Posts

Showing posts from October 12, 2013

HOUSIGELI (Mfanyakazi wa ndani ) amnyonga mtoto na kumtupa kwenye dimbwi la maji machafu

Image
Hausigeli aliyejulikana kwa jina moja la Ester (14) yupo matatani kwa madai ya kumuua mtoto Arafat Allan (3) kwa kumnyonga shingo na kumpiga na kitu kizito kichwani kisha kuutumbukiza mwili wake kwenye dimbwi la maji machafu. Tukio hilo lilijiri Jumapili iliyopita Mailimoja, Kibaha mkoani Pwani ambako marehemu alikuwa akiishi na wazazi wake. Akizungumza kwa uchungu, mama mzazi wa mtoto huyo, Zakia Peter ambaye amelazwa katika Zahanati ya Kellen kutokana na mshtuko wa kifo cha mwanaye, alisema siku ya tukio, hausigeli huyo aliyekuwa na siku mbili tangu aanze kazi aling’ang’ania kutumwa sokoni saa mbili asubuhi ambapo alimkubalia na kumuagiza mboga. AONDOKA NA MTOTO Bila mwanamke huyo kujua, msichana huyo alimpitia Arafat kwa jirani alikokuwa akicheza na wenzake na kuondoka naye kwa madai anamsindikiza. “Nilipoona muda unasonga mbele bila hausigeli kurudi na mtoto nilianza kuwatafuta,” alisema mama wa marehemu. Akasema aliwatafuta kwa muda mrefu bila mafanikio mwisho

ADAM MCHOMVU "(mtangazaji)awakwaza watu kwa kuweka picha yake mtandaoni akitiririsha KAMASI"

Image
Kupitia Account yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram Mtangazaji wa Clouds Fm Adam amepost picha hii .Ni picha ambayo imezua gumzo sana miongoni mwa mashabiki wake... Wapo wanaohoji UTIMAMU wa akili yake kwa kuweka picha kama hiyo huku wengine wakidai ni bangi zinamsumbua..... Yafuatayo ni baadhi ya maoni ya mashabiki wake:

KIUNO changu kimeniongezea idadi ya wanaume wanaonitongoza....Wapo wanaotaka kuninunulia gari huku wengine wakiahidi nyumb

Image
Staa wa Majanga, Snura Antony Mushi ‘Snura’ amesema kuwa mauno anayoyakata katika shoo zake yamemfanya apate maombi mengi toka wanaume hasa waume za watu.. Akiongea na mpekuzi wetu, Snura alisema kukata mauno kwenye shoo ndiyo silaha yake ya kuwateka mashabiki lakini anashangaa kuona wanaume za watu ndiyo wanaongoza kwa kumtongoza huku wakiahidi kumnunulia magari na wengine nyumba. “Sipendi kabisa kusikia masuala ya wanaume za watu, Wapo wanaoniahidi gari na wengine nyumba.Labda wangekuwa sio waume za watu ningeweza kufikiria . ,” alisema Snura.

TATOO ya LULU JUU YA MATTITI YAKE YAWA GUMZO

Image
JUZI kabla hajalala mwigizaji Lulu aliwaonyesha mashabiki zake picha ya tatoo yake mpya ambayo imechorwa juu ya Matiti yake kuelekea begani ikiwa ni picha aliyoipost na ikaambatana na maneno yafuatayo:-   "ONLY GOD CAN JUDGE ME…." “ Kumekuwa na kawaida ya watu kuongea na kuhukumu wenzao bila ya kujua wanachokiongelea pengine!! kwa upeo wangu mdogo nafahamu sisi wote ni binadamu na tunamtegemea mtu mmoja MWENYEZI MUNGU… "Lakini cha kushangaza ni kuwa watu wako busy kuhukumu wenzao kuliko hata huyo mwenye cheo chake, hivi Mungu angetaka kufanya kama wanadamu tunavyofanya tungeangaliana kweli? "Nadhani umefika wakati wa kumuachia mwenye majukumu yake kufanya kazi…tuache kujipa u busy usio wa lazma….!!!

Msanii wa Bongo Movie AVULIWA nguo zote na WACHINA na kisha kuchzewa NYETI zake

Image
MSANII wa Bongo Movie, Devota Mbaga hivi karibuni alipatwa na kisanga cha mwaka baada ya kuvuliwa nguo na maofisa wa uhamiaji alipoenda Hong Kong, nchini China kwa ajili ya shughuli zake za kibiashara. Kwa mujibu wa staa huyo, alifanyiwa kitendo hicho cha kuvuliwa nguo zote na maofisa wa uhamiaji mara alipotua Uwanja wa Ndege wa Hong Kong na kumsachi kwa kuhofiwa kuwa amebeba ‘unga’. Akizungumza na mwandishi wetu kwa njia ya simu, Devota alisema baada ya kuvuliwa, alishikwa sehemu zake za siri kitendo alichokiita ni cha kidhalilishaji. “Ilikuwa ni baada ya kugongewa pasipoti yangu nikaingizwa kwenye kitengo cha polisi wa madawa ya kulevya ambao walinitaka nivue nguo zote ili nikaguliwe,” alisema kwa masikitiko. Msanii huyo alisema mbaya zaidi siku hiyo alikuwa katika mzunguko wake wa mwezi lakini maofisa hao hawakujali. Kama vile haitoshi, Devota alisema kuwa, baada ya kumalizika kwa zoezi hilo maofisa hao walimchezea sehemu za kifuani huku wakimwambia kam

NYALLA, NYAULINGO, NYENZI WASHINDA RUFANI

Image
Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imewarejesha warufani wote watatu katika kinyang'anyiro cha uchaguzi wa Kamati mpya ya Utendaji ya TFF utakaofanyika Oktoba 27 mwaka huu jijini Dar es Salaam. (HM) Samwel Nyalla, Ayubu Nyaulingo na Ayoub Nyenzi walikata rufani mbele ya Kamati hiyo inayoongozwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Bernard Luanda kupinga uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF kuwaondoa katika uchaguzi huo ambapo wote wanagombea ujumbe wa Kamati ya Utendaji kuwakilisha kanda mbalimbali. Akisoma uamuzi wao leo (Oktoba 11 mwaka huu) mbele ya Waandishi wa Habari kwenye ofisi za TFF, Jaji Luanda amesema baada ya kusikiliza hoja za Mrufani Nyalla walipitia Kanuni za Uchaguzi za TFF na kugundua yafuatayo; Ibara ya 10(3) imeweka masharti makuu mawili ya ujazaji wa fomu za kugombea uongozi. Fomu hiyo ni lazima iwe na saini ya mgombea na ni lazima ithibitishwe na viongozi wa shirikisho. Kamati imepitia Kanuni za Uchaguzi ha