi ya wananchi kwa madai ya kujihusisha kimapenzi na wanafunzi wa kike wa shule hiyo. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, Onesmo Lyanga aliwaeleza waandishi wa habari jana ofisini kwake kuwa mwalimu huyo alifariki dunia Julai 31 mwaka huu saa nane usiku. Kamanda Lyanga alisema kuwa siku ya tukio Julai 27 mwaka huu saa 6.30 usiku, wananchi hao ambao idadi yao haijafahamika, walivamia nyumba ya mwalimu huyo baada ya kupata taarifa kuwa kuna mwanafunzi ambaye amelala nyumbani kwake, jambo ambalo halikuwa la kweli. “Wananchi hao walipata taarifa ya kuwa nyumbani kwa mwalimu kuna mwanafunzi ambaye amelala humo hivyo walimvamia kwa kuvunja mlango na kuanza kumshambulia kwa kutumia silaha mbalimbali za jadi na kumsababishia majeraha makubwa s

Wastara agombewa kuosha magari

Image
Wastara Juma akiwa bize kuosha gari. Na Dustan Shekidele, RISASI Mchanganyiko MOROGORO: Msanii maarufu wa filamu za Kibongo, Wastara Juma, mwishoni mwa wiki iliyopita aligeuka gumzo wakati wa harambee maalum ya kuchangia madawati kwa njia ya kuosha magari iliyofanyika mjini hapa, ambapo wateja wengi walikuwa wakimgombea awaoshee magari yao. Harambee hiyo iliyofanyika kwenye kumbi za Samaki Sport na Nyumbani park, iliandaliwa na kundi la wanawake wanaojiita Best Friends Forever (BFF) ambao waliosha magari ya wateja kwa lengo la kukusanya fedha za madawati kuunga mkono harakati za Rais Dk. John Pombe Magufuli kuhakikisha hakuna mwanafunzi anayekaa chini. Mwandishi wetu alimshuhudia Wastara akiwa bize kuosha gari la mheshimiwa diwani wa Kata ya Mafiga, Spear Komanya huku wateja wengine nao wakimsubiri amalize kisha aoshe yao, jambo lililomfanya muda wote aonekane kuwa bize. “Leo tumeamua kuja hapa kwa sababu watu wengi wenye magari huja kustarehe hapa kwa

Kingunge azua hofu

Image
  Na Mwandishi Wetu, RISASI Mchanganyiko DAR ES SALAAM: Ukimya wa mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombare Mwiru umezua hofu kubwa baada ya kutoonekana katika matukio muhimu tangu alipojiondoa kutoka Chama Cha Mapinduzi mwishoni mwa mwaka jana. Kingunge alijiondoa ndani ya chama tawala, muda mfupi baada ya kukatwa kwa jina la Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa na kiongozi huyo kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambako alipewa fursa ya kuwania urais wa Tanzania, akichuana na aliyeibuka mshindi, Dk John Pombe Magufuli. “Huyu mzee yuko wapi jamani, maana yupo kimya sana, wenzake wote tunawaona na kuwasikia, wengine wanarudi CCM, wengine wanaonekana katika matukio, lakini yeye haonekani kabisa, anatupa hofu kwa kweli,” alisema msomaji aliyejitambulisha kwa jina la Giggs, akitokea mkoani Mtwara. Msomaji mwingine, Samson Bilal wa Tabora, alisema kimya cha mwanasiasa huyo huenda kikawa na mshindo mkuu, kwani ukimya wake umekuwa siyo

MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAREHE 03.08.2016

Image