Posts

Showing posts from July 15, 2013

HALI YA MZEE MANDELA YAWAACHA MIDOMO WAZI MARAFIKI ZAKE

Image
Mzee Nelson Mandela. Mke wa Nelson Mandela amesema hana wasiwasi na afya ya mumewe kama alivyokuwa wiki moja iliyopita. “Anaendelea kupokea matibabu vizuri,” amesema Graca Machel. Hata hivyo kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 94 anaelezwa kuwa katika hali mbaya, ikiwa ni wiki ya tano sasa hospitalini.  Juzi Rais Jacob Zuma alisema mpambanaji huyo dhidi ya ubaguzi wa rangi wa watawala wachache weupe wa Afrika Kusini “ameendelea kuwa mpiganaji imara hivi sasa kama ilivyokuwa miaka 50 iliyopita.” Alilazwa tangu Juni 8 kutokana na matatizo ya mapafu. Wiki jana, Zuma alikanusha madai kuwa Mandela hivi sasa hajitambui. Watu wengi ambao wamemwona tangu hapo wamekuwa wakisema anajitambua na ana hisia.   BBC imeripoti kuwa Graca amekuwa pembeni mwa kitanda cha Mandela muda wote hospitalini hapo-Medi-Clinic, Pretoria-na amekuwa akijitenga na mgogoro wa kisheria ndani ya familia ya kiongozi huyo ambao umewekwa hadharani katika wiki chache zilizopita.

ANGALIA PICHA ZA NDEGE YA MH.RAIS JAKAYA KIKWETE WA TANZANIA

Image
Hii ndio Ndege ya Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inatambulika kama 5H - ONE Posted by Phars Nyanda at 09:58 AM No comments: Email This BlogThis! Share to Twitter Share to Facebook Read more: http://phars.blogspot.com/#ixzz2Z5vn0MkQ

JWTZ KUONGEZA NGUVU ZAIDI DARFUR BAADA YA VIFO VYA ASKARI WAKE SABA...

Image
  Mkurugenzi wa Habari na uhusiano wa Jeshi la wananchi Tanzania (JWTZ), Kanali Kapambala Mgawe alipokuwa akizungumzia kuuawa kwa askari 7 wa Tanzania na wengine 14 kujeruhiwa na waasi Darfur Sudan juzi. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), linatarajia kuongeza nguvu ya kujilinda, wakati wa kulinda amani katika Jimbo la Darfur nchini Sudan, ili kujikinga na mashambulizi kama la juzi, ambalo lilisababisha askari wake saba kupoteza maisha. Msemaji wa JWTZ Kanali Kapambala Mgawe, alisema hayo jijini Dar es Salaam jana, wakati akizungumzia shambulio hilo, lililosababisha pia majeruhi wengine 14. Kauli hiyo imetolewa wakati Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Jakaya Kikwete akiungana na Watanzania wote na hasa maofisa na wapiganaji wa JWTZ na familia za wafiwa, kuomboleza vifo vya vijana hao hodari wa Tanzania. Kanali Mgawe alisema mawasiliano yanafanyika kati JWTZ na Umoja wa Mataifa (UN), kuhusu uwezekano wa ku

MIKAKATI YA KUMKAMATA FREEMAN MBOWE YAANZA...POLISI WAMVAMIA USIKU WA MANANE...

Image
KUNDI la polisi wenye silaha za moto juzi usiku walivamia nyumbani kwa Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, kwa nia ya kumkamata. Askari hao wanaokisiwa kufikia saba, wakiwa na silaha nzito katika gari la wazi waliwasili nyumbani kwa Mbowe majira ya saa saba na nusu usiku na kuwaamuru askari wanaolinda nyumbani kwake kumtoa Mbowe nje ili waonane naye. Walinzi wa Mbowe walihoji uhalali wa ukamataji huo na kuwataka polisi wawaoneshe hati ya kumkamata, lakini hawakuweza kuionesha, hali iliyozusha wasiwasi kwa walinzi wa kiongozi huyo. Hata hivyo walinzi hao waliwaambia polisi hao kuwa Mbowe ambaye pia ni kiongozi mkuu wa kambi ya upinzani bungeni alikuwa safarini, jibu ambalo lilipokewa kwa shingo upande na askari hao. Polisi hao baada ya kuona wameshindwa kukamilisha kazi hiyo, waliwaachia walinzi hao namba ya simu 0754-085600 ya Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Ernest Kimola, wakiwaagiza kuhakikis

ASILIMIA 7 YA WATU WAZIMA TANZANIA WANA KISUKARI...

Image
Asilimia saba ya watu wazima nchini wanaumwa kisukari huku theluthi moja kati yao, haina uelewa juu ya ugonjwa huo, jambo linalosababisha wafike hospitalini katika hali mbaya. Taarifa hiyo ilitolewa jana na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi.  Aidha, alizungumzia ugonjwa wa shinikizo la damu na kusema theluthi moja ya watu wazima wameathirika na asilimia 10 ndio wenye uelewa wa ugonjwa huo. Dk Mwinyi alisema hayo jana wakati akizindua  gari la  Chama cha Kisukari nchini (TDA) la kutoa huduma ya kliniki kwa wenye kisukari, shinikizo la damu pamoja na magonjwa mengine.  Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa TDA, Dk Kaushik Ramaiya, wapo watoto 900 wenye ugonjwa huo wa umri kati ya miaka minne na  21 na kwamba kwa walio na umri chini ya miaka 15 wako wagonjwa 475. Waziri alisema idadi kubwa ya watanzania wamekuwa hawana utaratibu wa kupima afya zao. Alisema hufika wakati wakiwa katika hali mbaya.  “Ninaw

WAKATI NANDO AKIHANGAIKA NA GONJWA LA ZINAA ALOPEWA, FEZA NAYE AMETANGAZA NIA YAKE YA KUZALISHWA NDANI YA JUMBA LA BIG BROTHER

Image
Huenda Jay (mtoto wa kiume wa Feza Kessy) anaweza kupata wadogo zake wa kucheza nao soon. Hiyo ni kutokana na mama yake anayeiwakilisha Tanzania mwaka huu kwenye shindano la Big Brother Africa ‘The Chase’ kumwambia mchumba wake raia wa Botswana, Oneal kuwa angependa azae naye watoto. Wapenzi hao waliopo Ruby House walikuwa wakiongea mipango kuhusu uhusiano wao kwenye chumba cha Rendezvous mjengoni humo.   “Please put a little thought into your answers,” anasikika Oneal akimwambia Feza.   “Natamani tungekuwa na mazungumzo haya bila kamera zozote zinazotuzunguka,” Feza alimjibu Oneal. Lakini baadaye alimjibu, “Nataka furaha na wewe, future, nataka mahaba, nataka watoto, nataka maisha na wewe.”  Hata hivyo Feza amekisema kitu kinachomkwaza toka kwa Mbotswana huyo anayefanya kazi ya UDJ nchini mwao kuwa wanapokorofishana yeye huondoka bila kuyamaliza japo amesema atajaribu kumwelewa.   “I know I am a complex man, I don’t even understand myself at time

SHEIKH MKUU WA WILAYA YA ARUMERU AMWAGIWA TINDIKALI NA KUUMIZWA VIBAYA

Image
Shekhe Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Said Juma Makamba amejeruhiwa vibaya kwa kumwagiwa maji yanayohisiwa kuwa tindikali na watu wasiojulikana juzi usiku akiwa nyumbani kwake jijini Arusha. Shekhe Makamba, ambaye amelazwa katika Wodi ya Majeruhi kwenye Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru, amejeruhiwa vibaya maeneo ya usoni, kifuani na mgongoni huku akiendelea na matibabu. Akizungumza kwa tabu, shekhe huyo alisema tukio hilo lilitokea saa 5 usiku wa kuamkia jana nyumbani kwake kwa Mromboo Arusha, wakati akijiandaa kulala baada ya kutoka kuswali Swala ya Tarawei. Shekhe Makamba ambaye pia ni Imamu wa Msikiti wa Sekei mjini Arusha, alisema baada ya swala hiyo alirejea nyumbani kwake akisindikizwa na vijana wawili ambao walikuwa wakiswali pamoja na kuingia ndani ya nyumba yake ili kulala. Alisema hata hivyo, kabla ya kulala alikwenda kujisaidia katika choo cha nje na kwamba wakati akirudi ili aingie ndani akipitia nyuma ya nyumba ghafla alimuona mtu akiwa

BENKI YA CRDB YAFUTURISHA WATEJA WAKE MJINI ZANZIBAR

Image
Mkurugenzi wa Masoko , Utafiti na Huduma kwa Wateja  wa  CRDB  ya Benki,  Tully Esther  Mwambapa  akizungumza katika hafla ya kufuturisha iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake.   Waziri  asiyekuwa na Wizara Maalum  Zanzibar  Machano  Othman Said  akizungumza wakati wa hafla ya kufuturisha wateja wa benki ya CRDB iliyofanyika mjini Zanzibar.  Wadau mbalimbali wakipata futari.  Wafanyakazi wa benki ya CRDB wakijumuika pamoja. Baadhi ya wateja wa benki ya CRDB katika hafla ya kufuturisha. Baadhi ya wateja wa benki ya CRDB wakiwa katika hafla hiyo. Waziri  asiyekuwa na Wizara Maalum  Zanzibar  Machano  Othman Said akizungumza katika hafla hiyo. Meneja wa benki ya CRDB tawi la zanzibar, Nassor Uzigo akipata Chai.  Wafanyakazi wa benki ya CRDB wakishiriki katika hafla ya kufuturisha iliyofanyika mjini Zanzibar.  Wafanyakazi wa benki ya CRDB pamoja na wateja wakipata futari.  Baadhi ya wateja wa

RAIS KIKWETE ATOA TAMKO RASMI KUHUSU MAUAJI YA ASKARI SABA WA TANZANIA WAKILINDA AMANI DARFUR SUDAN.

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ameshtushwa na kuhuzunishwa sana na tukio la kushambuliwa na kuuawa kwa vijana saba hodari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania waliokuwa wanalinda amani katika eneo la Darfur, Sudan. Kwa hakika, Rais amesikitishwa sana na kitendo hicho ambako wanajeshi wengine 14 wa Tanzania wamejeruhiwa na waasi wa Sudan na ametuma salamu za rambirambi za moyoni mwake kwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania na kwa familia za wafiwa wote. Aidha, Rais Kikwete anaungana na Watanzania wote na hasa maofisa na wapiganaji wa JWTZ na familia za wafiwa kuomboleza vifo vya vijana hao hodari wa Tanzania. Rais pia anaungana na Watanzania wote kuwaombea wale walioumia katika tukio hilo waweze kupona haraka na kuendelea na majukumu yao ya ulinzi wa amani chini ya Umoja wa Mataifa. Katika salamu zake za rambirambi kwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinz

MBATIA AIPONDA RED BRIGADE YA CHADEMA

Image
MWENYEKITI wa Chama cha NCCR- Mageuzi James Mbatia, amekikosoa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kwa kitendo cha kutangaza kujihami kwa kuboresha kikosi chao cha ulinzi na usalama cha Red Brigade, kwamba kufanya hivyo ni kushindana na serikali. Wakati Mbatia akisema hayo siku chache zilizopita Rais Jakaya Kikwete alitoa kauli yenye mwelekeo wa  kukiponda chama hicho juu ya mpango wake huo akisema kuwa mpenda amani haundi kikosi cha mgambo. Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, katika kikao cha Halmashauri Kuu (NEC) ya chama hicho, Mbatia alisema ushindani wa kisiasa unatokana na hoja za msingi na si kushindana kwa vitendo. “Kitendo cha Chadema kuunda kikosi chao ni sawa na kushindana na serikali kwani jeshi linatakiwa kudhibitiwa na serikali na si kila chama wala kabila, kwa sababu kufanya hivyo ni kupoteza amani ya nchi,”alisema Mbatia. Alisema kuwa chama cha NCCR- Mageuzi, kitaendele

MATOKEO YA UCHAGUZI WA UDIWANI KATIKA KATA NNE JIJINI ARUSHA

Image
THEMI CDM -678 CCM-326 CUF-313 KIMANDULU CDM-2665 CCM-1169 KALOLENI CDM-1019 CCM-389 CUF-169 ELERAI CDM-1715 CCM-1239 CUF-213

ANGALIA PICHA YA HALI ILIVYOKUA JANA JIJINI ARUSHA WAKATI WA UCHAGUZI MDOGO WA MADIWANI KATIKA KATA 4

Image
 Polisi wakimsihi Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari  aondoke nje ya kituo cha kupigia kura cha Ofisi ya kata ya Kimandolu,pamoja na makada wa CCM hawako pichani ambapo walitakiwa kukaa mita 200 badala ya mita 100.  Polisi wakimsihi Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari  aondoke nje ya kituo cha kupigia kura cha Ofisi ya kata ya Kimandolu,pamoja na makada wa CCM hawako pichani ambapo walitakiwa kukaa mita 200 badala ya mita 100.  Makarani wa uchaguzi wakiingiza masanduku ya kura katika ofisi ya kata ya Kimandolu kutoka  kituo cha kupigia kura cha shule ya msingi kimandolu.  Makarani wa uchaguzi wakiingiza masanduku ya kura katika ofisi ya kata ya Kimandolu kutoka  kituo cha kupigia kura cha shule ya msingi kimandolu.   Polisi wakiimarisha ulinzi katika lango kuu la kuingilia  kituo cha kupigia kura cha Ofisi ya kata ya Kimandolu katika uchaguzi ulifanyika leo mjini Arusha.   Mkazi wa kata ya kima