Posts

Showing posts from May 15, 2014

UVUMILIVU NI SOMO LA MAISHA, UPO TAYARI KUJIFUNZA?

Image
Kuna mtu mmoja alishawahi kusema hivi, “Mwonekano wako ni halisi unapojionyesha wakati wa mambo magumu, huwezi kuwa zaidi ya hivyo katika utu wako”. Ukiendelea kuwahukumu watu wengine kutokana na tabia zao huwezi ukaona kitu kizuri ndani yao. Badala ya kumwona mfanyakazi mwenzako ni mtata, msumbufu, katili , hana utu, jaribu kumwona mtu huyo kama mwema na anahitaji kueleweka. Tafuta kitu kizuri ndani yake na uweze kwenda naye kwa hicho kizuri. Ingawa mambo kama hayo yamejengeka kwa muda mrefu kutokana na wapi mtu huyo alizaliwa, maisha gani amepitia na mambo gani yameikabili familia yake akiwa mtoto, kama wazazi kupigana, kutoonyeshwa upendo kwa wazazi wake mwenyewe hivyo kuathirika na vitu vingi. Unapojaribu kuchukuliana na udhaifu wa mtu mwingine na jinsi alivyo unahitaji uvumilivu. Fikiria kwamba kuna mfanyakazi unataka abadiLike kutokana na tabia zake, je yuko hapo kukufundisha nini? je wanakupa mwangaza gani na wewe kujiona kwenye kioo? Mara nyingine ni

MAISHA MAZURI NI NINI? NINI TAFSIRI YA MAISHA BORA?

Image
Tunapoutizama ulimwengu, kila mtu anataka maisha mazuri na wakati mwingine unakaa kujiuliza maisha hayo mazuri ni yapi? Katika Tanzania hii tumechanganya maisha mazuri na kuwa na fedha nyingi au utajiri. Na imetupelekea vijana wengi tukaanza kufanya vitu vya ajabu ili tuwe na maisha mazuri bila kujua hayo maisha mazuri ni yapi? Inategea na uelewa wako wa mambo na sehemu ambayo ulilelewa. Maisha mazuri ni pale ambapo unaridhika na kile ulichonacho,kupata mahitaji ya msingi ya kibinadamu kulingana na eneo ulilopo. Mfumo wa maisha unabadilika kila siku, na tumekuwa na tafsiri tofauti tofauti kuhusu maisha mazuri bali ukweli wa mambo ni kwamba ukishindwa kuridhika na kufuruahia ulichonacho sasa itakuwa ngumu kujua kama unamaisha mazuri. tatizo litakuja pale unapotaka kujilinganisha na watu wengine au marafiki zako na unajikuta unaanza kuishi kulingana na watu wengine au marafiki zako wanavyotaka au kuelezea maisha mazuri. Kuna watu walifikiri watu wenye ma

MPENZI WA CHRISTAN RONALDO AAMBULIA MATUSI MAZITO NA KUSHAMBULIWA NA MASHABIKI BAADA YA KUPOST PICHA AKIWA UTUPU NA BANGO LILILOANDIKWA "BRING BACK OUR GIRLS

Image
  Tangu wasichana 276 wa Nigeria walipotekwa nyara na kundi la Boko Haram, watu mbalimbali maarufu duniani wamepost picha kwenye mitandao ya kijamii wakiwa na mabango yaliyoandikwa ‘Bring back Our Girls’, ikimaanisha wanajiunga na kampeni ya raia wa Nigeria.   Mwana mitindo Irina Shayk ambaye ni mpenzi wa mchezaji wa mpira wa miguu Christian Ronaldo yeye amepost picha kwenye twitter na Instagram akiwa amepoz mtupu huku akiwa ameshikilia bango linaloonesha amejiunga na kampeni hiyo, na bango hilo ndilo lililofunika kifua chake. Hata hivyo kitendo chake hakikuungwa mkono na baadhi ya followers wake ambao walionesha moja kwa moja hisia kwa kumshambulia kuwa ameenda kinyume na maadili. “Pretty tasteless and disrespectful. No class. This is exactly the justification terrorists are probably using to prevent women from receiving 'western education.”  Aliandika mtu mmoja. Mwingine aliona kama amefanya dharau kwa kuwa tatizo hilo sio la nchi kubwa

BAADA YA WAFANYA KAZI WA SAMSUNG KUPATA KANSA, HATIMAYE KULIPWA NA KAMPUNI

Image
Kampuni kubwa duniani ya vifaa vye elektroniki, Samsung inasema kuwa itawalipa fidia wafanyakazi wake waliougua Saratani kutokana na kufanya kazi katika viwanda vyake. Kampuni hiyo iliomba radhi kwa kesi ya muda mrefu kati yake na wafanyakazi hao waliokuwa wanadai fidia na badala yake kukubali kujiondoa katika kesi hiyo huku ikikubali kuwalipa fidia wagonjwa hao. Hatua ya Samsung kukubali kuwalipa wafanyakazi hao inaleta matumaini katika kukamilika kwa mvutano huo ambao ulionekana kukwama kwa muda mrefu Lakini afisa mkuu mtendaji wa kampuni hiyo, Kwon Oh-hyun nusura kukiri kuwa kulikuwa sababu ya wafanyakazi hao kupatwa na Saratni ilichangiwa na wao kufanya kazi katika kiwanda cha Samsung. Wengi walipata Saratani ya damu au Leukaemia. Bwana Kwon alisema wafanyakazi kadhaa katika viwanda vyetu walipatwa na Saratani ya damu na kuugua magonjwa mengine yasiyokuwa na tiba ambayo yalisababisha baadhi yao kufariki.''   tulipaswa kumaliza

MTOTO WA MWAKA MMOJA AANGUKA KUTOKA GHOROFA YA 11 NA KUNUSURIKA KIFO

Image
Mtoto mwenye umri wa mwaka mmoja amenusurika kifo baada ya kuanguka kutoka orofa ya 11 ya jengo moja mjini Minnesota Marekani. Vyombo vya habari katika jimbo hilo vimeripoti kuwa Musa Dayib, amevunjika mkono mara mbili na kwa sasa anapumua kwa usaidizi wa mashine japo madaktari wanamtarajia kuishi. Musa aliteleza katikati ya mianya inayozingira sebule yao katika orofa ya 11 ya mjengo huo wenye nyumba na makazi ya watu. Muuguzi mkuu katika zahanati aliyolazwa amesema kuwa Musa anatarajiwa kuishi baada ya kuanguka katika eneo lisilo kavu sana. Jamaa na marafiki wa familia hiyo ya kisomali wamepigwa na butwaa kutokana na tukio hilo. Tukio hilo lilizua mjadala kama ni muujiza au la kuwa amenusurika kifo lakini watafiti wameelezea kuwa mtoto ananafasi nzuri zaidi ya kuishi hata baada ya kuanguka ama kupatwa na janga lolote lile kwani mwili wao bado ni mwororo na mifupa ya mtoto huwa bado ni laini kinyume na mtu mzima ambaye tayari mifupa yake ni kavu n

ANGALIA PICHA ZA VURUGU ZILIZOTOKEA KWENYE MKUTANO WA UKAWA MOROGORO

Image
Kijana  mmoja amepigwakutoka kwa wafuasi wa Ukawa waliokuwa na mkutano mkoani Morogoro jioni hii baada ya kudaiwa kuwa miongoni mwa waliomteka Mbunge Rose Kamli wakati wa uchaguzi mdogo jimboni Kalenga, mkoani Iringa. Njemba huyo akipokea kichapo kutoka kwa wafuasi wa Ukawa mkoani Morogoro na baadaye kuokolewa na polisi. Mwenyekiti wa Bavicha, John Heche akithibitisha kumtambua kijana huyo anayedaiwa kushiriki kumteka mbunge wao kwenye uchaguzi mdogo uliofanyika Jimbo la Kalenga, lringa. Mmoja wa viongozi wa Chadema mkoa wa Morogoro, lnnocent Zawadi ambaye alikuwepo jimboni Kalenga naye akithibitihsa pia kumtambua kijana huyo. Njemba huyo ambaye hakufahamika jina lake mara moja, aliangushiwa kipigo baada ya kuibuka na kuanza kumpiga picha Mwenyekiti wa Bavicha Taifa, John Heche. Baada ya kipigo cha nguvu, njemba huyo alinusuriwa na polisi waliomchukua kumtoa mikononi mwa wafuasi hao. Mwenyekiti huyo wa Bavicha akithibitisha kumtambua kijana huy