Posts

Showing posts from April 17, 2017

Ufisadi Mkubwa Wizara ya Afya Wagundulika..Wakati Watoto Wakikosa Chanjo Mahospitalini..Hivi Ndivyo Mabilioni ya Pesa Yalivyotafunwa na Wajanja Wachache..!!!

Image
Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kwa mwaka wa fedha 2015/16 imebaini ufisadi wa mabilioni ya fedha katika mradi wa chanjo ya Surua Rubella na ameshauri kufanyika uchunguzi wa kijinai na waliohusika warejeshe fedha hizo. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, hayo yalibainika wakati wa ukaguzi maalumu katika halmashauri za wilaya na ofisi za waganga wakuu wa mikoa. Ukaguzi huo umebaini Sh20.9 bilioni zilipokelewa na Wizara ya Fedha kutoka Gavi Alliance na kiwango hicho chote kilipelekwa Wizara ya Afya kugharamia chanjo ya Surua Rubella. Kati ya kiwango hicho, Sh19.09 bilioni zilitolewa kwa ajili ya chanjo; Sh18.3 bilioni zilitumika Tanzania Bara na Sh725 milioni zilipelekwa Zanzibar na Sh1 bilioni zilitumika kama gharama za uendeshaji. Ripoti hiyo imeainisha kuwa hadi Desemba 31, 2014 kulikuwa na bakaa ya Sh838,423,408. Fedha zilizopokelewa halmashauri Ripoti hiyo inaainisha kuwa Sh17.3 bilioni zilitumwa katika mikoa na kuing

Kwa Mara Nyingine Tena Mke wa Rom Amefunguka Haya Makubwa Kuhusu Tukio la Kutekwa kwa Mumewake Roma Mkatoliki..!!!

Image
Mke wa msanii Roma Mkatoliki, Nancy Mshana amefunguka kwa mara ya kwanza toka mume wake alipotekwa na kupatikana na kuwashukuru Watanzania ambao walikuwa pamoja na yeye katika kipindi kigumu. Mrembo huyo ametumia maneno ya kwenye Biblia kutoka katika kitabu cha Yeremia kufikisha ujumbe wake kwa watu ambao wamemfanyia ubaya mume wake na kusema kuwa na wao watakutwa na mabaya hayo. “(Yeremia 30:16-17) Basi, watu wote wakulao wataliwa; na adui zako wote watakwenda kufungwa; kila mmoja wao; na hao waliokuteka nyara watatekwa; na wote waliokuwinda nitawafanya kuwa mawindo. Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema Bwana.Ameen” Alinukuu mke wa Roma Mkatoliki. Mbali na hilo Nancy alitumia nafasi hiyo kuwashukuru wote ambao wamesimama na wao katika kipindi hiki kigumu. “Ahsanteni wote mliosimama na sisi katika kipindi kigumu tulichopitia !! Mungu awabariki sana” aliandika Nancy. Msanii Roma Mkatoliki bado anaendelea na mati

Huyu Hapa Muuza Madawa ya Kulevya Aliyependwa na Wananchi Mpaka Kupewa Jina la Yesu na Mlinzi wa Amani

Image
TAJIRI WA UNGA AKAWA MWEMA MPAKA AKAITWA YESU Christopher Coke a.k.a Dudus, ni tajiri wa dawa za kulevya, akiongoza genge la Shower Posse. Genge hilo na mtandao mzima wa unga, Dudus au President alirithi kutoka kwa baba yake, Lester Coke a.k.a Jim Brown au Ba-Bye aliyeuawa gerezani mwaka 1992. Shower Posse makao makuu yake yapo Tivoli Gardens, Kingston, Jamaica. Dudu alikuwa mtu mwema. Alisaidia fedha familia maskini, alilipia ada wanafunzi ambao wazazi wao hawakuwa na uwezo, zaidi alitengeneza ajira nyingi kwa vijana. Hayo yalisababisha apendwe sana. Dudus aliitwa Rais wa Tivoli Gardens, alilindwa na kila mwananchi. Serikali ya Jamaica pia ilimlinda, maana alikuwa mfadhili wa viongozi. Marekani ilitaka Dudus akamatwe lakini Serikali ya Jamaica haikutekeleza. Dudus alipokamatwa na Marekani mwaka 2010, kwananchi wa Jamaica, hususan wakazi wa Tivoli Gardens, waliingia mitaani na kuandamana, wakitaka Dudus aachiwe huru. Wananchi walikuwa na mabango yaliyoandik

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA AFUNGUKA HAYA KUHUSU KATIBA MPYA

Image
Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi amesema kuwa mchakato wa Katiba mpya uko pale pale. Prof. Kabudi amesema hayo wakati alipokutana na Kamati ya Katiba na Sheria ya Bunge, amesema kuwa hajakutana na viongozi wake kuzungumzia suala la Katiba Mpya, ingawa anajua mambo mengine kuhusu mchakato huo ambao wakati wa maandalizi yake alikuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.  Amesema kuwa mchakato wa Katiba mpya uko pale pale hivyo pindi mchakato huo utakapo kamilika kwenye ofisi yake atauwasilisha kwenye kamati hiyo. Aidha, Prof. Kabudi ameongeza kuwa ana muda mfupi katika wizara hiyo na kwamba, hajapata muda wa kukutana na mabosi wake akiwamo Waziri Mkuu, ili wazungumzie suala la Katiba Mpya. Hata hivyo, amesema kuwa mchakato huo unahitaji umakini mkubwa hivyo atafanya kazi kulingana na utaratibu wa kisheria ili liwe na mwanzo na mwisho mzuri. CHANZO:UDAKU SPECIAL

Nape afunguka kwanini anaitwa Mkorofi

Image
Kupitia ukurasa wake wa Instagram Mbunge huyo wa Jimbo la Mtamba Nape Moses Nnauye amaeandika ujumb unaosomeka...  "Niliyashuhudia maisha haya mikoani (38months), nadhani ndio nikiyakumbuka naonekana mkorofi!!Iko haja kama Taifa kuangalia vipaumbele vyetu!‬" Facebook Twitter Google+ Pinterest Linkedin

Mwakyembe: Maisha yangu yapo hatarini

Image
Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe amesema maisha yake yapo hatarini . Amesema "...pamoja na kuwa hawezi kulinganisha miaka saba iliyopita na sasa lakini bado maisha yangu hayako salama." akizungmza na Gazeti la MwanaHALISI, DkMwakyembe amesema " Siwezi kuwa salama siwezi kuwa naweza kutumia uhuru wangu wa kwenda kokote nikakota au wakati wowote ninaotaka. "kwamba naweza kutumia uhuru wangu huo kama unavyotakiwa. na katiba .... bado nina hofu ya maisha yangu ingwa siyo kama ilivyokuwa miaka ya mitano iliyopita " ameeleza DK Mwakyembe. DK Mwakyembe alikuwa ni mmoja wa watu waliotajwa kwenye orodha ya wanaotishiwa maisha. wengnie wanaotajwa kwenye orodhra hiyo  ni pamoja na Dr Willibrod Slaa. kauli ya Dk Mwakyembe imekuja siku tano baada ya watu wasiojulikana kumteka na  kumtesa mwanamuziki Ibrahim Musa Roma Mkatoliki. Dk Mwakyembe aliwahi kulipoti Februari Mwaka 2011 kuwepo kwa hatari ya kutokomeza miasha yake