Posts

Showing posts from July 28, 2013

HAUSIBOI ALIYEMLAWITI BINTI WA MIAKA MINNE AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA JELA HUKO MPANDA

Image
Mahakama  ya Hakimu Mkazi ya Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi imemhukumu kijana, Baraka  Juma (22) mkazi wa kijiji cha Nkungwi  wilayani humo, kifungo cha maisha jela  baada ya kupatikana  na hatia  ya  kosa la kumlawiti mtoto wa kike mwenye umri  wa  miaka minne  baada  ya kumhadaa na  kumlewesha bia. Akisoma  hukumu  hiyo  juzi, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Chiganga Tengwa  alisema ameridhishwa  na  ushahidi  pasipo kutia shaka uliotolewa mahakamani hapo na upande zote  mbili za mashitaka na utetezi.   “Nimelazimika kutoa adhabu  kali  kwa mshtakiwa  baada ya  mahakama  hii kumtia  hatiani  ili  iwe  fundisho  si kwake  tu, lakini  pia  kwa wengine  wenye tabia  kama  yako .... kitendo  ulichomtendea mtoto  huyo  ni  cha kinyama hustahili  kuonewa  huruma, “ alisema Tengwa. Awali Mwendesha Mashitaka, Mkaguzi wa Polisi, Lazaro Masembo alidai mahakamani hapo kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo Aprili 2 mwaka huu nyumbani kwa wazazi  wa mtoto h

PATA KUWASILIANA NA RAFIKI ZAKO UKIWA NA KIFURUSHI CHA TIGO KABAANG!

Image
The blogger Sir. Phars akiwa na rafiki zake wakifurahia Tigo KABAANG' toka kushoto ni Prof akiwa Steve  fuahia huduma mbalimbali za kifurushi cha KABAANG,  Steve mzee wa chuga na  Phars the blogger wakifurahia kwa pamoja huduma za kifurushi cha tigo KABAANG; the blogger Sir. Phars akiwa na rafiki zake wakifurahia Tigo KABAANG' toka kushoto ni Prof akiwa Steve

ANGALIA PICHA ZA MSANII DIAMOND ENZI ZAKE ZA UTOTO

Image
Diamond Platinumz ametoa picha nyingine ambayo inawaonyesha yeye na ndugu yake Romie Jones wakiwa wadogo,  kuna picha kadhaa ameshawahi kuzitoa na zilionekana hapahapa millardayo.com. ambapo leo icheki hii picha tena kwenye enzi zao za utotoni wakiwa na baiskeli ya kitoto ambayo ni moja ya vitu vikubwa sana kwa mtoto kuwa nayo kwa kipindi hicho, kwa wale mliokuwa nazo kama hizi BMX najua tunaelewana… ilikua nomaa   Diamond ni huyu wa katikati, Rommy Jones ni huyu wa mbele Hii ni picha ambayo pia waliwahi kuiweka waziiii,source bongoclantz

RAIS KIKWETE AKIWA WILAYANI KARAGWE

Image
 Umati uliojitokeza katika sherehe za uzinduzi wa wilaya mpya ya Kyerwa  Umati uliojitokeza katika sherehe za uzinduzi wa wilaya mpya ya Kyerwa.  Umati uliojitokeza katika sherehe za uzinduzi wa wilaya mpya ya Kyerwa  Umati uliojitokeza katika sherehe za uzinduzi wa wilaya mpya ya Kyerwa  Umati uliojitokeza katika sherehe za uzinduzi wa wilaya mpya ya Kyerwa  Wananchi wakimshangilia Rais Kikwete baada ya kuzindua kivuko cha MV Ruvuvu Jumamosi Julai 27, 2013 Wananchi wakimshangilia Rais Kikwete baada ya kuzindua kivuko cha MV Ruvuvu Jumamosi Julai 27, 2013.Picha Na Ikulu

MBUNGE NASSARI ASOTA POLISI KWA MADAI YA KUMPIGA KADA WA CCM

Image
Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari jana alishikiliwa na jeshi la polisi mkoani Arusha kwa saa tatu na nusu kwa tuhuma za kumshambulia kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Hussein Warsama siku ya uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Makuyuni, wilayani Monduli. Nassari aliyefika Kituo Kikuu cha Polisi Arusha saa 2:30 asubuhi jana ili kuitikia wito wa kutakiwa kuripoti kituoni hapo, alinusurika kuswekwa mahabusu baada ya kujidhamini mwenyewe majira ya saa saa 6:02 mchana na hivyo kuachiwa kwa dhamana. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi ya Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai mkoani Arusha (RCO), Nassari anadaiwa kumshambulia Warsama Juni 16, mwaka huu, eneo Makuyuni alikokuwa wakala mkuu wa mgombea udiwani kupitia Chadema, Japhet Sironga. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas hakupatikana jana kuzungumzia suala hilo, baada ya simu zake zote mbili za kiganjani kuita bila kupokewa wakati RCO, Duwan Nyanda alisema Nassari aliripoti kwake.  Hata

"SASA NIMEOKOKA.....UJINGA SITAKI TENA"...LULU MICHAEL

Image
MUIGIZAJI machachari wa filamu nchini, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amesema baada ya kupata misukosuko ya kimaisha, sasa maisha yake ameyaelekeza katika sala kumuomba Mungu amsamehe makosa yake.  Lulu alisema hayo juzi, katika kipindi cha Friday Night Live (FNL), kinachorushwa na kituo cha Televisheni cha EATV cha Jijini Dar es Salaam. “Sasa hivi nasali sana, namuamini Mungu katika maisha yangu na mbali ya kwenda kanisani, pia nasali mwenyewe katika sala zangu. “Ningependa maisha ya sasa ninayoishi ningeishi siku za nyuma, lakini yote ya Mungu labda maisha yale nisingeyaishi siku za nyuma, ningekuja kuyaishi baadaye,” alisema Lulu. Katika hatua nyingine, alisema anavutiwa na kazi ya msanii wa bongo fleva, Bernard Paul ’Ben Pol’ ambaye tungo za nyimbo zake zinamkosha kuzisikiliza.

BONDIA MTANZANIA OMARI KIMWERI 'LION BOY' AMTWANGA MTHAILAND KWA KO YA RAUNDI YA KWANZA

Image
Omari Kimweri BONDIA Mtanzania Omari Kimweri  'Lion Boy 'anaefanya shughuli zake nchini   Australia amendelea kutamba katika nchi hiyo baada ya jana kumtwanga kwa  KO ya raundi ya kwanza bondia  Ekkalak Saenchan  wa Thailand   ikiwa ni mchezo wake wa 16 tangia angie katika ngumi za kulipwa akiwa nchini humo  Bondia huyo ambaye anaitangaza vema nchi ya Tanzania Kimataifa ameaidi kuwa ataenderea kutoa vipigo kwa mabondia  mbalimbali  pindi wakutanapo ulingoni  Bondia huyo aliezaliwa Tanzania katika jiji la Dar es salaam mwaka1982 amekuwa gumzo nchini humo kwa kuonesha mchezo mzuri unaowavutia raia wengi wa Australia na kuweza kuwa bondia namba moja katika nchi hiyo uku katika Dunia akishikilia nafasi ya 52 katika mabondia 450 duniani wenye uzito wa light flyweight Anasema lengo lake kubwa ni kuukamata ubingwa unaotambulika kimataifa Duniani wa WBA World light flyweight title unaoshikiliwa na bingwa namba moja Dunia